Tuesday, June 21, 2011

Askofu Wa TAG Aiponda Bajeti Ya Serikali, Asema Haina Lengo La Kumkomboa Masikini

HUKU wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania hasa wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wakiipinga mapendekezo ya bajeti ya serikali kwwa mwaka wa fedha 2011/2012 iliyowasilishwa bungeni na waziri wa fedha na uchumi Mustafa Mkulo ,askafu wa kanisa la Tanzania Assembulise Of God (TAG) jimbo la Iringa Jonas Mkane (pichani) ameipinga bajeti hiyo kuwa haijalenga kumkomboa mwananchi wa kawaida.

Pamoja na kuipinga bajeti hiyo pia askofu huyo aliitaka serikali kuwashughulikia vikali mafisadi ambao ndio wanafanya watanzania kuishi maisha magumu.

Katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kufungua semina ya wachungaji wa jimbo la Iringa iliyofanyika TAG Mlandege ,askofu Mkane alisema kwa upande wake anaona kuwa bajeti hiyo haijalenga kumkomboa mwananchi wa kawaida .

Alisema kwa upande wake alifikiri kuwa kabla ya kutenga bajeti hiyo serikali inapaswa kushughulika na watu wachache ambao wamekuwa wakiichakaza nchi kwa kuendekeza ufisadi na baada ya hapo kukaa chini na kutenga bajeti ya wananchi itakayowatoa katika dimbwi laumaskini ila kuendelea kutenga bajeti hiyo na kuwakabidhi mafisadi ni kumkomoa mwananchi.

"Mimi nadhani kabla ya kutenga bajeti hiyo serikali inageanza kushughulika na watu wachache ambao wanafanya ufisadi ndani ya Taifa ambao wanafahamika soma zaidi

No comments: