Monday, December 19, 2011

Uchumi wa Taifa hatarini: Mfumuko wa Bei tishio kwa Serikali, Wafanyabishara na Wananchi

Mfumuko wa Bei umezidi kuongezeka kama taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu inavyoonesha kwamba, wakati mfumuko wa bei mwezi Julai mwaka huu (Bajeti ya mwaka wa Fedha 2011/2012 ilipokuwa inaanza) ulikuwa asilimia 13, umefikia asilimia 19.2 mwezi Novemba. Hii maana yake ni kwamba, Bajeti ya Serikali iliyopitishwa na Bunge mwezi Juni 2011, imepunguza uwezo wa kununua bidhaa na huduma kwa takribani asilimia 6. Hii ni sawa na shilingi 780 bilioni kuyeyuka katika Bajeti katika kipindi cha miezi Minne tu ya utekelezaji wa wake. Kutokana na kasi ya ukuaji wa Mfumuko wa Bei ni dhahiri kwamba, itakapofika mwisho wa mwaka wa Bajeti Serikali itakuwa imepoteza kwa kiasi kikubwa uwezo wa kununua bidhaa na huduma kwa zaidi ya robo ya Bajeti yake.

Hali ni mbaya zaidi kwa wananchi kwani Mfumuko wa Bei za vyakula umekua kwa kasi kikubwa mno. Ofisi ya Takwimu imeonesha kuwa wakati mfumuko wa Bei za vyakula ulikuwa asilimia 14.8 mwezi Julai, umefikia asilimia 24.7 mwezi Novemba 2011. Ukilinganisha na bei za vyakula mwaka 2010, mwananchi amepoteza uwezo wa kununua chakula kwa zaidi ya robo katika ya Novemba 2010 na Novemba 2011. Jumla ya vyakula ambavyo mwananchi alinunua kwa shilingi 10,000 mwaka 2010, sasa atanunua kiwango kile kile kwa shilingi 12,500. Bei za vyakula zimeongezeka kwa kiwango hiki ilhali kipato cha mwananchi aghalabu kipo pale pale. Mwathirika mkubwa ni mwananchi wa kawaida wa kijijini ambaye mapato yake ni kidogo na hivyo sehemu kubwa huyatumia kununua chakula.

Ukiangalia kwa undani utakuta mfumuko wa bei wa bidhaa kama mchele, sukari, nyama na samaki umekua maradufu. Bei ya mchele imekua kwa asilimia 50, sukari asilimia 50, nyama asilimia 30 na Samaki kwa takribani asilimia 40. Bidhaa hizi zote ni muhimu sana kwa afya ya binadaamu na hasa watoto kwa upande wa vyakula vya protini. Tusipokuwa makini na kupata majibu sahihi ya tatizo la mfumuko wa bei za vyakula, wananchi wengi na hasa watoto watapata utapiamlo na Taifa kuingia gharama kubwa katika kuwapatia huduma ya afya.

Kwa upande wa bidhaa zisizo za vyakula, mfumuko wa bei wa mafuta ya taa na gesi asilia unapaa kwa kasi kama moto wa nyikani. Wakati mafuta ya taa yamepanda bei kwa asilimia 71 katika ya mwezi Novemba mwaka 2010 na mwezi Novemba 2011, bei ya gesi asilia imepanda kwa asilimia 35. Madhara ya hali hii ni makubwa mno maana wananchi watakimbilia kwenye matumizi ya mkaa na kuni, hata hivyo bei za mkaa zenyewe zimepanda kwa asilimia 24. Kwa hali hii, na kutokana na ukweli kwamba wananchi wengi wa Tanzania wapo kwenye mpaka wa umasikini na daraja la kati chini, juhudi za muongo mzima za kupunguza umasikini zitafutwa ndani ya mwaka mmoja tu.

Mfumuko wa Bei unasukuma Watanzania wengi zaidi kwenye dimbwi la umasikini, unapunguza uwezo wa Serikali kutoa huduma za jamii kupitia Bajeti na hata kutimiza mipango ya miradi ya maendeleo kama miundombinu ya barabara, umeme, bomba la gesi, madaraja nk. Mkakati mahususi unatakiwa kubadili hali hii. Hatua zifuatazo zinapendekezwa ili kuuhami uchumi na kupunguza upandaji wa kasi wa gharama za maisha.

1. Kuongeza uzalishaji wa chakula kwa kuweka mbinu za kukuza uchumi wa vijijini ni njia mojawapo endelevu ya kupunguza mfumuko wa Bei hapa nchini. Serikali sasa iache maneno matupu kuhusu sekta ya uchumi vijijini kwa kuelekeza nguvu nyingi huko. Serikali iruhusu na ivutie kwa kasi na kutoa vivutio kwa wazalishaji binafsi wa Sukari na mpunga katika mabonde makubwa. Waziri wa Kilimo na Maafisa wake watoke Ofisini na kuhimiza uzalishaji mashambani, fedha zielekezwe kujenga miundombinu ya barabara vijijini.

Vyakula vilivyolundikana mikoa ya Mbeya, Iringa na Rukwa ambapo Serikali iliahidi kununua na kutotimiza ahadi yake vinunuliwe mara moja na kusambazwa mikoa yenye shida ya chakula kama Mwanza, Mara, Kagera na mikoa ya Kaskazini. Chakula kukuta msimu mwingine katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ni kashfa kubwa kwa Serikali na inaonesha Serikali isivyokuwa makini na maisha ya wananchi.

Wakati huu ambapo tunaweka mikakati ya kuongeza uzalishaji wa chakula, Serikali inunue chakula cha kutosha na hasa mchele na sukari kutoka nje na kukisambaza kwenye soko ili kupunguza upungufu wa bidhaa (scarcity) katika masoko.

Mfumo uliotumika kununua Sukari tani laki moja hivi karibuni usitumike tena kwani ulizaa rushwa ya hatari na ufisadi ambao haujaripotiwa kwenye kutoa vibali. Wizara ya Kilimo iruhusu wauzaji kutoka nje walete sukari nchini moja kwa moja na kununuliwa na Bodi ya Sukari kisha kuiuza kwa wauzaji wa Jumla. Mfumo wa kutoa vibali umeonesha kutokuwa na tija na kwa kweli kunufaisha maafisa wachache wa Wizara ya Kilimo na Bodi ya Sukari.

2. Kitengenezwe kiwanda cha kutengeneza gesi ya matumizi nyumbani (LPG extraction plant) kwa haraka ili kupunguza bei ya gesi, kuepuka kuagiza gesi kutoka nje na hivyo kuokoa fedha za kigeni na kutengeneza ajira hapa nchini. Kupanda kwa bei ya gesi asilia kunatokana na kwamba Tanzania inaagiza gesi hii yote kutoka nje ilhali malighafi ya kutengeneza gesi ipo hapa Tanzania na kwa kweli huchomwa moto (flared). Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini liingie ubia na kampuni Binafsi ili kuwekeza katika kiwanda cha kuzalisha gesi hatimaye kushusha bei na hivyo kuwezesha wananchi wengi zaidi kutumia gesi kwa matumizi ya kupikia n.k, hivyo kutunza mazingira.

3. Ushuru wote unaokusanywa kwenye Mafuta ya Taa upelekwe Wakala wa Nishati Vijijini ili kufidia kupanda kwa bei ya mafuta ya Taa. Mfumuko wa Bei katika bidhaa ya mafuta ya taa unatokana na uamuzi wa kuwianisha bei ya mafuta ya taa na diseli ili kuondoa tatizo la uchakachuaji wa mafuta. Tatizo limeondoka (au hatulisikii tena) lakini wananchi wanaumia sana. Uamuzi sahihi wa kisera ni kupanua huduma za umeme vijijini kwa kuipa fedha zinazotokana na ushuru wa mafuta ya taa Wakala wa Umeme Vijijini. Usambazaji wa Umeme Vijijini utaongeza shughuli za kiuchumi vijijini, kukuza uchumi wa vijijini, kuongeza mapato ya wananchi kwa kuongeza thamani za mazao yao na hivyo kupunguza athari za mfumuko wa bei.

4. Sera ya Matumizi ya Serikali iangaliwe upya kwa kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi yasiyo ya lazima, na kuelekeza fedha nyingi zaidi katika uwekezaji umma (public investments). Matumizi Mengineyo ya Serikali yanaongeza fedha kwenye mzunguko ama kwa kulipa watu wachache stahili mbalimbali kama posho n.k au kwa kununua bidhaa na huduma bila mpango, na hivyo kusukuma bei kuwa juu kinyume na uhalisia wa soko. Tafiti za mfumuko wa Bei Tanzania zinaonyesha kwamba sera za fedha na zile za matumizi (monetary and fiscal policy) zina nafasi kubwa katika kukuza mfumuko wa bei. Hivi sasa nakisi ya Bajeti inayopelekea Serikali kukopa kwa kwa kiwango kubwa inapandisha gharama za viwanda kukopa mitaji ya muda mfupi na hivyo kuongeza gharama za uzalishaji na kasha bei za bidhaa. Wizara ya Fedha ambayo mpaka sasa imekaa kama imeishiwa namna ya kufanya, inapaswa kuamka na kutoa maelekezo mapya kwa Wizara, Idara na Wakala za Serikali kuhusu namna ya kubana matumizi na kuziba mianya yote ya kukwepa kodi.

Hitimisho

Serikali imeonesha udhaifu mkubwa sana katika kusimamia uchumi katika nusu ya kwanza ya Bajeti ya mwaka 2011/2012 ambayo pia ni Bajeti ya kwanza ya kipindi cha pili cha Serikali ya awamu wa Nne. Kuna hatari ya dhahiri kwamba ifikapo mwezi Januari 2012 tutakuwa tumerejea mfumuko wa Bei wa kiwango cha mwaka 1992 (21.9%). Tusipochukua hatua za haraka tutafikia na hata kuzidi mfumuko wa Bei kiwango cha juu kabisa ambacho kilifikiwa mwaka 1994 (33%) na hivyo viwanda kushindwa kukopa kwenye Mabenki kwa mahitaji yao ya haraka ya mitaji ya muda mfupi, wazalishaji wadogo kushindwa kulipa mikopo yao kwenye Taasisi za fedha na hivyo kufunga uzalishaji, Shirika la Umeme kushindwa kabisa kulipa gharama za mafuta ya kuendesha mitambo na kipato cha mwananchi kutomudu gharama za za kila siku. Uchumi utadorora kabisa. Taifa litakuwa hatarini.

Wizara ya Fedha, Benki Kuu ya Tanzania na Wizara ya Kilimo na Chakula iamke kuhami uchumi dhidi ya adui namba moja, Mfumuko wa Bei. Huu sio wakati wa kupiga porojo, viongozi wafanye kazi zao, Wananchi wajitume.

Inabidi sasa turejee kauli mbiu za miaka 50 iliyopita za Uhuru ni Kazi. Tuseme Demokrasia ni Kazi. Demokrasia sio lelemama.

Ndg. Kabwe Zuberi Zitto, Mb

Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Waziri Kivuli Fedha na Uchumi

18 Disemba 2011

Friday, December 16, 2011

TATHMINI YA GDSS YA MWAKA 2011


SEMINA ZA JINSIA NA MAENDELEO

UNAKARIBISHWA KATIKA MFULULIZO WA SEMINA ZA JINSIA NA MAENDELEO (GDSS) KILA JUMATANO, AMBAPO WIKI HII TGNP WATAWASILISHA:

MADA: TATHMINI YA GDSS YA MWAKA 2011

Lini: Jumatano Tarehe 21 Disemba, 2011

Muda: Saa 09:00 Alasiri – 11:00 Jioni

MAHALI: Viwanja vya TGNP, Barabara ya Mabibo Karibu na Chuo cha Taifa Cha Usafirishaji Mabibo Sokoni

WOTE MNAKARIBISHWA

Thursday, December 15, 2011

Wanafunzi 43 wafukuzwa UDSM

CHUO Kikuu cha Dar es Salaam, Sehemu ya Mlimani (UDSM), kimewafukuza chuo jumla ya wanafunzi 43 waliokuwa wamesimamishwa masomo wakisubiri kumalizika kwa kesi zilizoko mahakamani pamoja na kuwa viranja wa vurugu zilizotokea chuoni hapo mwanzoni mwa wiki hii.

Aidha, chuo hicho kimewasimamisha wanafunzi tisa kutokana na makosa hayo hayo ambapo wanasubiri uamuzi wa Baraza la Chuo na iwapo watakuwa na hatia, adhabu stahiki itafuatwa.

Kadhalika kimesema kitafanya mawasiliano na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) ili wanafunzi waliofukuzwa, wasipate tena mkopo wa Serikali wala kuruhusiwa kudahiliwa tena katika chuo chochote cha umma.

Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala alitoa uamuzi huo jana Dar es Salaam ambo ni wa Baraza la Chuo Kikuu kuhusu vurugu za wanafunzi ambazo zilisababisha uvunjifu wa amani na ukosefu wa utulivu chuoni hapo.

Baada ya kumaliza kusoma uamuzi huo mbele ya waandishi ya habari, ulibandikwa kwenye kuta za matangazo chuoni hapo na kila mwanafunzi alifika na kusoma.

Kuhusu wanafunzi waliofukuzwa, Profesa Mukandala alisema wako wa mwaka wa kwanza hadi wa tatu, lakini wengi wa waliofukuzwa ni wa mwaka wa pili na wa tatu na ambao wanasoma masomo ya sanaa.

Profesa Mukandala alifafanua kuwa kati ya wanafunzi 51 waliokuwa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam Novemba mwaka huu wakikabiliwa na makosa ya kufanya mkusanyiko usio halali na kukaidi amri ya Jeshi la Polisi, 43 kati yao ndio waliofukuzwa, watatu sio wanafunzi wa chuo hicho, tisa hawajasikilizwa na Baraza la Chuo hicho na kutolewa mapendekezo.

Aidha, alisema matukio yaliyojiri Jumatatu na Jumanne wiki hii ni mwendelezo wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyoanza mwanzoni mwa Novemba mwaka huu ambapo kila mara vitendo hivyo vilianzishwa na kikundi kidogo cha wanafunzi na hatimaye kupata wafuasi katika kuvuruga shughuli za chuo.

Makamu Mkuu wa Chuo alisema madai ya wanafunzi waliokuwa wakiendesha vurugu hizo, yamekuwa yakibadilika kila kukicha ambapo mwanzo walidai mikopo kwa ajili ya wanafunzi waliochaguliwa katika mwaka huu wa masomo na ambao hawakupata mikopo.

Alisema baadaye dai kubwa likawa ni kuachiwa huru wenzao waliokamatwa na kufunguliwa mashitaka kutokana na kuendesha maandamano kinyume cha sheria na kukaidi amri ya Jeshi la Polisi ya kutawanyika.

Profesa Mukandala alisema katika siku mbili za vurugu madai ya awali yalikuwa kuondolewa kwa adhabu za kinidhamu walizopewa wenzao wachache kwa mujibu wa Kanuni na Sheria za Chuo, lakini baadaye wakageukia suala la kupatiwa fedha za malazi na chakula kuanzia Desemba 10, mwaka huu.

Kuhusu vurugu zilizotokea kwa siku hizo mbili, alisema kikundi hicho kiliingia madarasani na kuwatimua wenzao kwa kutumia fimbo na wakati mwingine kuwamwagia maji wahadhiri waliowakuta wakifundisha, kuziba lango kuu la kuingilia jengo kuu la utawala na kusababisha shughuli ndani ya jengo hilo kusimama.

Alisema mbaya zaidi kikundi hicho kilikwenda kantini na kuendesha vurugu kubwa, ikiwemo kuwamwagia wenzao chakula walichokuwa wanakula, kumwaga mavumbi katika chakula kilichokuwa kikisubiri kugawiwa, kuwapiga wafanyakazi wa kantini, kuharibu majokofu na kushambulia mabasi yapitayo eneo la chuo na hata yale yanayotoa huduma za usafiri kwa wanafunzi wanaoishi katika hosteli ya Mabibo.

Kuhusu uharibifu wa mali, tayari wamefungua jalada Polisi na kwamba kwa vile wanafunzi waliohusika wanafahamika watawajibika katika hilo.

Tuesday, December 13, 2011

Wanafunzi: Mafisadi CCM Wang’olewe

WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari Kwiro ya mjini Mahenge wilayani Ulanga, Mkoa wa Morogoro, ambao ni wanachama cha Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wamewaomba viongozi ngazi ya juu wa CCM kuwawajibisha na kuwavua magamba mafisadi wote wanaotuhumiwa kwa kashfa mbalimbali.

Wamesema kutowawajibisha kwa kuwavua magamba mafisadi hao, kutaendelea kuwafanya wananchi waendelee kutokuwa na imani na CCM pamoja na Serikali yao kutokana na viongozi wenye dhamana kushindwa kuchukua maamuzi magumu ya kuwavua magamba waliotuhumiwa

ufisadi. Wanafunzi hao ambao wengi wao ni wa kidato cha tano na sita, walisema hayo kwa nyakati tofauti hivi karibuni mjini Mahenge mbele ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Sarah Msafiri, ambaye pia ni Mbunge wa Vijana kwa tiketi ya UVCCM.

Mjumbe huyo wa NEC Taifa alifanya ziara katika wilaya za Mkoa wa Morogoro ili kukutana na vijana kwa lengo ya kupata maoni na changamoto zinazolikabili kundi hilo ikiwa pamoja na kutoa misaada ya vifaa vya aina mbalimbali vitakavyotumiwa kuanzisha miradi ya maendeleo
ya vijana.

Akizungumzia dhana ya kujivua magamba, mwanafunzi wa kidato cha sita, Frank Mauya, alisema kitendo cha viongozi wa juu wa CCM kutekeleza maamuzi yaliyopitishwa na kujivua gamba kwa mafisadi kunakishusha chama chini na pia kuendelea kuchafuliwa.

“Ni kweli hawa aliotajwa kwa kashfa ya ufisadi, ni watuhumiwa tu, lakini kuendelea kuacha kwa sababu ya hizo ni tuhuma pekee, kunaendelea kuididimiza CCM na wananchi kupoteza imani ya Chama na Serikali,” alisema mwanafunzi huyo.

Naye Nurdin Makonya pia wa kidato cha sita, alisema hivi sasa Umoja wa Vijana wa CCM unatumika kama kivuli cha baadhi ya wakubwa ndani ya CCM ya kufanya kampeni za kuwania urais wa mwaka 2015.

“Sisi wanafunzi ambao ni wanachama wa UVCCM tunaona Umoja wetu unatumika vibaya kwa
baadhi ya viongozi wa ngazi ya juu wanapotoa matamko ambayo hayajengi umoja wa chama,” alisema Makonya.

“Kinachoonekana matamko yao yana mwelekeo wa kuwagawa wanachama na hilo ni kutokana na sababu ya mbio za urais katika uchaguzi mkuu wa 2015,” aliongeza mwanafunzi huyo.

Hata hivyo, alisema katika uchaguzi ujao wa ndani ya jumuiya za chama hicho, wenyeviti wa Umoja huo watakaochaguliwa pamoja na wajumbe wao, wasiwe watu wa kuandaliwa kwa ajili ya kuwachagua marais wajao, bali wawe ni chachu ya kupigania maendeleo ya kiuchumi na
kijamii kwa kundi la vijana nchini.

Akijibu baadhi ya hoja za wanafunzi hao, Mjumbe huyo wa NEC Taifa alisema dhana ya kujivua gamba bado ipo pale pale ni kuanzia kwa viongozi wa ngazi ya Taifa hadi wale wa chini na kinachohitajika ni ushahidi unaojitosheleza kuwafikisha mahakamani.

“Zipo tuhuma za ufisadi na endapo atajitokeza mtu mwenye ushahidi auwasilishe kwa viongozi
wa juu wa CCM na hao wanaotuhumiwa watafikishwa mahakamani ili wawajibishwe,” alisema Msafiri.

Hata hivyo, aliwataka vijana nchini wasikubali kutumiwa na makundi ambayo yana mwelekeo wa kuifanya nchi isitawalike na kuwasihi wajitokeze kwa wingi kutoa maoni ya uundwaji wa Katiba mpya mara Tume ya kukusanya maoni itakapoteuliwa na kuanza kufanya kazi mapema Januari mwakani.

Serikali Yasimama Kidete Kupinga Ushoga

SERIKALI imepinga kwa nguvu zote na kukataa mapendekezo manne yaliyotolewa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa yakiwemo ya ndoa za jinsi moja, tohara kwa wanawake, mahari na ndoa za mitala ambayo yanakwenda kinyume cha misingi ya maadili,
utamaduni, mila na desturi za Watanzania.

Mapendekezo yaliyokataliwa na Serikali ya Tanzania yaliyoamuliwa na Baraza hilo, yalilenga kuruhusu haki ya ndoa za jinsi moja “ushoga,” kufutwa kwa ndoa za mitala (mke zaidi ya mmoja), kufuta utoaji wa mahari wakati wa kuoana pamoja na tohara za wanawake.

Mapendekezo hayo yalifikiwa kwenye mkutano wa Baraza la Haki za Binadamu la UN uliofanyika ,Oktoba mwaka huu mjini Geneva nchini Uswisi, baada ya kujadili taarifa za nchi mbalimbali kuhusu utekelezaji wa haki za binadamu kwenye nchi zao zilizowasilishwa Julai mwaka huu.

Kukataliwa kwa mapendekezo hayo manne kati ya 53 yanayofanyiwa uchambuzi wa kina kwa
kuhusisha wadau mbalimbali wakiwemo wanasheria kutoka wizara mbalimbali, kumelenga kudumisha utamaduni, maadili, mila na desturi za Watanzania kwa vile mapendekezo hayo ni pandikizi, si ya msingi na yameletwa kutaka kuyahalalisha.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, alisema hayo jana mjini hapa wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua warsha ya siku tatu ya maofisa wa Serikali kutoka wizara mbalimbali na wakuu wa idara zake ya kupitia, kujadili na kutoa mapendekezo yao juu ya taarifa ya mapendekeo 153 yaliyopitishwa na Baraza hilo.

Kwa mujibu wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, nchi mbalimbali ziliwasilisha taarifa zao zinazohusu Haki za Binadamu kwenye Baraza la Umoja huo Julai mwaka huu, ambapo mapendekezo 153 yaliyoamuliwa na Baraza hili yakiwemo manne ambayo Serikali ya Tanzania
imeyakataa moja kwa moja.

Masaju alisema Serikali imekubali mapendekezo 96 wakati mapendekezo 53 hayajakubaliwa na yatawasilishwa kwa wadau ili kuwashirikisha waweze kuyajadili ili kufikiwa makubaliano ya pamoja kabla ya kuwasilishwa tena kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.

“Katika majadiliano juu ya mapendekezo ya Baraza la Umoja wa Mataifa, yaliyofikiwa 153, ambapo mapendekezo 96 yameafikiwa na kuungwa mkono ya Serikali ya Tanzania,” alisema Masaju na kuongeza: “Lakini mapendekezo 53 bado hayajafikiwa, ndiyo yanapaswa kwanza kujadiliwa na wadau wakiwemo watumishi wa Serikali ambayo yanagusa katika sekta zao, yanahitaji kuungwa mkono na wananchi, lakini haya manne tumeyakataa kabisa,” alisema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Alisema Serikali imekataa pendekezo la kuingizwa kuwa ni jambo la haki za binadamu la kuwa na ndoa za jinsi moja kwa kuwa jambo hilo ni kwenda kinyume cha sheria za nchi na haliwezi kukubaliwa na jamii ya Watanzania pamoja na Waafrika kwa ujumla.

Pia Serikali imekataa kufuta ndoa za mitala ambazo zimekuwepo kulingana na msingi wa imani za dini na utamaduni wa baadhi ya makabila nchini, kama ilivyo kwa pendekezo la kufuta mahari wakati wa kuoana.

Alisema mila na desturi za makabila ya Tanzania, moja ya msingi wake ni wakati wa kuoana mke na mume, suala la mahari ni sehemu ya utamaduni ambao ukoo unaooa unatakiwa kutoa mahari kabla ya kufungwa ndoa, hivyo jambo hilo haliwezi kufutwa.

Lakini kwa upande wa tohara kwa wanawake, tayari Serikali ya Tanzania ililipiga marufuku kuanzia mwaka 1998, hivyo imeliunga mkono kwa kuwa Tanzania inazuia vitendo vya kuwafanyia tohara wanawake.

Pamoja na hayo, alisema maamuzi ya mapendekezo 53 yaliyoamuliwa kujadiliwa kwanza na
wadau pamoja na wataalamu wa sheria kutoka wizara mbalimbali yanatakiwa kuwasilishwa
makubaliano yake katika Baraza hilo la Umoja wa Mataifa kabla Mkutano wa 19 wa Haki za Binadamu utakaofanyika Machi mwakani.

Alisema Tanzania ni nchi inayotekeleza na kusimamia misingi mizuri ya haki za binadamu kwa kutoa uhuru wa kujieleza, uhuru wa vyombo vya habari, uwakilishi wa jinsia zote katika maamuzi na usawa wa binadamu.

Naye Mwakilishi wa Kamishina wa Haki za Binadamu katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki wa UN, Musa Gassama, aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa kusimamia vyema haki za binadamu kwa njia ya ushirikishwaji wa makundi na taasisi nyingine.

Hivi karibuni, Tanzania ilieleza kwamba haiko tayari kupokea misaada yenye masharti au shinikizo kuhusu kuruhusu ndoa za jinsi moja baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron kutoa tamko hilo akiwa Australia.

Marekani nayo imeonesha dhamira kama hiyo ya kufuta misaada kwa nchi zisizoruhusu ndoa ya jinsi moja ambazo kwa mujibu wao, ni suala la haki za binadamu.

Monday, December 12, 2011

Land, Labour And Livelihoods: Tanzanian Women’s Struggles

FRIDAY FILE: Land, labour and livelihoods were the themes of the 2011 Gender Festival in the East African nation of Tanzania. Organized by the Tanzania Gender Networking Programme (TGNP), the Festival brought together about 4000 predominantly grassroots women’s rights and gender equality advocates over four days.

By Kathambi Kinoti

The Gender Festival was founded by TGNP in 2001 as a space for Tanzanian women’s rights advocates to learn, network and strategize for collective action. It is held every two years and past themes have included land ownership rights, poverty eradication, structural frameworks that foster inequality and critiquing the capitalist economic model.

In her keynote address at the 2011 Festival, Prof. Dzodzi Tsikata, Head of the Centre for Gender Studies and Advocacy (CEGENSA) at the University of Ghana, drew attention to the intricate and gendered links between land, labour, livelihoods:

“The importance of land and labour rights for … livelihoods in sub-Saharan Africa is on account of the predominantly agrarian nature of livelihood activities, which is the result of the failure of agrarian transformation in much of Africa… [T]he low technological base of agriculture makes labour a critical factor…[B]eyond agriculture, land has a wide array of uses in the organisation of livelihoods (for housing, for business premises and as a source of labour, technologies and inputs; fuel, medicinal plants, naturally growing resources such as Shea, fruit etc which are harvested for sale). As well, land is the basis of social and political power, and therefore at the heart of gender inequalities in the control of resources."

Land

Dispossession and displacement was a dominant theme at the Gender Festival. Throughout Tanzania, women’s rights activists report widespread unfair acquisition of land, mainly by foreign investors, such as the government of the United Arab Emirates (UAE) and European and Asian corporations such as Bioshape and Sun Biofuel, frequently without the informed consent of local populations, and with the complicity of the Tanzanian government. Land is acquired for the purposes of growing food crops for the home markets of these foreign governments or corporations; to grow biofuel crops to supplement and potentially replace fossil fuels as a key source of energy in the European Union; to extract minerals and in some cases, simply to acquire land for tourism interests. Land grabs have emerged as a prominent and urgent challenge facing Tanzanians, with their rights being subordinated to the interests of foreign governments and corporations who are acquiring land to ensure food, energy or economic security.

For instance, women from the pastoralist Maasai community from Loliondo in north-eastern Tanzania who attended the Festival recounted the events of 2009, when government forces evicted their community from their land and burnt their houses. During the operation the residents were beaten, women were raped and over 3000 people were left homeless. This was done to clear the area for a company from the UAE who had acquired the land as a hunting reserve for tourists.

Elsewhere in the country land has been acquired for the cultivation of food and biofuel crops and for the extraction of minerals. In Shinyanga province, land was appropriated for a large-scale mining operation and a piped water scheme has been developed to only benefit the mining project. The pipeline brings water from Mwanza, a town on Lake Victoria to Shinyanga. While the local populations who live along the route of the pipeline have no access to that water and women have to walk many kilometres daily to fetch water and only have limited access to water from rivers and streams. A similar situation occurred in the Hanang area where land was acquired to grow onions for export, where an irrigation scheme was developed and yet local women still have to walk long distances in search of water for household use.

Women’s rights activists at the Gender Festival highlighted that there are numerous situations where the Tanzanian government has allowed foreign investors to acquire land and other natural resources at the expense of its own citizens.

Livelihoods challenges

Over the past decade Tanzania’s economic growth rates have been relatively high, but this growth has not translated into better livelihoods for the majority of women

There is little protection of the labour rights of poor people and, as Tsikata stated, those whose most important resource is their labour are in a crisis because it does not bring sufficient returns to enable them have decent livelihoods and yet their labour may be all they have to offer. There is also the possibility that they may be made redundant by technology and ‘superior’ education or qualifications; or that they become victims of failed business models. For instance, a failed biofuel project started by a British company in Tanzania’s Kisarawe District, which had acquired one quarter of a village’s land, left hundreds jobless and landless with nowhere to turn to.

Tanzanian women – like women the world over - are involved in immensely labour-intensive activities: bearing and rearing children, cooking, cleaning, caring for the sick and elderly, farming, selling farm produce, and so on, but this work is not adequately valued in economic terms

In “Food Sovereignty: Exploring debates on development alternatives and women’s rights,” Pamela Caro writes:

“Feminists and researchers of gender relationships assert that a patriarchal ideology is at the centre of capitalist trade and export trends, which aim to continuously increase production in search of greater profits, under the assumption that economic, productive and reproductive systems are not autonomous.”

This sentiment was affirmed over and over at the Gender Festival. Women spend hours fetching firewood and water for household use, caring for immediate and extended family members, and are expected to participate in the free-market where their labour is commodified without regard to their non-market reproductive labour. Women‘s productive and reproductive energy is a mainstay of the capitalist economy. Yet it remains unacknowledged and unrewarded, and even worse, it often deprives women of the fruits of their extensive labour.

Exploring solutions to precarious situations

The Gender Festival was a space for thousands of women and women’s rights advocates to explore solutions to the socio-economic struggles they face everyday: poverty, poor socio-economic status, land grabs and disenfranchisement.

Tsikata says: “Increasingly, popular struggles [in Africa] are being led by NGOs, and mass mobilization has been replaced by policy advocacy fragmented in single issues.” The Gender Festival, on the other hand, represents a powerful mobilization of grassroots women from all the regions of Tanzania and a potentially powerful force for change.

Maasai women from Loliondo are at the forefront of their communities in challenging their eviction from their homes. Representatives of the community at the Gender Festival reaffirmed their commitment to resisting the loss of their land, property and livelihoods to foreign investment. They have vowed not to leave Loliondo; where they were born, raised and have borne their children. Their shared experiences can provide learning for other communities affected by land grabs and displacement.

At the Festival women from Nronga village also shared their experiences of taking control of their livelihoods, by starting a women-only dairy cooperative 24 years ago. When an investor tried to take control of water resources in the area, the women resisted and formed a dairy cooperative and have now generated enough income to build a secondary school and have achieved 100% primary school enrolment. They have challenged the traditional saying “The man owns the cow, while the woman owns the milk.” Now, they own all the proceeds from dairy farming and are putting them to use in developing their community.

Women at the Festival also resolved to get involved more powerfully in the upcoming Tanzanian constitutional reform process, lessons having been gleaned from neighbouring Kenyan women’s steadfastness and solidarity to secure significant gains for women’s rights in the 2010 constitution and land policies.

The Gender Festival is a unique space for grassroots women in Tanzania to share experiences and strategies, not only from within the country, but also regional and international movements. This year provided yet another opportunity for participants to define, share and strategize about their continuing struggles over land, labour and livelihoods.

Thursday, December 8, 2011

Sheria Kandamizi Zirekebishwe -Waziri

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Celina Kombani amesema iko haja ya kufanya utetezi na ushawishi kwa kurekebisha sheria na sera zote ambazo haziendani na mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu zikiwemo za wanawake.

Alisema hayo katika uzinduzi wa machapisho mbalimbali ya Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) uliofanyika katika ofisi za kituo hicho zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Alisema wakati huu ambapo bado kuna migongano mingi ya sheria, wameona vyema ukafanyika ushawishi na marekebisho ya pamoja katika mkataba wa kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake, kama ilivyokubaliwa katika maazimio ya ulingo wa Beijing, Malengo ya Maendeleo ya Millenia na mikataba mingine ya kimataifa ambayo nchi imeridhia.

Alisema mwanamke amekuwa ni mtu wa kunyanyasika katika suala zima la mirathi kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo mila na desturi potofu zinazoendelea kutumika nchini.

Awali Mkurugenzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya WLAC, Nakaziel Tenga alisema machapisho yaliyozinduliwa ni sehemu ya harakati za kumkomboa mwanamke katika mfumo dume uliogubika jamii ambapo mwanamke amekuwa hapati thamani iliyo sawa na mwanamume.

Wednesday, December 7, 2011

Wanawake Waaswa Kutonyanyasa Kijinsia

WANAWAKE wanaowanyanyasa waume zao kijinsia wametakiwa kuacha tabia hiyo mara moja kwa kuwa siyo desturi kwa mwanamke kujihusisha na matendo maovu yakiwemo ya ukatili wa kijinsia.

Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete aliyasema hayo jana Dar es Salaam wakati wa akizindua kampeni ya kupinga unyanyasaji wa kijinsia ya ‘Kuwa Mfano wa Kuigwa’ na Mradi wa CHAMPION.

“Ipo dhana potofu kuwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia hufanywa dhidi ya wanawake tu, hii si kweli, wapo baadhi ya wanawake wachache ambao hudiriki kufanya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wenza wao,” alisema Mama Kikwete katika hotuba yake
iliyosomwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani.

Mama Kikwete alisema wanawake hao yawezekana wanawanyanyasa waume zao kutokana na kipato chake au uduni wa maisha na ambao hufanya ukatili huo ni wabaya zaidi ya wanaume kwa kuwa hudhamiria vitendo hivyo bila huruma.

“Unyanyasaji wa kijinsia ni moja ya changamoto kubwa ulimwenguni na zipo sababu balimbali zinazosababisha unyanyasaji wa kijinsia lakini kwa hapa nchini mila potofu na hali duni ya uchumi ni moja ya vichocheo vya kuwapo kwa unyanyasaji wa kijinsia,” alisema.

Alisema kwa mujibu wa utafiti, asilimia 44 ya wanawake wameshawahi kukutana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kutoka kwa wenza wao, hivyo unahitajika ushiriki wa pamoja kukomesha hali hiyo.

“Pamoja na takwimu hizo, lakini jambo la kutia moyo ni kwamba zaidi ya asilimia 50 ya wanaume hawashiriki katika vitendo vya kunyanyasa wenza wao. Kwa mantiki hiyo ni vema kuwatambua wanaume hao kuwa ni mfano wa kuigwa na wengine,” aliongeza Mama Kikwete.

Aliwataka kina baba kutumia ushawishi wao kwa wenza wao na jamii kwa ujumla bila ya kutumia mabavu kuamsha majadiliano juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, kuvipinga kwa nguvu zote na kuonesha mfano kwa wenzao katika kupinga unyanyasaji wa kijinsia.

Alisema anategemea kila mmoja ataunga mkono kampeni hiyo kwani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vinakwamisha na kudumaza mchango wa wanawake katika shughuli za uchumi na maendeleo ya nchi.

Pia aliishukuru Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa (USAID) Tanzania na Engenderhealth- Champion kwa juhudi zao za kukomesha unyanyasaji wa kijinsia na kuupongeza Mradi wa CHAMPION na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa kufanikisha kampeni hiyo.

Spika Atetea Posho Mpya

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda amekiri nyongeza ya posho za vikao vya wabunge kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000 kwa siku na kusema imesababishwa na kupanda kwa gharama za maisha mjini Dodoma.

Ametetea uamuzi wa nyongeza hizo kuwa una nia njema ya kuwawezesha wabunge wamudu
gharama za kuwawakilisha wananchi vizuri, kwa kuwa mishahara wanayolipwa ni midogo ikilinganishwa na gharama wanazoingia wakiwa bungeni.

Makinda alisema hayo Dar es Salaam jana baada ya kuzindua Ripoti ya Maendeleo ya
Wanawake Duniani kuhusu Haki kwa mwaka 2011.

Ripoti hiyo imeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Jinsia na Uwezeshaji kwa Wanawake
(UN Women) na Shirika la UN la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA).

Makinda alitaja siku ambazo wabunge walilipwa posho hizo mpya kuwa ni Novemba 08, 09
na 11, mwaka huu pamoja na wiki ya pili ya Bunge la Mkutano wa Tano na kueleza kuwa
pasipo kuwa na vikao vya Bunge, wanacholipwa ni mshahara pekee.

“Ni vyema jamii ifahamu kuwa wabunge hawalipwi fedha nyingi kama inavyozungumzwa
na baadhi ya watu na kwamba, wanachobaki nacho baada ya makato ya mkopo wa gari na kodi, hakiwatoshi kumudu gharama zote wawapo Dodoma kuhudhuria vikao vya Bunge, kama vile malazi na nyinginezo,” alisema Makinda.

Akichanganua kipato cha mbunge kwa mwezi, Makinda alisema mbunge analipwa Sh
milioni 2.3 tu kama mshahara na katika malipo hayo, hukatwa Sh 700,000 za kodi na Sh
800,000 za mkopo wa gari. Kwa hesabu hizo, mbunge kwa mwezi anabakiwa na Sh 800,000 tu.

“Hebu fanyeni hesabu muone katika mshahara huo mbunge anabaki na shilingi ngapi?

Na mkumbuke pia kuwa fedha hiyo ndiyo anayoitumia kwa gharama za kutengeneza gari lake endapo litapata matatizo, mafuta na kwa ajili ya matumizi mengine kama atataka kwenda jimboni na kwingineko kwa sababu za kikazi,” alisema Makinda ambaye ni Mbunge wa Njombe Kusini (CCM).

Alisema posho ya Sh 70,000 isingemsaidia kumudu gharama hata za chumba kwa sababu
zimekuwa juu mno kutokana na mji wa Dodoma kuwa kituo cha elimu ya vyuo vikuu kwa sasa.

“Kila kitu kimepanda bei na kwa bahati mbaya nyumba zile za CDA (Mamlaka ya Ustawishaji
Makao Makuu) zilizokuwa nafuu zilichukuliwa na wabunge wa Bunge la Tisa kwa
mikataba binafsi na wengi hawajazirudisha hadi sasa ili kuwezesha wapya kuzipangisha,”
alisema Spika.

Kitendo hicho cha wabunge wa Bunge la Tisa kung’ang’ania nyumba za CDA kwa mujibu wa Makinda, kimesababisha wabunge wapya wapange hoteli ambako hutozwa fedha nyingi tofauti na kipato wanachokipata.

“Pia sio kweli kwamba posho hizo zinatolewa kinyemela kwa sababu zilipitishwa katika vikao halali na kukubaliwa kuwa atakayezipata ni yule mbunge atakayehudhuria vikao vya Bunge asubuhi mpaka vitakapoahirishwa tu.

“Atakayesaini asubuhi na jioni ndiye atakayekuwa na uhalali wa kulipwa. Hata Kabwe Zitto anayezizungumzia, hajapewa hata senti moja kwa kuwa hakuwepo vikaoni, alikuwa mbali,” alisisitiza Makinda na kuongeza kuwa mshahara huo ni wa tangu mwaka 2003 na haujawahi kufanyiwa marekebisho yoyote hadi sasa.

“Sioni kama kuna malipo ya kustaajabisha umma kwa sababu hali halisi inajionyesha wazi, mazingira ya gharama za maisha nazo zinaonekana kiasi cha kushawishi kuwepo kwa nyongeza hiyo katika posho,” alisema.

Hivi karibuni, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akikanusha kuwepo kwa nyongeza hiyo.

Dk. Kashililah katika taarifa hiyo alikiri kuwa wabunge wanataka waongezewe posho za vikao, lakini mapendekezo hayo, hayajaanza kutekelezwa.

Alisema mapendekezo ya nyongeza hiyo yaliibuka katika mkutano wa wabunge mjini Dodoma Novemba 8 mwaka huu, lakini hadi sasa hayajaanza kutekelezwa.

“Suala la mabadiliko ya posho za vikao vya Bunge lilijitokeza katika Mkutano wa Wabunge, tarehe 8 Novemba, 2011 walipoiomba Serikali iangalie upya suala hilo kwa lengo la kuboresha,” alisema Dk. Kashililah katika taarifa hiyo.

“Hadi tunapotoa tangazo hili (Jumapili), Serikali haijatoa taarifa iwapo posho hiyo imeongezeka kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000," taarifa hiyo ilieleza.

Monday, December 5, 2011

CAG alalamikia fasheni ya ukaguzi maalumu

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ameonya kuwa endapo watendaji wanaosababisha uwepo wa ukaguzi maalumu hawatadhibitiwa mapema, ukaguzi wa hesabu hautakuwa na tija kwa taifa.

Amelalamikia kuelemewa na shughuli za ukaguzi maalumu zinazoongezeka katika ofisi yake kila kukicha.

Utouh alisema hayo juzi Dar es Salaam wakati akifunga mafunzo ya mwezi mmoja kwa wakaguzi wapya 100.

Alisema ni lazima Serikali ichukue hatua kukomesha usimamizi mbovu wa miradi ya maendeleo katika ngazi za vijiji, kata na Serikali za Mitaa kwa ujumla, vinginevyo ubadhirifu utaendelea licha ya kulundikana kwa ukaguzi maalumu.

Kwa mujibu wa Utouh, kukithiri kwa usimamizi mbovu wa miradi ya maendeleo serikalini ndio chanzo kikuu cha kuongezeka kwa ukaguzi maalumu unaoilazimisha ofisi yake kuondoka katika utaratibu wa ukaguzi wa kawaida.

Kwa sasa kwa maelezo ya Utouh, ofisi hiyo inalazimnika ‘kubeba mzigo’ wa ukaguzi maalumu usio na uwiano na nguvu kazi ndogo aliyonayo wala tija kwa Taifa.

“Imekuwa ni mtindo wa kawaida sasa hivi kwa kila ofisi kudai ukaguzi maalumu wa miradi yake ya maendeleo, huu sio utaratibu wa kawaida wa kufanya kazi kwa sababu hauna tija kwa taifa.

“Cha msingi wanaosimamia miradi katika vijiji, kata na Serikali za Mitaa wajirekebishe na kuweka mbele maslahi ya Taifa badala ya kuachia mianya ya rushwa na ubadhirifu mwingine, inayosababisha miradi kutokuwa na thamani halisi,” alisema Utouh.

Alisema hata kama ukaguzi maalumu utatekelezwa kwa wingi kiasi gani, wasimamizi wa miradi
wasipomulikwa, kukemewa na kulazimishwa wabadilike na kuweka maslahi ya umma mbele, ukaguzi huo utaendelea kuongezeka huku thamani ya miradi inayokamilika ikiendelea kufanyiwa ubadhirifu na kushuka.

“Ukaguzi maalumu sio ishara nzuri kwa wasimamizi wanaojali kazi yao na kupenda maendeleo, zinamaanisha kuna walakini na kuonesha ishara ya kutotendeka vizuri kwa jambo fulani. “Wasimamizi wa miradi katika vijiji, kata na Serikali za Mitaa wasitengeneze mazingira ya kutoaminiwa kiasi hicho kwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo,” alisema Utouh.

Alisema Serikali imejitahidi kumwongezea vijana wengi wa kazi, lakini hapati ahueni kutokana na kuongezeka kwa idadi ya ukaguzi maalumu unaoibuka kila kukicha.

“Kwa mtindo huu wa ukaguzi maalumu, hata nikipewa idadi gani ya wakaguzi, mzigo wa kazi
utakuwa ni mzito tu kwa ofisi yangu kwa sababu inakuwa kama fasheni. “Sasa kwa jinsi wafanyakazi wanavyoongezeka ndio ukaguzi maalumu unavyoongezeka, pia kutokana na wasimamizi wa miradi kuongeza kasi ya usimamizi mbovu,” alisema na kuongeza kuwa
kazi haiwezi kuwa na tija kwa staili hiyo.

Katika hatua nyingine, aliwataka wakaguzi wapya kutekeleza majukumu yao hata wakiwa nje ya makao makuu kwa kuwa maeneo hayo yanatambuliwa pia kuwa ni mahali pa kazi.

Aliwataka waondokane na dhana ya kufanya kazi katika makao makuu tu au kwenye miji mikubwa kwa sababu mchango wao unahitajika katika maeneo yote ya nchi.

Mafunzo hayo yalijumuisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama) katika ukaguzi wa hesabu pamoja na mambo mengine mbalimbali yanayohusu taaluma hiyo.