Tuesday, October 30, 2012

Tamwa kuzindua mradi wa kutokomeza unyanyasaji kijinsia

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) kinatarajia kuzindua mradi wao unaojulikana kama ‘mradi wa kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia.’

Uzinduzi huo utafanyika leo katika ofisi za chama hicho, jijini Dar es Salaam, huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Valerie Msoka, malengo ya mradi huo ni kujenga na kuimarisha usawa wa kujinsia na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini.

Malengo ya mradi huo, ambao utazinduliwa kwa ufadhili wa Ubalozi wa Denmark, yanatarajiwa kutekelezwa kwa ushirikiano na mashirika mengine, kama vile Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP), Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (Tawla), Jumuiya ya Wanawake Wanasheria  Zanzibar (Zafela) na Kituo cha Usuluhishi (CRC).

Katika uzinduzi huo, pia elimu kwa wanahabari kuhusu jinsi ya kuibua vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto ndani ya jamii ili hatua za kuvikomesha ziweze kuchukuliwa na vyombo husika, itatolewa.

Mradi huo wa miaka miwili, unatarajiwa kuzinuifaisha jumla ya wilaya 10 za Tanzania Bara na visiwani.

Baadhi ya wilaya hizo, ni Wete, Unguja Mjini Magharibi, Unguja Kusini (Zanzibar); Kisarawe, Newala, Mvomero, Lindi Vijijini, Ruangwa, Kinondoni na Ilala (Tanzania Bara).


CHANZO: NIPASHE

3 comments:

Anonymous said...

With having so much written content do you ever run into any problems of plagiarism or copyright infringement?
My website has a lot of unique content I've either written myself or outsourced but it seems a lot of it is popping it up all over the internet without my agreement. Do you know any methods to help reduce content from being ripped off? I'd definitely appreciate it.


my webpage Desktop Gadgets

Anonymous said...

Gday,
It looks as though we both have a passion
for the same thing. Your blog and mine are very similar.
Have you ever thought of writing a guest post for a similar
website? It will definitely help gain publicity to your website (my website receives a lot of targeted traffic).
If you might be interested, email me. Thank you

Also visit my weblog: Best iPhone App

Unknown said...

nitafurahi zaidi hizi taasisi zikijikita mashuleni, kufanya utafiti kwa wanafunzi, kuna ukatili mwingi sana wa kijinsia unaopelekea wanafunzi kushuka kimasomo.