Thursday, June 18, 2009

Tamasha la Jinsia 2009


Mtandao wa Mashirika Watetezi wa Haki za Binadamu na Jinsia nchini Tanzania (FemAct), Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) tunayo furaha kubwa kutangaza rasmi Tamasha la Jinsia la Mwaka 2009.

Mahali:Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Mkabala na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)

Tarehe: 8 Septemba - 11 Septemba 2009

Mada Kuu: "Rasilimali Ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni"

Mada zitakazojadiliwa:

(1)Heshima ya Mwili na Ujinsia
(2)Haki za uchumi na maisha endelevu
(3)Maarifa, Sanaa na Utamaduni
(4)Siasa, Uongozo na uwajibikaji
(5)Virusi vya Ukimwi na Ukimwi: Zaidi ya Uhai

Malengo ya Tamasha la Jinsia 2009
1.Kusisitiza na kuimarisha vuguvugu la ukombozi wa wanawake kimapinduzi, kutengeneza nafasi kwa ajili ya: kuibua, kubadilishana, na kuanzisha fikra, uchambuzi na kutengeneza mikakati ya pamoja kwenye suala la rasilimali kuweza kunufaisha wanawake walioko pembezoni;

2.Kusherekea nguvu zetu za pamoja, kupanua na kuimarisha ushirikiano katika vuguvugu la kuwakomboa wanawake kimapinduzi katika ngazi na sekta zote za kijamii;

3.Kuimarisha kujinoa na kuongeza uwezo wa kuchambua, kutafiti na kutathamini masuala yahusuyo Jinsia na harakati za ukombozi wa wanawake na wanyonge wengine kote duniani na

4.Kuandika nyaraka na kusambatisha maarifa kuhusu harakati za ukombozi wa wanawake dunia na kuchangia kwenye mjadala wa mada kuu ya Tamasha la Jinsia 2009 na ile ya la Jinsia, Demokrasia na Maendeleo.

Ushiriki wako wako unaweza kuwa katika:
•Kuandaa mada na mawasiliano mbalimbali kwa njia tofauti (sanaa, wimbo, shairi, mjadala, paneli, n.k) kwenye warsha kutokana na masuala yaliyo tajwa hapo juu;
•Kuandaa na kuratibu warsha na mijadala ya kujenga uwezo;
•Kualika na kuwezesha ushiriki mtu mmoja mmoja au vikundi kwa ajili ya kuhudhuria Tamasha;
•Kutengeneza na kufanya maonesho ya vitabu, picha, kazi za mikono n.k;
•Kuandaa maonesho ya sanaa, tumbuizo, ngoma, michezo ya kuigiza n.k;
•Ushiriki katika mijadala ya warsha na semina za Tamasha;
•Kuchangia gharama za wale watakaohudhuria, na/au waandaaji wa Tamasha.

Tutafarijika sana endapo mtajiandikisha kwa wingi mapema iwezekenavyo kwa kulipa ada ya ushiriki TGNP mapema. Lugha rasmi za Tamasha ni Kiswahili na Kingereza. Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kupitia barua pepe: gf_coordinator@tgnp.org Simu: +255 754 784050, +255 715 784050 na +255 22 2443450/2443205/2443286 au tembelea tovuti yetu www.tgnp.org

No comments: