Friday, May 29, 2009

Afrika Itaweza Kuwa na Serikali Moja?

Tangu bara la Afrika lipate uhuru wake kutoka kwa wakoloni, viongozi wa afrika wamejaribu mara kadhaa kuunda serikali moja ambayo itasimamia mambo ya Afrika na kuifanya Afrika iwe na sauti katika anga za kimataifa lakini jambo hilo bado halijafanikiwa. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba kazi yao ilikuwa ni kuleta Uhuru na Umoja, na wamefanikiwa kuleta uhuru, lakini umoja bado haujafanikiwa. Kazi ya kuiunganisha Afrika moja waliachiwa viongozi na wasomi wetu wa sasa. Katika siku za karibuni, viongozi na wasomi wa Afrika wamekuwa wakikutana na kujadili juu ya kuwa ana Afrika moja, lakini baadhi ya wasomi wanasema, Afrika kuwa na serikali moja ni ndoto za alinacha. Je, ni kweli kwamba Afrika haiwezi kuwa na serikali moja? Hapa chini kuna mahojiano na Dr. Benson Bana wa Chuo kikuu cha Dar es salam juu ya Umoja wa Afrika.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Dk Bana:Afrika kuunda Serikali moja ni ndoto za Alinacha

Mhadhiri wa Chuo cha Fani na Sayansi za Jamii cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Cass) Dk Benson Bana. Maswali na majibu ya mahojiano kati ya Mwananchi na Mhadhiri wa Chuo cha Fani na Sayansi za Jamii cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Cass) Dk Benson Bana.

Unafikiria nchi za Afrika zinaweza kuunda serikali moja?

Kwa kweli ni ndoto za Ali Nacha kwa sasa kusema Bara la Afrika liwe na serikali ya pamoja. Hii ni kwa sababu tuna udhaifu wa aina nyingi ambao unatukwamisha na kutusuta katika azma ya kutaka kuungana na kuunda serikali moja.

Kwanza tujenge Asasi za Shirikisho la bara la Afrika na kuziimarisha, ikiwa ni pamoja na ushuru wa forodha, soko la pamoja kwa sababu Afrika hadi sasa bado ni 'heterogonous' kwa mfano Somalia ina matatizo yake, Misri ni Afrika lakini wanathamini zaidi Shirikisho la nchi za kiarabu, Comoro wanajifanya Wafaransa, Afrika ya Kusini wanajifanya wazungu.


Unafikiria ni kwa nini miungano mingi ya nchi za Afrika inavunjika?

Miungano hii inakufa kwa sababu waafrika wengi wanafikiria na kujali zaidi utaifa na 'vijikabila' vyao kuliko Jumuiya zao au miungano yao.

Pia ujenzi wa utaifa katika nchi nyingi za bara la Afrika bado unaendelea, ni Tanzania tu ambao tumefanikiwa lakini pia tuna muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao pia bado unatupelekesha kwa kutawaliwa na kero kuntu.

Mathalan wenzetu wakenya karibu kila kabila linataka kuwa na jeshi lake, Uganda kuna matatizo kibao ya kikabila, Burundi na Rwanda ndio usiseme kwa matatizo ya kikabila sasa utakuta yote haya yanatusuta kufanikisha azma ya kuunda serikali moja ya Shirikisho la Afrika.

Soma zaidi mahojiano haya kwa kubofya hapa.

Wabunge Wawe na Ukomo wa Kuwakilisha.

TANGU ulipoanzishwa tena mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 taratibu na sheria mbalimbali zilirekebishwa na mpya kupitishwa ili kuendana na mabadiliko hayo. Mojwapo wa sheria na mabadiliko hayo ni ile ambayo inatoa fursa kwa wabunge kuendelea kulitumikia taifa kwa vipindi zaidi ya viwili. Aidha sheria hiyo inatoa fursa kwa wabunge wetu kuwakilisha wananchbi wao kwa muda ambao hauna kikomo. Katiba ya Jumuhuri ya Muungano ya Mwaka 1977 na marekebisho yake ya 2005, sura ya tatu, sehemu ya pili, kifungu cha 71(1) kinaeleza muda wa wabunge kushika madaraka.

Kifungu hiki kinaeleza mambo takriban saba ambayo yanaweza kusababisha mbunge kupoteza sifa yake ya kuwa mwakilishi. Kati ya hayo saba hakuna ukomo unaotokana na muda wa uwakilishi, hivyo basi mbunge anaweza kuwakilisha wananchi wake mpaka utashi wake utakapoamua kuachia wengine wawakilishe.

Kupata bahati ya kulitumikia taifa lako ni kitu kizuri, na wengi tunapenda kufanya hivyo. Katika Tanzania yetu ambayo ina nafasi chache za kulitumika taifa, kila mtu angependa kulitumikia taifa hili. Wabunge wetu wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia taifa hili tangu hapo awali, na tunawapongeza sana kwa hilo. Ila sasa wakati umefika kwa wabunge wetu ambao wameshalitumikia kwa vipindi zaidi ya viwili vya miaka mitano mitano kuachia ngazi na kuwapisha wananchi wengine wenye nia na uwezo kama wao walivyofanya.

Ipo haja kwa wadau na watetezi wa demokrasia kuangalia upya sheria hii ya uwakilishi na kurekebishwa ili iweze kutoa mwanya kwa watu wengine kuwakilisha wananchi na kuleta mawazo mbadala katika uongozi wa bunge letu na serikali yetu. Makala haya ni chachu ya kuanzishwa kwa mjadala mpana juu sheria hii, wakati huu tukielekea katika mwaka uchaguzi wa 2010. Ni vyema wadau wa demokrasia kuchukua fursa hii kuangalia upya sheria hii ili ibadilishwe na kutoa nafasi kwa wawakilishi wapya ambao watakuwa na mawazo na mbinu mpya za kuleta maendeleo ya taifa hili.

Kuachia nafasi kwa wengine nao waongoze ni uzalendo pia, kwani itasaidia kutoa fursa kwa wenye mawazo mbadala kuleta maendeleo, kutoa nafasi kwa wananchi wengi zaidi kuchangia katika maendeleo ya nchi yao, kutoa fursa kwa wazelendo wengine kuchangia katika ujenzi wa taifa lao. Pamoja na faida nyingi ambazo zitapatikana endapo sheria hii itarekebishwa, pia wabunge wetu watapata bahati ya kulitumikia taifa letu kwa vipindi visivyozidi viwili vya miaka mitano kila kimoja tofauti na sasa ambapo kuna baadhi ya wabunge wameshalitumika bunge kwa zaidi ya miaka kumi na mitano.

Miaka kumi na tano kwa namna yoyote ile ni mingi sana katika suala zima la maendeleo ya nchi husika. Watu wengi wanapenda kupata fursa hii ya kulitumikia taifa lao, lakini sheria hii inawazua kushiriki katika ujenzi huo wa taifa. Mwanzoni mwa mwa mfumo wa vyama vingi, wadau wa demokrasia waliibua hoja ya kuwa na katiba mpya ambayo itakidhi matakwa ya mfumo wa demokrasi.

Madai waliyoyatoa ni pamoja na kwamaba katiba iliyopo ina viraka vingi na iliundwa kukidhi matakwa ya mfumo wa chama kimoja, hivyo walionelea heri kuitishwa mkutano wa kitaifa kujadili uandaaji wa katiba mpya itakayokidhi matakwa ya watu wote. Jambo hili halikutokea. Kuna sababu kadhaa zilitolewa na chama tawala ili kuzuia katiba yetu isibadilishwe. Huu ni wakati mwafaka wa kuibuia hoja ya kuijadili upya katiba yetu.


Wabunge wengi wanatarajiwa kukataa sheria hii kubadilishwa. Wakati tunaelekea uchaguzi mkuu wa mwakani, ni bora wanaharakati wa maendeleo kupambana na kuwezesha kuanzishwa kwa mijadala na harakati za kitaifa za kudai wabunge wawe na uongozi wenye kikomo. Kwa haraka-haraka sheria hii ikibadilishwa itaongeza sana ufanisi kwa wabunge wetu na kuleta maendeelo haraka katika nchi yetu, pamoja na faida nyingine kibao zitafuata. Kwa nini wabunge wang’ang’anie kubaki madarakani kwa muda mrefu bila kuachia madaraka kwa wengine? Tanzania haina wawakilishi wa kutosha ama? au watu wenye uwezo wa kuongoza hawatoshi?

Mjadala huu bado upo wazi na tunatoa nafasi kwa wanaharakati na wapenda maendeleo ya nchi hii kuchangia na kuja na mawazo mbadala juu ya sheria inayonyima ukuaji wa demokrasia ya kweli ya uwakilishi.

Na aidan Mmari.


Makala haya yalichapwa katika gazeti la mwananchi la tarehe 26/05/09.

Gender and Development Seminar Series

Gender and Development Seminar Series

You are invited to the weekly Gender and Development Seminar Series in which this week, Moses Kulaba and Albanie Marcossy (Policy Forum) and, Marjorie Mbilinyi (TGNP) will facilitate GDSS Pre- Budget discussion on

People's Expectations and Demands using Budget Guidelines Digest as a Tool for Advocacy!

Date: 3rd June, 2009

Time: 3:00 pm - 5:00 pm

Venue: TGNP Grounds / Adj.NIT

Please confirm your participation through

info@tgnp.org

Come One Come All !!!!!!

Tuesday, May 26, 2009

Makala: Upelelezi wa Milele Kesi za Mimba Kisarawe.

Pale wilayani kuna ujanjaujanja unatumika kwa sababu mimi nina binti ambaye alikuwa anasoma shule ya sekondari Mwaneromango, nilimkamata mtuhumiwa kwa mkono wangu, nikampeleka Kisarawe, lakini mpaka leo tangu mwaka 2002 naambiwa upelelezi unaendelea, mtuhumiwa yuko uraiani na binti yangu alishajifungu

Taratibu zote muhimu alizotakiwa kufuata kufungua kesi alitimiza na sheria iko upande wake, lakini hadi leo hajapata haki. Juma Mwagala hasononeshwi na kitu kingine chochote zaidi isipokuwa umaskini wake anaona ndio chanzo cha kushindwa kwake kupata haki kortini dhidi ya kijana aliyempa mimba binti yake.

"Umaskini huu!" anapiga makofi na kunyanyua juu mikono yake kwa ishara ya kumuomba Mungu. Na pale anapogeuka nyuma na kumwona mtu akisogelea alipoketi, anajikusanya na kumkaribisha.

Kusoma makala nzima bofya hapa.

"Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni Changa la Macho"

Sheria ya maadili ya umma ilitungwa mwaka 1995 na bunge la Jamuhuri ya Tanzania kwa lengo la kuondoa migongano ya maslahi kwa watumishi wa umma wakati wanafanya maamuzi yao. Sheria hii ilitungwa kutokana na mambo matatu muhimu. Kwanza ilitokana na kuanguka kwa Azimio la Arusha lililokuwa likitekeleza sera za Ujamaa na kujitegemea. Azimio la Arusha lilikuwa na misingi ya maadili ya viongozi, kwahiyo baada ya kuanguka kwa Azimio hilo, ikabidi itafutwe njia mbadala. Pili, ni kutokana na mabadiliko kutoka mfumo wa chama kimoja kwenda kwenye mfumo wa vyama vingi. Na tatu ni kuwepo kwa matukio mbali mbali katika kipindi hicho ya matumizi mabaya ya madaraka. Ndiyo maana hata Mwalimu Nyerere katika kitabu chake cha ‘Uongozi na hatima ya Tanzania’ alisema, “Ikulu imekuwa pango la walanguzi” akiwaonya viongozi wa umma kutotumia ofisi za umma kwa maslahi yao binafsi.

Soma zaidi mahojiano na Mwanasheria mwandamizi wa chama cha Wanasheria watetezi wa Mazingira (LEAT) Tundu Lissu kuhusu mapungufu ya sheria hii kwa kubofya hapa.

Monday, May 25, 2009

Kwa nini Si Vyema kwa Wabunge Wetu Kuongezewa Mishahara?

Wanafunzi wa darasa la saba wa Shule ya Msingi Mbagala Kuu, Dar es salaam, wakiwa darasani wakifanya mitihani yao ya kila mwisho wa mwezi.

Katika hali kama hii ni aibu kwa wabunge wetu kudai nyongeza ya mishahara na marurupu. Huduma za jamii kama Elimu, afya, na miundombinu ikiendelea kudorora kila siku, huku gharama za maisha zikipanda kwa wananchi wa kawaida. Picha hii inawakilisha maelfu ya wanafunzi ambao wanakaa chini na wanakabiliwa na upungufu mkubwa wa madawati, walimu, vitabu, vyumba vya madarasa, chakula, madawa na nk. Je, upo umuhimu wowote kwa waheshimiwa wabunge kudai nyongeza ya mishahara katika kipindi hiki?

Friday, May 22, 2009

FemAct Press Release on UFISADI.

‘WAR AGAINST CORRUPTION: THE GOVERNMENT SHOULD RESPOND TO THE VIEWS OF THE PEOPLE’

We members of the Feminist Activist Coalition (FemAct), over fifty civil society organisations (50), who work together to advocate for women’s and human rights, social transformation and the empowerment of all women and marginalised groups, met on 20th May 2009 to reflect on the on-going debate about grand corruption in Tanzania and the future of the country. We are deeply concerned with the current situation and especially the inadequate way with which the Government is handling the ever-increasing syndicated grand corruption and organised crime cases and scandals in the country. Stories of syndicated grand corruption in the country are horrifying, and force us to draw one solid conclusion, that the Tanzania state has been hijacked!

FemAct recognises syndicated grand corruption as all private gain-motivated abuse of public office, plunder of public property, corruption in the electoral process, lack of transparency in public contraction processes, (i.e. public procurement, public investment, privatisation), budget execution without consideration of national priorities, discriminatory enforcement of laws and regulations, and disobedience of public leadership ethics.

FemAct has noted numerous scandalous events which document the mushrooming of grand corruption and state hijacking operations in Tanzania. Just to mention a few, we note acts of grand corruption in Mining Development Agreements (MDAs) with specific reference to the Buzwagi project scandal; energy contracts with specific reference to the sagas of Richmond LLC/Dowans and Independent Power Project –Tanzania Limited (IPTL); wanton privatisation contracts with specific reference to the National Bank of Commerce (NBC), Kiwira Coal Mine, Tanzania Telecommunications Company Limited (TTCL), Kilimanjaro International Airport (KIA), Tanzania International Container Terminal Services (TICTS) and Tanzania Railways Corporation (TRC); plunder/embezzlement of public financial resources with specific reference to inflated construction cost of Bank of Tanzania Twin Towers, fraudulent appropriation of public finances (with impunity) in the External Payment Arrears (EPA) account [Kagoda Agricultural Limited and others], defaulted Commodity Import Support (CIS) fund and Debt Conversion Programme (DCP) fund; syndicated grand corruption in the public procurements with specific reference to acquisition of military equipment, aviation radar, and presidential jet; plunder of public funds by falsification with specific reference to Tangold, Meremeta, and Deep Green conspiracies; plunder of natural resources with specific reference to fisheries, forestry and wildlife; land alienation shielded by claims of Foreign Direct Investments (FDIs) policy with specific reference to bio-fuel farming (Rufiji saga); and grand corruption involving obsolete/expired medical supplies risking Tanzanians life.

It is FemAct’s conclusion that this increasing trend of syndicated grand corruption is due to the capture of the state by powerful moguls working as one in a powerful corruption network/syndicate. The network is reinforced by such strategies as money laundry and corruption in the electoral process; “free-market” neo-liberal macro economic policy, including liberalisation and privatisation, which benefit big capitalists and imperialists rather than sustainable development for all women, men, and children; lack of strong good governance institutions, structures and systems (weak state); greed and selfishness of political and public leadership; weak civic engagement by the people themselves; continued application of many colonial era legislations [in effect regulations and procedures] and antiquated constitution; weak political party systems giving opportunity to corrupt entrepreneurs to take leadership positions; and government support for a small group of leaders who act against the people’s interests with impunity.

FemAct believes the syndicated grand corruption and the free-market economy policy are to blame for adversities Tanzanians have been forced into, including the current weak state; economic crisis; political leadership entrepreneurship; the increasing gap between the rich and the poor; increasing poverty amongst the majority of Tanzanians; increasingly low quality and quantity of social service delivery – education, health, physical infrastructure, power utility and administration of justice; declining social and economic wellbeing across majority sections of society [in effect increasing cost of living, which majority cannot afford]; increasing unemployment; increasing insecurity [in effect increasing gender-based violence, criminal and banditry acts]; emboldening of corruption syndicates and actors; increasing of otherwise avoidable deaths such as those involving road accidents, maternal deaths, HIV&AIDS infection arising from sexual abuse, and child mortality; examinations leakage and cheating [in effect declining standard of education]; and fall of cooperatives and declining agriculture and rural economy in effect threatening food security.

Consistent with the above observations, FemAct is hereby declaring its position and demands the following:-

1. The Government acts indiscriminately, immediately and without excuse to prosecute all persons suspected of grand corruption cases and dismantle their corruption networks.

2. The Government is held responsible to immediately: implement wholly the Parliamentary resolution on Richmond; provide credible a public statement on all grand corruption scandals currently in public debate; disclose all existing investment contracts for public access and scrutiny; and ensure state function enforcement organs specifically the Police Force, the Office of Director of Public Prosecution, the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) and the National Security (intelligence services) conduct their respective business in an accountable manner under strict adherence to professional ethics and expected competences.

3. Citizens are held responsible to: identify and reject all corrupt elements to occupy elective political offices through ballot; refuse to implement policy decisions reached without public participation/scrutiny and reached outside the law; be vigilant against acts of land alienation by corrupt elements; fearlessly continue interrogating and exposing grand corruption and persons behind the schemes; and continue supporting like-minded elements exposing acts and actors of grand corruption.

4. The corporate entities are held responsible to: follow legal procedures and business ethics in all their dealings, prioritising humanity and public interest; and expose corporate sector actors involved in grand corruption.

5. Civil society entities are held responsible to: rescind from taking part in any act related to grand corruption; and continue mobilising and enlightening the public on war against corruption and culprits.

6. The public and mass media are held responsible to: maintain their exemplary public advocacy to expose grand and petty corruption; rescind from being ‘used’ by and in favour of corrupt syndicates/actors to misinform the public about the genuine common cause of fighting corruption; and continue disseminating civic education that will ultimately contribute to increased civic competence to hold the Government to account.

7. Religious leaders are held responsible to: declare their respective positions in the war against grand corruption and thereby mobilise the pubic at large to fight corruption; and continue preaching against corruption and corruption in the electoral process.

8. Political parties are held responsible to: critically assess inter-party electoral systems with a goal of ensuring political parties are no longer prone to influences of corrupt elements assuming public offices/leadership through political parties.

9. The multilateral organisations and other development partners are held responsible to stop imposing their agenda and conditionalities on the government and other recipient partners, especially the free market neo-liberal macro economic framework which has proven to be bankrupt by the global crisis.

10. Citizens, civil society organisations and the Government are together duty bound to engage in a national debate for a new Tanzania in which there is an alternative macro economic framework for sustainable development that will ensure equal social and economic benefits for all Tanzanians without any type of discrimination – by race, sex, ethnicity, class, age, nationality, religion, disability or HIV and AIDS status.


Issued by FemAct members and signed by
1. Tanzania Gender Networking Programme (TGNP)
2. Legal and Human Rights Centre (LHRC)
3. Concern for Development Initiatives in Africa (ForDIA)
4. Youth Action Volunteers (YAV)
5. The Leadership Forum (TLF)
6. Coast Youth Vision Association (CYVA)
7. Walio Katika Mapambano na AIDS Tanzania (WAMATA)
8. Tanzania Media Women’s Association (TAMWA)
9. Youth Partnership Countrywide (YPC)
10. Tanzania Human Rights Fountain (TAHURIFO).
11. HakiArdhi
12. Women Legal Aid Centre (WLAC)
13. Tanzania Coalition on Debt and Development (TCDD)
14. Lawyers Environmental Action Team (LEAT)

22 Mei 2009

Wednesday, May 20, 2009

Salama: Jasiri Aliyetangaza Kuishi na Virusi vya UKIMWI

Maisha tunayoishi hapa duniani, yanahitaji uvumilivu, ujasiri pamoja na busara miongoni mwa jamii inayotuzunguka. Nashawishika kusema hayo baada ya kukutana na Salama Jumanne(Pichani), ambaye ana ujasiri wa kueleza kitu kinachomsibu pamoja na kupambana na misukosuko kwa jamii ambayo ilimcheka baada ya kuamua kujitangaza kuishi na Virusi vya Ukimwi (VVU). Nilipomwona mara ya kwanza, sikuamini kile alichokieleza kuwa anaishi na VVU, hali iliyonilazimu katika nafasi yangu ya uandishi wa habari, kuandika habari zake na kufuatilia kila tukio analokumbana nalo nami kuliandika ili watu mbalimbali waweze kumsaidia kutokana na matatizo anayokumbana nayo.

Nilihuzunika baada kunieleza historia ya maisha yake, pia nilijiuliza maswali mengi, je, ingekuwa mimi nakumbana na tatizo hili ningekaa kimya au ningewaeleza wenzangu? Je, marafiki, wazazi na jamii kwa ujumla wangelipokeaje tatizo langu ingawa mimi mwenyewe nimeshaamua kulitangaza ili nipate msaada? Binafsi sina uwezo mkubwa wa kumsaidia Salama lakini naamini watu mbalimbali pamoja na wahisani, wataguswa na habari hii na kumsaidia kwa kuwa licha ya kuwa anaishi na VVU, pia ana watoto watatu na mjukuu mmoja.

Salama ni mtu mwenye haiba, huwezi kuamini kuwa anaishi na VVU mpaka alipojitangaza kuwa na hali hiyo, umati uliokusanyika pale Mabibo katika Viwanja vya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Siku ya Maadhimisho ya Mwanamke Duniani, inayofanyika Machi 8 kila mwaka. Isome zaidi habari hii kwa kubofya hapa.

Friday, May 15, 2009

Wabunge Kuongezewa Mishahara; Hii Imekaaje Wadau?

Katika miezi ya hivi karibuni Wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wamekuwa katika malumbano makali baina yao, baadhi wakipinga hoja ya kutaka kuongezewa mishahara, marupurupu na posho, na wengine wakidai nyongeza hiyo. Kwa wananchi walio wengi katu hawawezi kukubaliana na hoja hii ya kuongezwa mishahara ya wabunge, ambayo kama mapendekezo hayo yakiridhiwa, wabunge wetu watalipwa jumla ya shilingi za kitanzania Milioni Kumi na mbili kwa mwezi. Hiki ni kiasi kikubwa cha pesa kwa hali yoyote ile. Katika Tanzania kama hii ya sasa ambayo Huduma za Afya zimedirora sana, Miundombinu ya barabara, maji, umeme, ni hafifu, Elimu inayodidimia kila ukicha, Ukosefu wa Ajira kwa vijana, Ukosefu wa Masoko kwa bidhaa za Wakulima, na changamoto nyingine kibao ambazo nchi yetu inazikabili sidhani kama wabunge wetu kuongezewa mishahara katika kipindi hiki ni busara na haki. Wanaharakati na waandishi wengi wamejaribu kutoa mawazo yao juu swala hili na kuonyesha wazi nia ya kupinga muswada huu kupitishwa,lakini wabunge wanaong'ang'ania muswada huu ni wengi na wamekuwa wakiongezewa nguvu na spika wa bunge, waziri mkuu na wabunge kadhaa wa chama Tawala.

Je, Wadau mna maoni gani juu ya mswada huu?

Kwa kusoma zaidi juu ya mjadala huu bofya katika linki hapa chini.

Sipendi tena sitaki wabunge wajiongezee mishahara

Pinda atetea wabunge

Dk. Slaa apita kipindi kigumu bungeni

Thursday, May 14, 2009

Wateja akaunti ya wanawake kupata punguzo

Wateja wa Benki ya Standard Chartered wenye akaunti ya Diva Club ambayo ni kwa ajili ya wanawake, sasa watapata punguzo la bei za bidhaa au huduma katika maduka maalumu.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Jeremy Awori alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa sherehe ya Siku ya Mama ambayo benki hiyo iliandaa kwa ajili ya wateja wake wa akaunti ya Diva.

Awori alitaja baadhi ya maduka ambayo wateja wanaweza kupata punguzo kuwa ni pamoja na Living Room, Game, Night Support na DT Dobie. Katika sherehe hizo zilizofanyika Hoteli ya Kempinski, Benki hiyo ilitoa zawadi kwa wanawake waliohudhuria katika sherehe hiyo kwa kutambua mchango wao katika kutunza fedha katika benki hiyo kupitia akaunti hiyo.

Wednesday, May 13, 2009

Mengi, Rostam wamweka Kikwete njia panda

-Iddi Simba ampinga Rostam kuhusu NICO
KUNA maoni kuwa ombwe la uongozi ndilo ambalo linachangia katika malumbano, ambayo yameigawa nchi, kati ya wafanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ambao kila mmoja anamtuhumu mwenzake kwa kuhujumu Taifa.

Baadhi ya wanazuoni, wanasiasa wastaafu na raia wa kawaida, wameiambia Raia Mwema wiki hii kwamba malumbano hayo hayawezi kuachwa yaendelee, na kwamba sasa lazima Serikali ionyeshe njia katika kuyamaliza kwa kuwatosa, japo wote wawili wanaelezwa kuwa watu wa karibu na Rais Jakaya Kikwete.

Mmoja wa wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), amesema kinachojulikana kwa Watanzania wote ni kwamba hakuna Serikali ya Rostam Aziz au Reginald Mengi, na kwamba ukimya wa Serikali unaweza kuchochea wananchi kujichukulia sheria mikononi.

Mhadhiri Mwandamizi wa UDSM, Profesa Mwesiga Baregu, ameiambia Raia Mwema kwamba Serikali ina wajibu wa kuchunguza tuhuma zinazorushwa kutoka kila upande na kwamba kilichofanywa na kila mmoja kati ya Mengi na Rostam ni kila mtu kutoa vidokezo tu na sasa Serikali ichukue hatua.

“Kama Serikali ikiendelea kukaa kimya italeta mguno miongoni mwa wananchi na hiyo ni hatari, wanaweza (wananchi) kuamua kuanza kujichukulia sheria mkononi,” alisema Profesa Baregu na kuongeza:

“Katika maelekezo yake au hatua itakazochukua, Serikali inapaswa kulinda haki za raia kwa mujibu wa sheria zilizopo lakini kwa maslahi ya Taifa.”

Soma zaidi

Mengi, Rostam wamweka Kikwete njia panda

-Iddi imba ampinga Rostam kuhusu NICO
KUNA maoni kuwa ombwe la uongozi ndilo ambalo linachangia katika malumbano, ambayo yameigawa nchi, kati ya wafanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ambao kila mmoja anamtuhumu mwenzake kwa kuhujumu Taifa.

Baadhi ya wanazuoni, wanasiasa wastaafu na raia wa kawaida, wameiambia Raia Mwema wiki hii kwamba malumbano hayo hayawezi kuachwa yaendelee, na kwamba sasa lazima Serikali ionyeshe njia katika kuyamaliza kwa kuwatosa, japo wote wawili wanaelezwa kuwa watu wa karibu na Rais Jakaya Kikwete.

Mmoja wa wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), amesema kinachojulikana kwa Watanzania wote ni kwamba hakuna Serikali ya Rostam Aziz au Reginald Mengi, na kwamba ukimya wa Serikali unaweza kuchochea wananchi kujichukulia sheria mikononi.

Mhadhahiri Mwandamizi wa UDSM, Profesa Mwesiga Baregu, ameiambia Raia Mwema kwamba Serikali ina wajibu wa kuchunguza tuhuma zinazorushwa kutoka kila upande na kwamba kilichofanywa na kila mmoja kati ya Mengi na Rostam ni kila mtu kutoa vidokezo tu na sasa Serikali ichukue hatua.

“Kama Serikali ikiendelea kukaa kimya italeta mguno miongoni mwa wananchi na hiyo ni hatari, wanaweza (wananchi) kuamua kuanza kujichukulia sheria mkononi,” alisema Profesa Baregu na kuongeza:

“Katika maelekezo yake au hatua itakazochukua, Serikali inapaswa kulinda haki za raia kwa mujibu wa sheria zilizopo lakini kwa maslahi ya Taifa.”

Soma zaidi

Tuesday, May 12, 2009

Sakata la Mengi na Rostam: Serikali Yatoa Tamko


SERIKALI imewataka Wafanyabiashara Rostam Aziz na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuacha mara moja malumbano kati yao na kutotumia vyombo vyao vya habari kwa maslahi yao binafsi.

Sambamba na hilo imewataka kuwasilisha vielelezo na madai yao kwa mamlaka husika ili hatua zinazofaa zichukuliwe na wananchi wapewe taarifa na vyombo hivyo.

Akitoa tamko la serikali leo mbele ya waandishi wa habari, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera kwa niaba ya Waziri wake, George Mkuchika alisema serikali haitakubali kusikia malumbano hayo ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa amani nchini yakiendelea.

“Serikali imeyatafakari malumbano ya wafanyabiashara hawa na kubaini yanalipeleka taifa letu mahali pabaya kwani yana mwelekeo wa uvunjaji wa amani kama yataachwa kuendelea.

"…pia haitavumilia kuona vyombo vya habari nchini vikichangia kuligawa taifa katika makundi na kudumaza maendeleo”,alisema.

Badala yake amevitaka vyombo hivyo vya habari kutotomiwa kwa manufaa binafsi ya mmiliki au mtendaji; viongozwe na maadili ya taaluma na jamii husika na kisitangaze habari kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, kabila, dini, jinsia au ulemavu na kuchochea uhasama

Monday, May 11, 2009

Uhuru wa vyombo vya habari unufaishe jamii pana zaidi

MWISHONI mwa wiki hii Tanzania ilijiunga na wadau wa habari duniani kuadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani. Mwaka jana juma kama la leo niliandika makala kuhusu maana ya dhana ya uhuru wa vyombo vya habari kwa ujumla na pia nikatathmini mwenendo wa vyombo vya habari nchini.

Tunapoelekea katika uchaguzi, kama nilivyoeleza katika makala zangu za hivi karibuni, vyombo vya habari vinaweza kujikuta vikichezewa na wenye maslahi ya kisiasa na kupoteza mwelekeo. Lakini daima, faida zinazotokana na uwepo wa uhuru wa vyombo vya habari ni kubwa kuliko kinyume chake. Labda nirejee tena makala yangu ya mwaka jana niliyoitoa baada ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, Mei 3.

Siku hii hutumika na wanahabari duniani kote kutathmini ni kwa kiasi gani nchi husika imejitahidi kuhakikisha inalinda, au kuingilia, uhuru wa vyombo vya habari. Kwa kawaida, kama nilivyokwishasema huko nyuma, wapo watu ambao huchanganya dhana hizi mbili: Uhuru wa Habari na Uhuru wa Vyombo vya Habari.

Uhuru wa habari ni haki ya kila mtu kuwa na uhuru wa kupata taarifa, kuwa na maoni na kusambaza taarifa kupitia njia za kuhabarishana. Haki hii ni ya kila mtu, bila kujali fani yake wala hadhi yake katika jamii. Ni haki anayozaliwa nayo kila mtu.

Uhuru wa vyombo vya habari, kwa upande mwingine, unagusa moja kwa moja vyombo vya habari. Uhuru huu unahusu haki ya vyombo vya habari kufanya kazi zake kitaaluma bila kuingiliwa wala kusukumwa na mtu au taasisi yeyote.

Kwa hiyo kuwepo uhuru wa vyombo vya habari kunaweza kusaidia kushamirisha haki ya kila mtu ya kupata na kusambaza habari au maoni. Hapo ndipo dhana hizi mbili zinapokutana.

Msingi wa haki ya uhuru wa habari uko katika Ibara ya 19 ya Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu la 1948 (Universal Declaration of Human Rights) na ni sehemu ya haki zingine kadhaa za binadamu ambazo sehemu kubwa zimeainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika kuangalia Uhuru wa vyombo vya habari vipo vigezo kadhaa ambavyo ni muhimu kuvitathmini. Kwanza ni lazima sera na sheria za nchi ziendane na dhana nzima ya uhuru na haki za binadamu kama zilivyoainishwa katika matamko kadhaa ya kimataifa. Leo hii hapa Tanzania haki ya uhuru wa habari inalindwa na Katiba katika ibara ya 18 Kipengele cha (1) na (2).

Lakini bado nchi yetu iko katika mchakato wa kutunga sheria ya Uhuru wa Habari na nyingine ya mwongozo kwa vyombo vya habari ambazo zitasaidia kushamirisha uhuru wa habari kwa upande mmoja na uhuru wa vyombo vya habari kwa upande mwingine.

Soma zaidi

Ma-DC wapya Wanawake


Wakuu wa Wilaya wapya, sita wanawake kati ya 15 walioteuliwa na Rais hivi karibuni wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumaliza semina elekezi mjini Morogoro, majina na Wilaya zao kwenye mabano , kutoka kulia ni Fatma Mwassa ( Mvomero), Queen Mlozi ( Ukerewe), Fatma Ally ( Nanyumbu), Mery Silla (Arumeru), Dk Rehema Nchimbi ( Newala) na Angelina Mabula ( Mulemba)., mafunzo hayo ya awali yalifanyika kuanzia Mei 5,hadi 8, mwaka huu.
Picha na mdau wa Morogoro John Nditi.

Idadi hii ya uwakilishi wa akina mama inatosha jamani?

Friday, May 8, 2009

Minjingu haikubaliki au tunakimbia majukumu?


Wiki mbili zilizopita, kuliibuka mjadala bungeni kuhusu ubora wa mbolea ya Minjingu inayozalishwa na Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu kilichoko Babati mkoani Manyara, Kaskazini mwa Tanzania. Baadhi ya watunga sheria nchini, wakiwa katika mjadala wa Muswada wa Mbolea wa mwaka 2008, walidai mbolea hiyo haifai na wakaenda mbali zaidi kuitaka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, isiwapelekee pembejeo hiyo katika maeneo yao.

Miongoni mwao walikuwa ni Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi wa chama tawala, CCM na Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo wa United Democratic Party (UDP).
Pamoja na mambo mengi katika mchango wake, Zambi alisema yafuatayo wakati akijadili muswada huo, “…mwaka huu kule Mbozi na mahali pengi, tumepelekewa mbolea ya Minjingu ambayo imewaharibia uzalishaji sana wananchi wa Wilaya ya Mbozi na inawezekana na mahali pengine.

“Wananchi wale wanasema mbolea hii kama haitarekebishwa, naomba niseme kwa niaba yao, nina hakika kwa sababu ni wengi wananiona na wananisikiliza, wamesema serikali isituletee mbolea hiyo.”

Mbunge huyo wa Mbozi Mashariki aliendelea na mchango wake bungeni Aprili 22, mwaka huu na kueleza, “Nalisema hili kwa sababu ndio ujumbe wao, naweza nikawa nawakwaza wengine, lakini naungana na wananchi wa Wilaya ya Mbozi na mimi nimeona mashamba ya wananchi yameharibika sana kwa wale wote waliotumia mbolea ya Minjingu.”

Kwa upande wake, Cheyo naye alikataa mbolea hiyo ya Minjingu na kueleza kwamba ni bora wananchi wa kwao (Usukumani) waachwe waendelee kutumia mbolea za samadi na mboji, akidai mbolea ya Minjingu inaharibu ardhi na mazao hayapatikani.

Soma zaidi

Thursday, May 7, 2009

Mgodi wa Buzwagi waanza kutoa dhahabu




Barrick Gold Tanzania announced today the first gold pour at its new Buzwagi mine in Kahama District, Shinyanga Region. In production, the mine will be one of the country's largest mining operations. Buzwagi is the sixth Barrick project brought into production on time in the last six years.

"For any mining company, a new mine entering production is always an exciting time - particularly for the development team," said President and CEO Aaron Regent. "The team constructed Buzwagi on time and in line with its budget of about $400 million. They also successfully managed to do this with an outstanding safety record."

In 2009, Buzwagi is expected to produce approximately 200,000 ounces of gold at total cash costs of $320-$335 per ounce.

The Buzwagi project is a catalyst for economic growth with an initial investment of 450 billion shillings during its construction phase and over 1.3 trillion shillings when it becomes operational. During construction, Buzwagi provided more than 900 jobs and will cater for 700 jobs directly during operation.

Wednesday, May 6, 2009

Walemavu wa ngozi (Albino) kutungiwa sheria ya kuwalinda

Serikali inatarajia kuandaa muswada wa sheria kwa lengo la kuwahakikishia hifadhi na usalama zaidi watu wenye ulemavu nchini wakiwamo maalbino.

Kwa sasa iko katika mchakato huo ambao baada ya kukamilika, muswaada huo utawasilishwa bungeni na kutungiwa sheria.

Mpango huo wa serikali ulitangazwa jana na Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein wakati akihutubia Maadhimisho ya Nne ya Siku ya Maalbino nchini yaliyofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Dk. Shein alisema hatua hiyo ni miongoni mwa jitihada za serikali za kutekeleza kwa vitendo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara 14.

Alifafanua kuwa mchakato huo unafuatia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Hifadhi ya Watu Wenye Ulemavu ambao utekelezaji wake unasadifu matakwa ya Ibara ya 14 ya Katiba inayotamka kuwa kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka katika jamii, hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria.

``Serikali inaamini katika suala la utawala bora na mfumo wa sheria hivyo haitavumilia kuona kuwa haki za raia wake zinavunjwa au zinapuuzwa,`` alisema.

Alisema vitendo wanavyofanyiwa albino nchini sio tu visivyovumilika bali pia ni vya uvunjaji wa Katiba na sheria ya nchi na kwamba serikali itaendelea na vita dhidi ya watu wanaofanya vitendo hivyo.

Makamu wa Rais alisisitiza kuwa serikali itaendeleza mapambano makali dhidi ya vitendo hivyo kwa uwezo wake wote katika jitihada za dhati za kutokomeza udhalimu dhidi ya utu wa albino.

Hata hivyo, alisema ili kufanikisha azama hiyo, hapana budi kuwepo Katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza, Makamu wa Rais alitoa tena wito wa serikali kwa Watanzania wa kuacha kuendeleza imani potofu za kishirikina ambazo zinasababisha janga kwa albino.

Awali, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa,alitaja hatua zaidi zinazochukuliwa na serikali katika kuhakikisha walemavu na albino wanapata fursa na huduma zaidi na bora kuzingatia mahitaji yao.

Profesa Mwakyusa alizitaja miongoni mwa hatua hizo ni kupitisha baadhi ya miongozo ikiwamo ya elimu shirikishi na mwangozo wa kuwatambua mapema watoto wenye ulemavu.

Kuhusu ombi la kutaka matibabu ya albino yasilipiwe, alisema suala hilo limezingatiwa katika sheria mpya lakini aliongeza kuwa tayari huduma hizo hutolewa bure katika kituo cha Mkindo kilichopo mkoani Mwanza ambako kuna albino 92.

WAKULIMA WADAI MBOLEA YA MINJIGU KWA WAZIRI MKUU


WAKULIMA wa kijiji cha Mtama wilayani Mbinga, Ruvuma, wamemwomba Waziri Mkuu Mizengo Pinda ahakikishe kuwa wataendelea kupatiwa mbolea ya Minjingu kwa sababu imewasaidia kuongeza mavuno ya mahindi kwa karibu mara tatu.

Ombi hilo lilitolewa kwa Waziri Mkuu jana (Jumatatu, Mei 4, 2009) mara baada ya kukagua shamba la mahindi la majaribio ya matumizi ya mbolea mbalimbali katika kurutubisha ardhi kwenye kijiji hicho ambako alishuhudia mahindi yaliyopandwa kwa kutumia mbolea tofauti.

Akitoa taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Mwenyekiti wa kikundi cha majaribio ya mbolea Mtama (KIMTA), Bw. Gizla Mbugu alisema wanahitaji zaidi mbolea ya Minjingu kwa sababu wamebaini wakiichanganya na mbolea ya kukuzia aina ya urea wanapata mavuno mengi zaidi.

“Ukipanda kwa mbolea ya Minjingu na kutumia mbolea ya urea kukuzia una uwezo wa kuvuna si chini ya magunia 16 kwa ekari moja wakati ukipanda bila mbolea na usipotumia mbolea ya kukuzia unapata magunia matatu hadi matano kwa ekari moja, ukitumia DAP peke yake unavuna magunia 17 kwa ekari moja lakini tatizo ni bei kubwa ya mbolea hiyo,’’ alisema.

Alimweleza Waziri Mkuu kwamba katika majaribio yao wamebaini kwamba wasipotumia mbolea wakati wa kupanda mahindi lakini wakatumia mbolea ya kukuzia aina ya urea wanaweza kuvuna magunia matano hadi nane kwa ekari moja.

Lakini alimtahadharisha Waziri Mkuu kwamba walijaribu pia kutumia mbolea ya urea kupandia na kukuzia kwa sababu kuna wakulima ambao walikuwa wakifanya hivyo na mwaka jana waliweza kuvuna magunia nane kwa kila ekari lakini mwaka huu mahindi yameota bila kuzaa chochote kwa hiyo hawatavuna kitu.

Naye mkulima wa kijiji cha mtama, Bw. Allen Nombo alisema wanaomba uamuzi wa kuleta mbolea ya Minjingu usiwe ni wa majaribio bali uwe endelevu kwa sababu wameweza kumudu bei ya mbolea hiyo. Hivi sasa bei ya mfuko wa kilo 50 ni sh. 25,000/- hadi 30,000/- bila ruzuku wakati mbolea ya ruzuku inauzwa kati ya sh. 15,000/- hadi 18,000/- kwa mfuko huo huo wa kilo 50.

Taarifa kutoka ofisi ya kilimo zinasema wakulima wengi wanashindwa kumudu mbolea ya DAP kwa sababu mfuko mmoja wa kilo 50 unauzwa kati ya sh. 90,000/- hadi 120,000/- bila ruzuku wakati mfuko wa urea kilo 50 unauzwa kati ya sh. 40,000 na sh. 50,000/- kwa hiyo wakulima wanaona ni nafuu kuchanganya mbolea zaminjingu na urea.

Waziri Mkuu pia amekagua shamba la mahindi la majaribio ya matumizi ya mbolea mbalimbali katika kurutubisha ardhi katika kijiji cha Mtama; kukagua mtambo wa kukoboa kahawa katika kijiji cha Utiri na kutembelea kituo cha utafiti wa Kahawa cha TACRI katika kijiji cha Myangayanga.

Leo (Jumanne, Mei 5, 2009) Waziri Mkuu atakwenda Kigoma kwa ziara ya siku mbili ambako atazuru wilaya za Kigoma na Kasulu kwa kutembelea miradi ya kilimo na umwagilaijai ikiwa ni pamoja na kukabidhi power tillers.

Ziara ya Waziri Mkuu katika mikoa ya Ruvuma, Kigoma na Rukwa ni mfululizo wa ziara zake za kufuatilia maagizo ya kilimo yaliyofikiwa katika mkutano aliouitisha Oktoba mwaka jana kuweka malengo ya kuinua kilimo katika mikoa sita ya Morogoro, Iringa, Mbeya, Ruvuma, Kigoma na Rukwa.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

JUMANNE, MEI 5, 2009.

Tuesday, May 5, 2009

MENGI NAYE AMJIBU ROSTAM



Picha ya chini:Mojawapo ya nyaraka ambazo mawakili wa mengi na IPPedia wamezisoma leo.

Picha ya juu:Wakili Michael Ngalo wa Ngalo & Company Advocates akisoma baadhi ya vielelezo vya mteja wake, Mwenyekiti wa IPP Reginald Mengi, kudai kwamba tuhuma zote alizomwagiwa na Mbunge wa Igunga Mh. Rostam Aziz (kama inavyoonesha kwenye posti ya hapo chini) si kweli katika mkutano wa waandishi wa habari uliomalizika sasa hivi hoteli ya movenpik, Dar. Shoto ni mwanasheria wa makampuni ya IPP, Mh Agapirus Nguma ambaye pamoja na Mh. Ngalo walimwakilisha Mengi kwenye mkutano huo.

Monday, May 4, 2009

Rostam amvurumishia makombora Mengi


Mfanyabiashara bunge wa Igunga, Rostam Aziz, amemuelezea Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi kuwa ni nyangumi wa ufisadi na akatangaza kupeleka faili lenye ushahidi wa matendo yake maovu kwa vyombo husika ili vimchunguze.

Katika kujibu madai ya Mengi kuwa mbunge huyo ni miongoni mwa mafisadi papa watano nchini, Rostam alidai Mengi ni nyangumi wa ufisadi anayewahujumu masikini huku akijidai kwamba anawaonea huruma na wakati huo huo kuomba huruma ya wananchi.

Sanjali na hilo, Rostam anakusudia kumshitaki Mwenyekiti Mtendaji huyo wa IPP baada ya kushindwa kukanusha na kumwomba radhi katika muda wa saa 48 alizompa wiki iliyopita kutoka na madai hayo aliyoyatoa katika mkutano wake na waandishi wa habari Aprili 23, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Rostam ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alitoa nyaraka mbalimbali za kuunga mkono madai yake ya Mengi kufilisi mali za Watanzania ukiwamo ubadhirifu katika iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC).

“Mengi ni nyangumi wa ufisadi nchini, alianza kushiriki kuifilisi nchi kwa kushiriki katika vitendo vya ufisadi vilivyochangia kuifilisi iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), ambayo ni mali ya Watanzania na hatimaye kupelekea kubinafsishwa kwake kwa bei poa,” alisema Rostam katika mkutano huo.

Huku akitaja akaunti namba za kampuni zinazodaiwa kuwa za Mengi ikiwamo Anche Mwedu Limited (AML), Rostam alidai Mengi alichukua mkopo mwanzoni mwa miaka ya 1980 wa mabilioni ya shilingi na amegoma kuyalipa hadi leo na kulazimisha suala hilo kufikishwa mahakamani.

“Jumla ya fedha zote za NBC ambazo akidaiwa Mengi kupitia kampuni yake ya Anche Mwedu Limited (AML) hadi kufikia Januari 1996 zilikuwa ni Sh 5,863,002,196.45. Fedha hizi hadi kufikia sasa 2009 pamoja na hesabu ya riba zinafikia takriban bilioni 28,” alidai Rostam.

Alidai kuwa mbali na fedha hizo za NBC, alimtuhumu Mengi kwa kuchukua fedha nyingi kupitia msaada wa nchi wafadhili wa kuagiza bidhaa kutoka nje (CIS), ambazo anadai hajazilipa hadi leo.

“Wafanyabiashara wengi tulikopa, lakini tumelipa na tunaendelea kulipa. Mengi anayedai ana uchungu na Watanzania anawaongezea umasikini kwa kuchota fedha hizo na baadaye kuruka na kukataa kuzilipa hadi leo,” alidai Rostam na kuorodhesha kiasi hicho cha fedha alichokopa Mengi.

Aidha, alimtuhumu Mengi kwa kutumia nafasi yake ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji ya Kampuni ya NICO kukiuka maadili ya kibiashara na kuitumbukiza katika kununua hisa za kiwanda cha Interchem Pharma Ltd ambacho alisema kinamilikiwa na familia ya Mengi, wakati akijua kilikuwa njiani kufilisika.

“Huku akijua hali mbaya ya kiwanda hicho alitumia nafasi yake kuziteketeza Shilingi bilioni 2.558 fedha za Watanzania masikini wasiopungua 22,000 wenye hisa katika NICO kwa kuifanya inunue asilimia 51 ya hisa (majority shareholding). Kiwanda hicho sasa kimewekwa kwenye orodha ya kufilisiwa baada ya kushindwa kujiendesha chini ya mwaka mmoja tokea Mengi kuizamisha NICO,” alidai.

Alimtuhumu pia akiwa mbia na serikali katika kiwanda cha TANPACK, alitumia dhamana ya kiwanda hicho kisirisiri kwenda kukopa Sh milioni 600 kwa NBC na kuzitumia kwa njia anazozijua, na alitaka deni lilipwe na mbia mwenzake, ambaye alikataa kulitambua na hivyo TANPACK ikafilisiwa.

Mbali na hayo, Rostam alidai kwa ujumla Mengi si msafi kama anavyotaka jamii iamini, ikiwamo kutaja ugomvi wake na watu mbalimbali, uanzishaji wa magazeti kwa nia ya kuwachafua wagomvi wake na zaidi akadai ndiye kinara wa kuchafua wenzake kwa lengo la kuleta chuki na mifarakano nchini.

“Najua atakanusha haya kwa sababu yeye ni mwepesi wa kulalamika kuwa anaonewa huku akidhani amepewa haki na Mungu ya kuonea wengine,” alisema Rostam na kuongeza kuwa hatua ya Mengi kuwaita wengine wauaji pasipo kutoa ushahidi wowote na pia kurejea madai ya kutaka kuuliwa au kudhuriwa mara kwa mara ni dalili ya kuchanganyikiwa.

Alisema mbali ya Mengi kumtuhumu yeye na wengine kuwa na akaunti ya fedha za kigeni nje ya nchi ambako ndiko wanakoweka fedha zao, alidai Mengi ndiye mwenye akaunti ya fedha za kigeni nje ya nchi. “Nampa changamoto akanushe kwamba hana akaunti ya fedha za kigeni nje ya nchi,” alisema.

“Niseme kwamba tofauti na yeye ambaye ameishia kutoa porojo zake bila ya kufikisha hoja na ushahidi wake kwa vyombo vya sheria vinavyohusika au kutoa ushahidi, mimi nawagawia hapa baadhi tu ya ushahidi wa ufisadi wa Mengi ambao pia nakusudia kuuwasilisha pamoja na maelezo haya kwa vyombo husika ili wamchunguze Mengi na kuchukua hatua zipasazo,” alisema Rostam.

“Kwa upande mwingine, nimewaagiza wanasheria wangu kuzifanyia kazi tuhuma za uzushi alizozitoa na kuchukua hatua za kisheria zinazofaa dhidi yake,” alisema Rostam na kuongeza kuwa atawasilisha ushahidi huo kwa vyombo husika ndani ya saa 48.

Alisema aliamua kumjibu Mengi kwa sababu alishindwa kuwasilisha ushahidi wa tuhuma alizotoa dhidi yake kwa vyombo vya sheria vinavyohusika na pia kumwomba radhi.

“Na nilimwambia wazi kuwa asipofanya mojawapo kati ya hayo, nitakuwa na haki ya kumuanika ili Watanzania waelewe tabia na hulka ya mtu huyu. Hakufanya chochote kati ya hayo. Na hawezi kufanya hivyo kwa sababu anaelewa alichokisema ni uzushi alioutunga mwenyewe,” alisema Rostam na kuongeza kuwa hiyo ndiyo sababu ya kuitisha mkutano wa jana ili kuweka kumbukumbu sahihi.

Mbunge huyo akijibu maswali ya waandishi wa habari, alisisitiza kwamba hahusiki na kashfa mbalimbali zinazotajwa kumhusisha naye na kueleza kuwa kashfa hizo zimeenezwa ili jamii iamini ni za kweli, wakati ni uongo. Alirudia kutoa changamoto kwa ye yote mwenye ushahidi kumpeleka mahakamani.

Wiki iliyopita, Mengi aliitisha mkutano na waandishi wa habari na pia kusoma taarifa katika televisheni anayoimiliki ya ITV, akiwatuhumu wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia akiwamo Rostam, kuwa ni mafisadi papa, lakini pia kutaja ushahidi akisema yuko tayari kushitakiwa.

Watawala wasioheshimu utawala wa sheria, wanatawalaje?

KUNA kila dalili kuwa watawala wetu wana tatizo la kuheshimu utawala wa sheria.

Kuheshimu huko kunaonyeshwa kwa njia moja tu nayo ni kuifuata sheria na kutekeleza kile sheria inataka kwa namna yoyote ile.

Matukio kadhaa ya hivi karibuni yanazidi kunifanya niamini kuwa watawala wetu wanataka kutawala kwa hisia, vionjo na mitazamo yao binafsi, wakiamini kuwa vitu hivyo kwa namna moja au nyingine vina uhusiano wowote ule na sheria.

Sasa, kama mtu anayeonyesha kutokujali sheria ni mtu wa ngazi ya chini, ambaye hana madaraka makubwa, tunaweza kusema kuwa anahitaji kupelekwa semina au mafunzo fulani au kupewa maelekezo ya nini cha kufanya.

Lakini inapotokea kuwa mtu anayeonyesha kutokufuata sheria na kuheshimu utawala wa sheria ni waziri au kiongozi wa ngazi za juu serikalini, basi kiwango cha matatizo kinakuwa kimeongezwa kwa kasi ya ajabu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi) Hawa Ghasia wiki iliyopita alisema kitu bungeni ambacho kilinikumbusha alichosema Waziri Mkuu miezi michache iliyopita pale alipohalalisha uvunjaji wa sheria tena kwa machozi.

Wote wawili japo kwa namna mbalimbali wameendelea kuthibitisha kila ambacho wengi tunakijua, tumekishuhudia na kwa muda mrefu tumekivumilia yaani, sheria inafuatwa pale wanapojisikia, na pale wanapotakiwa kuifuata wanajizuia kwa kusingizia kujisikia.

Kwa Waziri Mkuu alipozungumzia lile suala la mauaji ya albino tulipiga kelele na kwa machozi yake akatutuliza. Lakini baadaye akaenda Iringa ambako huko nako akasema maneno fulani ambayo japo hayakupata mbiu kubwa kwenye vyombo vya habari lakini kimsingi yalikuwa yanaingilia utendaji kazi wa Mahakama kuhusiana na viongozi wa serikali kumfungulia mashtaka kiongozi mmoja wa CCM.

Lakini kilichonishtua zaidi ni haya ya mama Ghasia. Wengi walioandika juu ya kauli yake walikwazwa zaidi na suala la nyaraka kuwa ni za siri na wanaovujisha watachukuliwa hatua. Binafsi kilichonikwaza zaidi ya hicho ni madai kuwa kwenye Bunge letu kuna wezi!

Soma zaidi