Tuesday, November 30, 2010

Kikwete awaonya Mawaziri

WAKATI Rais Jakaya Kikwete akiwa katika ngwe yake ya mwisho ya uongozi wa nchi ameonesha kuwa mkali kwa mawaziri wake wapya aliowateua hivi karibuni.

Kikwete amewaeleza wazi kuwa safari hii hana simile wala subira kwa Waziri atakayeboronga katika utekelezaji wa majukumu yake.

Rais Kikwete ametoa msimamo wake wakati anawapa majukumu mapya mawaziri hao na akagusia nyanja mbali mbali zikiwemo uwajibikaji, kufuata kanuni, sheria na pia kupambana na rushwa huku akisisitiza kuwa vita dhidi ya rushwa ni suala la kikatiba na kuwataka kuhakikisha kuwa Mpango wa Pili wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (NACSAP-11) unatekelezwa.

Akizungumza na Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu Dar es Salaam jana, Rais Kikwete aliwaeleza mawaziri kuwa katika kipindi hiki cha pili cha uongozi wake hakutakuwa na muda wa kupoteza.

Amesema, hatakuwa tayari kukubali maelezo ya kwa nini utekelezaji wa majukumu ya msingi umeshindikana na amewataka mawaziri kusimamia mapato ya Serikali yasiyotokana na kodi na kudhibiti matumizi ya Serikali.

Pia aliwataka viongozi hao kuzingatia maadili ya uongozi ikiwa ni pamoja na kusimamia sheria za nchi, kuheshimu sheria katika shughuli na mambo yao binafsi na kutunza siri za Serikali kwa mujibu wa kiapo chao.

Rais Kikwete pia alisisitiza umuhimu wa Mawaziri na Naibu Mawaziri kuwasiliana na wananchi kwa maana ya kueleza mafanikio na mipango ya Serikali katika kushughulikia matatizo ya wananchi.

Rais Kikwete aliwataka mawaziri hao kuvitumia kikamilifu vitengo vya mawasiliano ya Serikali katika wizara zao ambavyo ndivyo vyenye jukumu la kutoa taarifa kuhusu Wizara inavyotelekeza majukumu yake.

“Uzoefu unaonesha kuwa mawaziri wengi ni wazito kufanya mawasiliano na wananchi hata pale ambako Wizara imefanya mambo mengi mazuri. Hivyo, mawaziri muwe mstari wa mbele kuelezea mafanikio ya utendaji wa Serikali katika Wizara zetu,” alielekeza Rais Kikwete na kuongeza:

“Lazima ujengwe utamaduni wa kudumu wa kuwasiliana na wananchi wote ambao ndio waajiri wetu kupitia kura zao. Mawaziri wote tumieni vitengo vyenu vya mawasiliano na vyombo vya habari kwa ustadi ipasavyo”.

Akiwapongeza kuteuliwa kwao, Rais Kikwete alisema: “Mnastahili pongezi hasa ukizingatia ukweli kwamba nyinyi mmebahatika kuteuliwa kutoka kwenye orodha ndefu ya wabunge wengi wenye sifa za kushika nafasi mlizo nazo.

Nimewateua kwa imani kuwa pamoja nanyi, tutatimiza matumaini ya wananchi wa Tanzania waliokichagua Chama Cha Mapinduzi kiendelee kuongoza nchi yetu".

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, wakati akizungumza na wakuu wa idara katika wizara yake baada ya kutoka Ikulu aliwaambia kutokana na msimamo huo wa Rais Kikwete, yeye na naibu wake, hakuna kulala hadi matarajio ya wananchi katika wizara hiyo yatakapopatiwa ufumbuzi.

Dk. Kawambwa aliahidi changamoto ya kwanza kufanyia kazi ni kuhakikisha mikopo inayotolewa kwa wanafunzi wa elimu ya juu inaboreshwa, ili kuondoa malalamiko yasiyokwisha kutoka kwa wanafunzi hao.

Akiwa amefuatana na Naibu Waziri wake, Phillip Mlugo, Dk Kawambwa alikiri kuwapo tatizo kubwa la utoaji mikopo, hali iliyofanya wanafunzi karibu wote wa vyuo vikuu kuinyima kura CCM katika uchaguzi wa Oktoba mwaka huu. Licha ya mikopo pia aliahidi kuhakikisha maslahi ya walimu yanaboreshwa ili kuondoa uwezekano wa walimu kugoma.

“Natambua kuwa watoaji na wapokeaji elimu, wote wako kwenye matatizo, hili eneo nitashughulika nalo zaidi.

“Leo tulikuwa na mkutano na Rais (Kikwete) ametwambia wazi, kuwa safari hii hana simile wala subira, anachotaka ni watu tufanye kazi. Na sisi tunakuja hapa kwa hadhari kuwa hakuna kulala,” alisema Dk Kawambwa ambaye awali alikuwa Wizara ya Miundombinu.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Cyril Chami, akianza kazi rasmi aliahidi kuandika waraka kwa Baraza la Mawaziri, kuomba Serikali iboreshe viwanda ikiwamo kufufua vilivyokufa kwa kuvichukua na kurudi kwenye miliki yake.

Waziri huyo ambaye amepandishwa kutoka Naibu Waziri katika wizara hiyo, alisema:“Miaka mitatu nyuma, tulifanya ukaguzi wa viwanda vyote na tukajua kwa nini vingine vilifungwa au havijaanza kazi na sasa tunataka vifanye kazi”.

Akizungumza na gazeti hili mara baada ya kupokewa rasmi wizarani hapo na wafanyakazi huku akifuatana na Naibu wake, Lazaro Nyalandu, alisema baadhi ya viwanda vilivyoshindwa kufanya kazi vitawezeshwa ili vifufuke.

“Kuna viwanda vingine tumeona wamiliki wameshindwa kuzalisha bidhaa walizoomba awali na wanataka kubadili aina nyingine, nao tutawasaidia wazalishe wanachoweza baada ya kutetea hoja zao,” alisema.

Kwa upande wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, wakati akizungumza na wafanyakazi wa wizara yake, alisema baada ya miaka miwili, watu watajua upole na ujana wake ukoje, kwani anaamini atakuwa amefanya kazi vizuri na kwenye hilo, hana shaka nalo.

Alisema licha ya kutegemea kuteuliwa katika wizara hiyo nzito, atatekeleza Ilani ya CCM kwa kasi zaidi, huku akiahidi kuhakikisha sheria zote zilizotungwa kusimamia maliasili vikiwamo vitalu na wanyamapori zinasimamiwa ipasavyo.

Alisema anaamini kutokana na kuwekwa sheria za uwazi na shirikishi, mianya ya rushwa na vitendo vyake wizarani hapo vitakwisha.

Kwenye Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Waziri Dk Haji Mponda, aliwataka wafanyakazi wa wizara hiyo, kushirikiana kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

Dk Mponda alitaja changamoto kubwa kwa wafanyakazi wa sekta hiyo kuwa ni kutoa huduma bora za tiba katika vituo vyote vya afya nchini ili kuinua uchumi wa nchi “Mtanzania wa leo anataka huduma bora za tiba … mtu anapoingia hospitalini au kwenye zahanati anachotaka ni kumwona mganga na kupata huduma bora, hivyo kila mtoa huduma hana budi kuwajibika katika hilo.”

Miongoni mwa mawaziri walioanza kazi kwa cheche ni wa Ujenzi, John Magufuli ambaye juzi aliagiza Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) kusimamisha nafasi za kazi za mameneja wa mikoa zilizotangazwa kwenye vyombo vya habari na kuamuru mameneja wote waliosimamishwa kazi warejee kazini.

Wakati huo huo, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na mashirika yapatayo 50 yanayotetea usawa wa kijinsia, haki za binadamu na ukombozi wa wanawake kimapinduzi (FemAct), yamepongeza uteuzi wa mawaziri na naibu mawaziri uliofanywa na Rais Kikwete Novemba 24 mwaka huu.

Hata hivyo, taarifa ya FemAct iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi, ilielezea kutoridhishwa na idadi ndogo ya mawaziri wanawake na pia ukubwa wa Baraza hilo kwa jumla.

“Idadi ya wanawake walioteuliwa kuwa mawaziri ni ndogo sana. Katika uteuzi huu, jumla ya mawaziri ni 29, kati yao wanaume ni 22 sawa na asilimia 76 na wanawake ni wanane, sawa na asilimia 24.

“Naibu mawaziri ni 21, wanaume ni 18 sawa na asilimia 86 na wanawake ni watatu sawa na asilimia 14. WanaFemAct walitarajia kuwa hiki kilikuwa kipindi mwafaka cha kufikia uwiano wa 50:50 ingawa mikakati iliyowekwa na fursa zilizokuwapo hazikutoa fursa hiyo,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Monday, November 29, 2010

Sitta: Tanzania haiuzwi

MAWAZIRI wateule jana waliapishwa kuanza kutekeleza majukumu waliyopewa serikalini.

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akisema wamekabidhiwa madaraka hayo kwa umakini ili asijetokea mtu akauza nchi.

Akizungumza muda mfupi baada ya kumaliza kupiga picha ya pamoja na Rais Jakaya Kikwete mara baada ya mawaziri hao na naibu mawaziri kula kiapo chao, Sitta alisema kazi waliyopewa inahitaji ujuzi wa kila namna.

“Kubwa la kuzingatia ni uzalendo, hii kazi (ya Uwaziri wa Ushirikiano Afrika Mashariki), humpi mtu tu, anaweza kutuuza,” alisema Sitta wakati akifafanua changamoto zinazomkabili katika wadhifa huo ambapo awali alianza kwa kumshukuru Rais Kikwete kwa kumteua kushika nafasi hiyo.

Alitamba kuwa utendaji wa kasi na viwango, sasa umehamia serikalini na kushangaa watu wanaoona kuwa atashindwa kupiga vita ubadhirifu kutokana na nafasi yake kama Waziri.

“Wakati ule nilikuwa nje, sasa nimeingia ndani ndio nitajua hali halisi ilivyo na kusaidia. Kwanza tutahakikisha sheria mpya ya maadili ya viongozi inapitishwa haraka.

“Unajua wananchi wanapata shida katika imani yao kwa Serikali hasa wanapomuona mtu aliyepata madaraka, ghafla ana pauni huko Uingereza na nyumba Ufaransa, tutapigia kelele hilo,” alisema Sitta ambaye alikuwa Waziri wa kwanza kuapa.

Alisisitiza nia ya kutetea kuwasilishwa bungeni haraka kwa muswada wa sheria mpya ya maadili ya viongozi ambayo inalenga kutenganisha biashara na siasa, ni ili kuepuka viongozi ambao wanatumia nafasi zao kujitajirisha wenyewe.

“Huwezi kutajirika katika siasa, kwa mfano mimi natakiwa Arusha Jumatatu na nitakuwa ofisini kuanzia asubuhi mpaka usiku, hiyo biashara utafanya saa ngapi halafu tunaambiwa wenzetu ni wachakarikaji, hakuna kuchakarika hapo.

“Ushahidi wa kwanza wa mwanasiasa mla rushwa ni kutajirika ghafla, labda kama aliingia madarakani akiwa na utajiri wake,” alisema Sitta na kujitolea mfano kuwa aliingia serikalini mwaka 1974 akitokea Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kama ofisa na katika hali hiyo asingeweza kujenga nyumba nje ya nchi.

Kuhusu umuhimu wa wizara hiyo kwa sasa, Sitta alisema Tanzania inakwenda kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na katika hilo maslahi ya Watanzania yanatakiwa kulindwa.

Alisema pia kuna changamoto ya kuwaondolea Watanzania hofu ya kuwa baada ya Shirikisho, watapata shida ikiwemo ya kukosa nguvu za kiuchumi na kuhusu mamlaka ya viongozi wao kama Rais.

“Tutaangalia mikataba na kuhakikisha tunaingia katika Shirikisho kwa kuzingatia maslahi ya Watanzania hasa katika ardhi na ajira yanalindwa,” alisema Sitta na kutamba uwezo wake katika sheria na uzoefu serikalini wa karibu miaka 36 umemfanya kuwa mtu mwenye kuweza kazi hiyo.

Alisema, alipoachia aliyekuwa Waziri katika Wizara hiyo, Dk. Diodorus Kamala ndipo atakapoanzia yeye na kusifu uteuzi wa Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk. Abdallah Juma Abdallah kuwa ni mtu mzuri atakayesaidiana naye kazi.

Alikiri kuwa Tanzania iko nyuma ikilinganishwa na baadhi ya nchi wanachama wa umoja huo na kuongeza kuwa atajitahidi kuomba muda katika mambo kama ardhi na ajira ili nchi isigeuke kama “shamba la bibi”. Alisema pia ataomba kuongezewa bajeti katika jukumu la kutoa elimu kwa Watanzania ili EAC ifahamike na kuondoa hofu.

Magufuli amkaanga bosi wa Tanroads

SIKU moja baada ya kuapishwa,Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli amemtaka Mkurugenzi wa Wakala wa Barabara (Tanroads), Ephraim Mrema kusimamisha mara moja nafasi za kazi za mameneja wa mikoa alizozitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa zipo wazi.

Magufuli amewataka mameneja wote ambao wamesimamishwa kazi, warudi kazini mara moja na kwamba tangazo hilo halina nguvu.

Kutokana na uamuzi huo, Dk. Magufuli amemtaka Mrema kutoa tangazo haraka kuanzia leo katika vyombo vya habari, kusitisha tangazo lake la awali la kuwasimamisha kazi mameneja wa Tanroads mikoani kwa kuwa hatua aliyoichukua inaonekana ni ya kulipizana visasi.

Dk. Magufuli alitoa maagizo hayo jana, Dar es Salaam katika mkutano wake na wakuu wa idara na vitengo mbalimbali vya wizara hiyo wakati akijitambulisha kwao.

Katika maagizo yake, Dk Magufuli alimtaka Mrema asifanye kazi kama mtu anayeondoka kesho, bali atekeleze majukumu yake kama atafanya kazi hiyo kwa miaka 100 ijayo.

“Tanroads jipangeni sawasawa, blaablaa ziishe, wewe Mkurugenzi uliona nafasi yako inatangazwa na wewe ukaamua kutangaza za mameneja wa mikoa ili kuchomeana na kila kitu kisimamishwe, kwanini ulitangaza kwamba waliopo hawachapi kazi?”

Alihoji Dk. Magufuli. Aliagiza mameneja wa mikoa waelezwe mara moja kuwa wamerudishwa kazini isipokuwa kwa nafasi ya Dodoma tu ambayo meneja wake hayupo. “

Nakuagiza Mrema, uandike katika vyombo vya habari kuwa umefuta tangazo hilo na mengine yatafuatia.”

Alimtaka Mkurugenzi huyo wa Tanroads, kufanya kazi kwa ushirikiano na kwamba kama Waziri na Naibu wake Dk. Harrison Mwakyembe watauliza jambo lolote, wajibiwe haraka, la sivyo itakuwa ni dharau.

Mkurugenzi huyo wa Tanroads inadaiwa kipindi chake cha kuongoza wakala huo kimemalizika kwa mujibu wa mkataba wake wa kazi, lakini ameendelea kukalia ofisi hiyo.

Dk. Magufuli alisema wao hawakufika katika wizara hiyo kwa ajili ya kutengua Torati, bali kuitekeleza na kwamba wanaweza kufanya kazi na yeyote na kusisitiza kuwa yaliyopita yaachwe na wafanye kazi kwa pamoja.

“Tushirikiane, tupendane, majungu yaishe, tuache rushwa kwa kuwa tutawategeshea hata fedha ya Polisi… na hivi ndio maana Rais ametuteua mimi na Naibu mwenye taaluma ya Sheria,” alisema.

Kuhusu rushwa, waziri huyo aliahidi kupanda lori lililozidisha uzito na kutoa rushwa na akasema akikamilisha kazi hiyo watakaohusika watamtambua. Aliwataka watendaji wa mizani kusimamia sheria, kukamata magari na kupiga faini na kuteremsha mizigo bila kujali mmiliki wa gari au mzigo.

Awali akizungumza katika mkutano huo, Dk. Mwakyembe, alisema uteuzi wao hautakuwa na maana kama wataachia kirusi aliyeingia katika Wizara hiyo na kutia doa kuendelea.

Alisema mwanzoni wizara hiyo ilikuwa mfano wa kuigwa lakini anashangaa kuona ufanisi umepotea na sasa imekuwa sehemu ya kunyoosheana vidole bila kujua ni kirusi gani huyo aliyeingia.

Alisisitiza kuwa sasa wanahitaji kuongea lugha moja na kuimba wimbo mmoja na kuifanya wizara hiyo kuwa ya mfano na kuagiza taarifa za kukinzana zisipewe nafasi kwa kuwa hawaendeshi wizara kwa majungu na umbeya.

Thursday, November 25, 2010

Familia ya Lowassa yapelelezwa London

-Polisi Uingereza wamchunguza mwanawe
-Washitushwa na uhamishwaji wa Sh.bil. moja
MTOTO wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa anayeitwa Frederick Lowassa anachunguzwa na Kitengo Maalumu cha Polisi wa Kimataifa wa Uingereza wanaofuatilia utata wa uhamishaji fedha kutoka Tanzania, Raia Mwema limedokezwa.

Fedha hizo zinahusishwa na ununuzi wa nyumba yenye thamani ya pauni za Uingereza 475,000 (takriban Shilingi bilioni moja) katikati ya Jiji la London, .

Hata hivyo, watu walio karibu na Frederick wameelezea kwamba kijana huyo hakuwahi kununua nyumba; bali aliwahi kutaka kupanga kwa ajili ya kuishi akiwa masomoni nchini Uingereza na fedha nyingine alizituma kwa ndugu yake aishie nchini humo.

Nyumba ambayo inatajwa katika maelezo ya awali iko mtaa wa Leinster Gardens, jijini London.

Hata hivyo, hakuna ofisa yeyote wa Serikali ya Tanzania aliyekuwa tayari kuzungumzia suala hilo, pamoja na kuwapo taarifa kwamba tayari vyombo vya dola vya Tanzania vimekwisha kuhusishwa katika uchunguzi huo.

Maofisa wa Polisi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (CID) wanaohusika na uchunguzi wa fedha haramu, wamekwepa kuzungumzia suala hilo na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Robert Manumba, hakuweza kupatikana, na alielezwa kuwa nje ya nchi kikazi.

Ofisa wa CID aliyeelezwa kuongoza kitengo kinachochunguza makosa ya uhalifu wa fedha na nyaraka, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Samson Kasala, alikanusha kufahamu chochote kuhusiana na suala hilo, kabla ya kukata simu alipohojiwa na Raia Mwema kuhusu taarifa hizo.

Taarifa zinaeleza kwamba Kitengo cha Ufuatiliaji wa Fedha Haramu (Financial Intelligence Unit-FIU) kilichopo chini ya Wizara ya Fedha nchini, kilipokea taarifa kutoka Polisi wa Kimataifa wa London, Uingereza, wakitaka taarifa muhimu kuhusiana na Frederick, kabla ya kitengo hicho kuomba msaada wa polisi.

Hata hivyo, Kamishna wa FIU, Herman Kessy, hakuweza kupatikana wiki iliyopita akielezwa kuwapo nchini Afrika Kusini kikazi, lakini hata aliporejea wiki hii Raia Mwema ilikosa ushirikiano kutoka kitengo hicho Jumatatu wiki hii.

FIU imeanzishwa chini ya Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu ya mwaka 2006 (Anti-Money Laundering Act-2006) kwa kuundiwa kanuni mwaka 2007, lakini hadi sasa kitengo hicho kimekuwa kikiendeshwa na maofisa watano tu, Kamishna Kessy, mchambuzi mmoja, mtaalamu wa mawasiliano na wasaidizi wawili wasio wataalamu, kitengo kilichopaswa kuendeshwa na watu wengi zaidi kutokana na unyeti wake.

Habari zinaeleza kwamba hata ofisa wa Polisi aliyewahi kuhamishiwa FIU kwa kazi maalumu alijikuta akitengwa na kutopangiwa kazi na maofisa hao ambao wengi wanatoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), baada ya kuwa ‘wameaminiwa’ sana na uongozi wa juu wa serikali.

Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo bado zinafanyiwa kazi, Frederick ambaye baba yake alijiuzulu Waziri Mkuu kwa kuhusishwa na kashfa ya ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme iliyokabidhiwa kwa kampuni tata ya Richmond Development LLC, anadaiwa kufanya mawasiliano kupitia kampuni ya uwakala iliyotajwa kwa jina la ‘Mishcon’.

Nyaraka alizowasilisha, zilidai kuwapo ubia kati ya mtuhumiwa huyo na kampuni tatu ikiwamo Integrated Property Investment(T) Ltd na Barare Ltd Company.

Mkataba huo unaonyesha kuwa Frederick Lowassa ana hisa kwenye kampuni hizo, na kwamba fedha za ununuzi wa nyumba hizo zinatokana na fedha za malipo ya hisa anazopata kutokana na kampuni hizo.

Hata hivyo, mkataba huo unaonyesha kusainiwa Machi 25 mwaka 2009 siku moja baada ya Frederick Lowassa kusaini mkataba kati yake na kampuni ya Mishcon kama wakala wake katika ununuzi wa jengo hilo.

Pia aliwasilisha nyaraka zinazoihusisha kampuni ya Alphatel kama moja ya kampuni ambayo pia yeye ni mkurugenzi wake ambayo pia ni chanzo chake kingine cha fedha anazotumia kununua jengo hilo.

Taarifa zimedokeza kuwa ununuzi huo ulikwama baada ya kushindwa kutoa malipo hayo kwa mujibu wa mkataba kati yake na wakala wa ununuzi wa nyumba hiyo (kampuni ya Mishcon) ambao ulimtaka awe amekamilisha kulipa fedha hizo kabla ya Aprili 14, mwaka 2009.

Hata hivyo, siku chache baadaye ndani ya mwezi huo wa Aprili, Frederick aliipelekea Mishcon kiasi cha pauni za Uingereza 199,940 zikitokea kwenye kampuni ya ununuzi fedha ya Wall Street Exchange.

Aidha kiasi cha pauni 100,000 kiliingizwa kwenye akaunti ya kampuni hiyo hiyo ya Mishcon kwa fedha taslimu katika mikupuo 12 tofauti zikitokea kwenye matawi tofauti ya benki ya NatWest Bank plc iliyoko Kaskazini mwa Jiji la London.

Raia Mwema limeelezwa kuwa mazingira ya kuingizwa fedha hizo kwenye akaunti ya wakala huyo ( Mishcon) ndiyo yameifanya Taasisi ya SCD 6 Economics and Specialist Proceeds of Corruption Unit ya Uingereza inayosimamia uchunguzi wa sakata hilo kuwa na mashaka makubwa kuhusu uhalali wa fedha hizo.

Kutokana na mazingira hayo, SCD 6 Economic and Specialist Crime Proceeds of Corruption Unit yenye ofisi zake Victoria Block, New Scotland Yard, London, ililazimika kuwasiliana na FIU ikitaka maelezo ya awali kuwezesha kufanyika kwa uchunguzi kuhusu fedha hizo.

Raia Mwema iliwasiliana na Fred ambaye alikana kununua nyumba Uingereza lakini alikiri kuwahi kutuma fedha huko. Aliliambia Raia Mwema pia kwamba hajawahi kuhojiwa na yeyote kuhusu suala hilo, na pia kwamba hana taarifa kuwa polisi wa Uingereza wanampeleleza.

Hata hivyo kwa upande mwingine, gazeti hili limebaini kuwa, maelezo ya awali ambayo yalitakiwa kutoka Tanzania na makachero hao wa Uingereza, ni pamoja na kutaka kufahamu kama kweli Frederick Edward Lowassa amezaliwa Agosti 26, 1977, Mwanza Tanzania na anamiliki hati ya kusafiria yenye namba AB 109402 iliyotolewa Tanzania na kwamba anwani yake nchini Uingereza ni 71 Hendrix Drive, Milton Keynes, MK8 0DY.

Pia makachero hao waliitaka Serikali ya Tanzania kutoa ufafanuzi wakitaka kujua kama Frederick Lowassa ni mbia katika kampuni za Alphatel Partnership (Tanzania) Barare Ltd na Intergrated Tanzania Limited, kampuni ambazo zimefahamika kumilikiwa na familia ya Lowassa.

Asasi hiyo ya Uingereza pia imeomba kujua kama FIU wana taarifa zozote za uhalifu dhidi ya Frederick Lowassa na kama baba yake Edward Lowassa anachunguzwa kwa tuhuma yoyote ya rushwa na mamlaka za uchunguzi wa rushwa nchini Tanzania kuhusu fedha haramu.

Uchunguzi wa awali uliofanywa na vyombo vya dola, ulielezwa na taarifa hizo kwamba Frederick Lowassa si mbia katika kampuni hizo na kwamba Barare Ltd wenye hisa ni Edward Ngoyai Lowassa mwenye hisa 500 na Regina Mumba Lowassa mwenye hisa 500 huku wakurugenzi wakiwa ni hao hao.

Ofisa wa Uingereza anayesimamia uchunguzi huo, George Simpson, ameliambia Raia Mwema kupitia barua pepe kwamba kanuni za uchunguzi kuhusiana na kesi zenye mguso wa kisiasa huwazuia kukanusha au kuthibitisha kuhusu uchunguzi unaoendelea hadi pale wanapofikia hatua ya kukamata mtuhumiwa ama anapofikishwa mahakamani.

Wednesday, November 24, 2010

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI HILI HAPA

TANZIA


Mtandao wa Mashirika yapatayo 50 yanayotetea Usawa wa Kijinsia, Haki za Binadamu, Maendeleo na Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi (FemAct), tunaomboleza kuondokewa na Mpendwa wetu, dada Mary Mwingira, mpiganaji wa muda mrefu wa haki za wanawake na haki za kijamii, aliyefariki siku ya jumapili usiku, tarehe 21 Novemba 2010, baada ya kuugua saratani kwa muda mrefu. Tunapenda kumuenzi kwa mchango wake katika ukuaji na uimarishwaji wa mashirika ya kijamii hapa Tanzania. Mary Mwingira aliongoza wanawake na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayojishughulisha na masuala ya kijinsia hapa Tanzania kushiriki katika Mkutano wa Ulimwengu wa muongo wa Wanawake uliofanyika Nairobi, Kenya, mwaka 1985, wakiunga mkono mashirika mbalimbali kutoka ngazi za kijamii hadi kitaifa na kupata fursa ya wazo mbadala wakati wa Kongamano la mashirika yasiyo ya kiserikali huko Nairobi, pamoja na kubadilishana mawazo na kuunga mkono ujumbe wa kiserikali. Mchakato huu ulipelekea kuanzishwa kwa TANGO, jumuiya mama ya mashirika yasiyo ya kiserikali Tanzania, ambayo Mary Mwingira aliiongoza kwa miaka mingi kama Mkurugenzi Mtendaji. Mary pia alikuwa mwanachama mwanzilishi wa taasisi mbalimbali za wanawake na haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na Taaluma Women and Christian Professionals of Tanzani, na pia alishiriki katika Kongamano la kijamii la Ulimwengu, Nairobi.

Kati ya 1992/1993, Mary Mwingira pamoja na vikundi vya viongozi wengine wa vikundi vya wanawake na jinsia walishiriki katika mchakato wa pamoja katika kutafakari na kupanga mikakati ambayo iliongozwa na waanzilishi wa Mtandao wa jinsia Tanzania katika kuandaa Kongamano la Wanawake la Ulimwengu lililofanyika Beijing, China, mwaka 1995. Kwa kutumia mbinu shirikishi za uraghibishi na uchambuzi wa ukombozi wa wanawake kimapinduzi, viongozi hawa wanawake wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali walifanya kwa pamoja uchambuzi wa kina wa nafasi ya wanawake hapa Tanzania, mfumo dume na mfumo wa utandawazi kibeberu iliyoendelea kuwakandamiza na kuwanyonya wanawake wakati wa mfululizo wa warsha hizo tatu, na hatimae kupanga kwa pamoja mikakati iliyokuwa inahitajika kwa ajili ya kuendeleza haki za wanawake, usawa wa kijinsia na mabadiliko ya kijamii. Mawazo haya baadaye yaliwasilishwa na viongozi wa TGNP kwa niaba ya Kikundi cha Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Tanzania katika Mkutano wa Maandalizi wa nchi za Kanda ya Afrika ya Mashariki Uliofanyika Uganda mwaka 1993, na kuchapishwa kama Hali Halisi ya Kijinsia Tanzania( Gender Profile of Tanzania), mwaka huo.

Mapema mwaka 1993, viongozi hawa hawa wa mashirika ya wanaharakati wa masuala ya wanawake na jinsia walidai wawezeshaji wa warsha waunde shirika jipya la kudumu na kufanya uchambuzi wa ukombozi wa wanawake kimapindu kwa kutumia mbinu shirikishi. Ni kutokana na mchakato huu TGNP iliweza kuzaliwa, ambapo iliandikishwa rasmi mwishoni mwa mwaka 1993, kwa mchango mkubwa wa Mary Mwingira, kwa upande wa ushauri na kutambulisha wafadhili. Muda mfupi baadaye, wengi kati ya viongozi hao hao wa Jumuiya zisizokuwa za kiserikali za wanawake na haki za kijinsia walianzisha FemAct, kwa ajili ya kuimarisha vuguvugu la ukombozi wa wanawake kimapinduzi na haki za binadamu katika ukuaji wa nguzu za pamoja. TANGO ni mwanzilishi wa FemAct na Mary Mwingira alibakia kuwa mshiriki imara katika mapambano mengi yaliyofanywa nchini Tanzania katika kukuza haki za wanawake na za kijamii kwa wote waliokandamizwa, walionyonywa na waliowekwa pembezoni.

FemAct inatuma salamu zake za rambiambi kwa familia ya Mary Mwingira, ndugu, jamaa na marafiki wote. Katika kipindi hiki cha maombolezo, tumkumbuke kwa uwezo wake wa kusimama imara katika mapambano ya kutetea haki, demokrasia na usawa wa kijamii katika ngazi zote.

Tunaiombea roho ya marehemu dada yetu, ilale mahali pema peponi, Amen.


Imetolewa na

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), kwa niaba ya FemAct.


Na kusaininwa na

……………………………
Lilian Liundi
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP

Monday, November 22, 2010

‘Panga’ lawasubiri manaibu waziri

IWAPO Rais Jakaya Kikwete atatekeleza matakwa ya wananchi ya kupunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri, kuna uwezekano kuwa nafasi zitakazopunguzwa ni za manaibu waziri.

Baraza lililomaliza muda wake lina manaibu waziri 21 huku Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi pamoja na Wizara ya Fedha zikiwa na manaibu waziri wawili kila moja huku wizara zingine 17 kati ya 26 zilizoundwa katika Baraza hilo zikiwa na naibu waziri mmoja.

Wizara saba hazina manaibu waziri, lakini wachambuzi wa mambo ya siasa wamedokeza kuwa kuna uwezekano Rais Kikwete akaendelea kupunguza idadi ya manaibu waziri ili kutoa fursa ya mawaziri kufanya kazi kwa karibu na makatibu wakuu wa wizara.

Kwa mfumo wa wizara, kila wizara ina Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu.

Wizara pia zina wakurugenzi wa idara mbalimbali ambao wanamsaidia Katibu Mkuu hali
iliyoelezwa kuwa inatoa fursa kwa waziri kumudu majukumu ya kazi hata pasipo kuwepo na naibu wake.

Waziri anayeteuliwa na Rais kazi yake kubwa ni kusimamia sera za Serikali iliyoko madarakani na kuhakikisha kuwa Ilani ya chama kilichoko madarakani itatekelezwa na wizara husika.

Makatibu wakuu ndio watendaji ambao mara zote wamekuwa wanasimamia maelekezo na sera za Serikali na kuhakikisha kuwa malengo yaliwekwa na wizara husika kwa kila mwaka yanafikiwa.

Ni kutokana na hali hiyo wachambuzi wanaamini kuwa Rais Kikwete atapunguza manaibu waziri katika baadhi ya wizara. Wizara ambazo kwa sasa hazina manaibu waziri ni Ardhi, Katiba na Sheria, Utawala Bora, Muungano, Utumishi, Sera na Uratibu na Bunge pamoja na Mazingira.

Wizara inayoweza kutokuwa na manaibu waziri ni Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambayo waziri wake mara nyingi shughuli zake zinafanywa na Mkuu wa Majeshi anayeshirikiana na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Wizara ya Jinsia, Wanawake na Watoto nayo inaweza isipewe naibu waziri pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi iliyoundwa na Rais Kikwete ili kuhamasisha ufugaji bora na uboreshaji wa sekta ya uvuvi.

Wizara nyingine ambayo inaweza isiwe na naibu waziri ni Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Wizara ya Kazi, Maendeleo ya

Vijana na Ajira. Wachambuzi hao pia wamebainisha kuwa ni ngumu Rais Kikwete kupunguza Baraza la Mawaziri hasa kutokana na vipaumbele vya Serikali yake ambavyo viko 13.

Baraza la sasa lina mawaziri 26 ukiacha Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Rais wa Zanzibar na Rais mwenyewe hivyo kulifanya Baraza hilo kuwa na watu 30.

Lakini Rais pia anaweza kuunganisha baadhi ya wizara ili kuleta ufanisi zaidi na kuepusha migongano ya kikazi, hali ambayo imefanya baadhi ya mambo yasishughulikiwe kutokana na wizara hizo kutupiana mpira.

Iwapo ataunda Baraza kwa kuzingatia vipaumbele hivyo ina maana kuwa kutakuwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi ili kukuza amani na usalama.

Pia kutakuwa na Wizara ya Muungano ambayo iko katika Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo kama atahitaji kupunguza Baraza, atalazimika kuchanganya na Mazingira ambayo nayo iko katika Ofisi ya Makamu wa Rais ili zishikwe na waziri mmoja badala ya mawaziri wawili kama ilivyokuwa hapo awali.

Katika hotuba yake ya kulizindua Bunge, Alhamisi iliyopita mjini Dodoma, Rais Kikwete alikiri kuwa zimebaki kero ndogo ndogo za Muungano, hali inayoonesha kuwa kwa kuwa suala hilo pia husimamiwa na kamati maalumu waziri wake lazima aongezewe majukumu ambayo wachambuzi hao wanahisi ni ya mazingira.

Lakini wengine wanasema kama Waziri huyo ataongezewa jukumu la mazingira, atalazimika kuongeza juhudi za kuhifadhi mazingira hasa wakati huu ambapo makali ya athari za mabadiliko ya tabianchi yanazidi kuiumiza nchi.

Katika Ofisi ya Rais, kunatarajiwa kuwepo na Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambavyo ni moja vya vipaumbele vyake.

Ili kutekeleza jukumu la kuimarisha uhusiano mzuri uliopo baina ya nchi jirani na mataifa mengine lazima, Rais ataunda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wizara hiyo ya Afrika Mashariki inaweza isiwe na naibu waziri huku Wizara ya Mambo ya Nje lazima itakuwa na naibu waziri ambaye atatoka sehemu moja ya Muungano kutokana na wizara hiyo kuwa ya Muungano.

Wamesema Wizara ya Maliasili na Utalii nayo lazima itakuwepo, lakini pia licha ya umuhimu wake wadadisi wanadokeza kuwa pia naweza kuwa na naibu waziri.

Lakini pia Rais anaweza kuunganisha Wizara ya sasa ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na mambo ya umwagiliaji akaiondoa kwenye Wizara ya Maji ambayo inaweza kubaki peke yake.

Kwa vile kilimo kinachosisitiziwa kwa sasa ni cha mwagiliaji, kuna uwezekano wizara hiyo ikawa moja.

Lakini kutokana na vipaumbele vya Serikali, matazamio ya kupunguzwa Baraza hilo yatakuwa ni madogo na kama akifanya hivyo, Rais anaweza kuua wizara tatu na kuziacha zingine 23 zikiendelea kuwepo, lakini kwa kiasi kikubwa akipunguza idadi ya manaibu waziri.

Rais Kikwete anatarajiwa kutangaza Baraza lake la Mawaziri siku yoyote wiki hii.

Friday, November 19, 2010

JK atoa vipaumbele miaka 5

RAIS Jakaya Kikwete amelizindua Bunge la 10 na kutaja vipaumbele vyake 13 atakavyovizingatia katika miaka mitano ijayo ya Serikali yake, huku akiahidi kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha za serikali.

Sambamba na hilo, ameeleza utayari wake kulivalia njuga na kuondoa nyufa za mgawanyiko wa kidini uliotokana na Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Rais Kikwete alisema “nitaboresha zaidi ukusanyaji wa mapato ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa pamoja na kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma…naahidi tutajipanga zaidi kusukuma kwa nguvu nidhamu na uwajibikaji katika Serikali Kuu na Serikali za Mitaa.”

Alitaja kipaumbele kingine ni kuhakikisha kunakuwa na umoja, amani na usalama na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unaendelea kudumu na kuimarika na kuahidi kero chache za Muungano zilizosalia ambazo hazijapatiwa ufumbuzi, kupatiwa ufumbuzi ulio muafaka kwa pande zote mbili.

Pia Serikali yake katika miaka mitano ijayo itaendeleza juhudi za kukuza uchumi na kupunguza umasikini kwa kuchukua hatua thabiti za kuharakisha mapinduzi ya kilimo, ufugaji, uvuvi na viwanda na kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara ili kuvutia wawekezaji wa ndani na nje.

Katika kufanikisha hilo, alisema bajeti ya kilimo itaendelea kuongezwa na kufikia asilimia 10 na kuhimizwa kilimo cha umwagiliaji; kuongeza juhudi za ujenzi wa viwanda vipya na kurahisisha taratibu za utoaji wa leseni za biashara na upatikanaji wa malighafi na ardhi.

Serikali ijayo itawawezesha wananchi kiuchumi na kuboresha mipango ya kusaidia wajasiriamali wadogo na wanaotaka kujiajiri, kuwatambua na kuwawezesha wajasiriamali wa kati, ili washiriki katika uwekezaji mkubwa wa ndani na nje ya nchi.

Rais Kikwete ameahidi kujenga na kuimarisha sekta binafsi na kutengeneza mazingira mazuri ya ushirikiano na sekta ya umma pamoja na kuifanya Tanzania kuwa lango kuu la biashara na usafirishaji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati hivyo kutaboreshwa miundombinu ya reli, barabara, viwanja vya ndege na teknohama.

Alitaja kipaumbele kingine ni kuongeza jitihada za kuhakikisha taifa linanufaika na maliasili zake kwa kuhakikisha kunakuwa na sera na sheria za uvunaji na matumizi ya rasilimali hizo zinazonufaisha taifa sawia ambapo sasa Shirika la Taifa la Madini (Stamico) kwa niaba ya serikali litaimarishwa ili kushiriki katika umiliki wa migodi mikubwa na ya kati na hivyo taifa kunufaika.

Vingine ni kukuza ajira hasa kwa vijana na kuongeza kasi ya kujenga majengo ya wafanyabiashara wadogo na kuongeza kuwa yatajengwa Dar es Salaam na Mwanza na baadaye katika miji mingine mikuu ya mikoa.

Alisema wataboresha elimu ya msingi na sekondari ambazo kwa sasa zinakabiliwa na changamoto na mkazo utakuwa katika masomo ya sayansi; kuboresha huduma za kijamii na uchumi kwa kuongeza fedha katika mifuko ya fedha, kuimarisha benki ya rasilimali na kuanzisha benki ya kilimo.

“Tutaendelea kutoa kipaumbele cha kwanza kwa bajeti ya elimu ili tufundishe na kuajiri walimu wengi zaidi, tupate vitabu na vifaa vya kujifunzia na kufundishia na kuongeza matumizi ya teknohama katika utoaji wa mafunzo na kujenga uwezo wa wanafunzi na walimu kiteknolojia ili kwenda sambamba na karne ya utandawazi,” alifafanua Rais Kikwete mbele ya wabunge.

“Tutaendelea kuimarisha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi yetu na majirani na mataifa mengine duniani na mashirika ya kimataifa na tutaendelea kutafuta marafiki wapya na kuboresha diplomasia ya uchumi na tutaongeza juhudi za kuhifadhi mazingira.”

Kwa upande wa afya, alisema huduma zitasogezwa zaidi kwa wananchi, kujenga uwezo wa ndani wa kutibu maradhi ili kupunguza watu wanaopelekwa nje kwa matibabu na bajeti ya afya itaendelea kuongezwa.

Kipaumbele cha mwisho ni kulinda mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na kukamilisha ahadi za mwaka 2005 ambazo hazijatekelezwa.

Rais Kikwete alisema mambo matatu aliyoyaahidi mwaka 2005 ataendelea kuyapa kipaumbele ambayo ni kuhakikisha nchi na watu wake wanakuwa wamoja na yenye utulivu na amani; kukuza uchumi na kupunguza umasikini na kuhakikisha demokrasia inastawi na serikali inaendeshwa kwa misingi ya utawala bora na kuendeleza mapambano ya rushwa na maovu katika jamii.

Akizungumzia kuhusu nyufa ya mgawanyiko wa kidini alisema; “hatuna budi kuchukua hatua za haraka kuziziba vinginevyo hatuna nchi, hatuna taifa, tutafanana na nchi nyingine tu. Nawahakikishia utayari wangu wa kushirikiana na wanasiasa wenzangu, viongozi wa dini na wa kijamii kulitafutia ufumbuzi suala hili.”

“Si vyema na si busara kuliacha likatoa mizizi na kulimong’onyoa taifa letu, nawaomba wenzangu mkubali tushirikiane tuinusuru nchi yetu,” alieleza Rais Kikwete. Kuhusu magereza, alisema, “tutalivalia njuga na kulipatia ufumbuzi muafaka tatizo kubwa la mlundikano wa wafungwa na mahabusu magerezani.”

Kwa upande wa kilimo na mifugo, alisema mavuno kwa mazao ya kilimo ya chakula na biashara yameendelea kuongezeka na mwaka huu, kipo chakula cha kutosha nchini.

Akizungumzia elimu, alisema Serikali yake itaendelea kutoa kipaumbele cha kwanza kwa bajeti ya elimu ili kufundisha na kuajiri walimu wengi zaidi, huku akisisitiza kwamba katika miaka mitano ijayo, “tutaendelea na upanuzi wa fursa za kupata elimu, lakini mkazo mkubwa tutauelekeza katika kuboresha elimu inayotolewa.”

Kuhusu mapato, alisema ukusanyaji mapato ya serikali umeongezeka kutoka wastani wa Sh bilioni 177.1 mwaka 2005 kwa mwezi hadi kufikia Sh bilioni 453 kwa mwezi hivi sasa, huku akiahidi kuongezwa maradufu jitihada za kukusanya mapato na kuimarisha matumizi ya serikali.

“Tutaboresha mfumo wa ukusanyaji mapato ya serikali na kupanua wigo wa walipa kodi. Tutakuwa wakali kuhakikisha mianya inayovujisha mapato inazibwa na pesa za umma zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa,” alifafanua Rais Kikwete na kuongeza: “Uzembe, wizi na ubadhirifu havitavumiliwa.

Tutaendelea kuzipa uzito unaostahili taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali na kuchukua hatua zipasazo kasoro zinapobainika. CAG akamate bila kusubiri Bunge.”

Akitoa hotuba ya kuahirisha Bunge, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alimpongeza Rais Kikwete kwa kutoa maelekezo mahsusi ya kutekeleza katika miaka mitano ijayo, akisema msingi wa maelekezo hayo ni Dira ya Maendeleo 2025, Mkukuta na Ilani ya Uchaguzi ya CCM na Malengo ya Maendeleo ya Milenia.

Alisema kama Waziri Mkuu anamuahidi Rais kuwa yeye pamoja na Baraza la Mawaziri litakaloundwa, kuwa karibu na wabunge, huku akieleza kuwa hotuba ya Rais inayo mambo mazuri kama vile kipaumbele cha umoja wa Watanzania akisema ni jambo lisilopaswa kugeuzwa la kawaida, kwani ni kubwa.

Mengine ni kupambana na umasikini, akisema bado ni changamoto kubwa na ameeleza jinsi Serikali yake itakavyokabiliana nayo katika kilimo, uvuvi na mifugo. “Ulipofafanua nikasema upele umepata mkunaji,” alisema Waziri Mkuu.

Jingine ni suala la ushiriki wa Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, akisema ni lazima serikali kwa muda wote itoe maelezo ya kina ya hatua kwa hatua ambayo yanafikiwa kwa wananchi ili azma hiyo itimie kwa kunufaisha Watanzania wote.

Bunge limeahirishwa hadi Februari 8, mwakani. Aidha, wabunge mbalimbali waliipongeza hotuba ya Rais Kikwete, huku Mbunge wa Kilosa, Mustafa Mkulo akisema ameweza kuelezea mafanikio yake na ahadi ya Tume ya Mipango kuanza kazi Januari kutaifanya Tanzania kuwa na dira ya kuleta maendeleo.

Naye Mbunge wa Lindi Mjini, Salum Barwany (CUF), amesema hotuba hiyo imekidhi kutokana na kuelezea kuwa demokrasia itaimarika na kutekeleza suala la amani kwa kudhibiti ujambazi na mauaji ya albino.

Mbunge wa Isimani, William Lukuvi (CCM), alisema imetoa mwelekeo mzuri hasa aliposisitiza serikali iondoe urasimu na watu wachape kazi ambapo alifafanua “hapo tutaondoa kero za msingi na kupata mafanikio.”

Kikwete ataka mawaziri wabanwe

RAIS Jakaya Kikwete amewataka wabunge wawabane mawaziri katika Serikali yake lakini wawasahihishe wakiteleza.

Rais Kikwete pia amewaeleza wabunge kuwa, wasiwe wachoyo wa kuwasifu mawaziri wakifanya vizuri.

Kikwete ameyasema hayo mjini Dodoma wakati akihutubia Bunge la 10 na kulifungua rasmi.

Amewaeleza wabunge kuwa hivi karibuni atateua mawaziri makini, waadilifu na wachapakazi hodari.

Kwa mujibu wa Kikwete, atakaowateua wataiongoza nchi yetu kwa umahiri mkubwa katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mipango ya Serikali.

Kikwete amesema, atateua watu watakaoondoa urasimu katika katika Serikali, watakuwa karibu na wananchi, na watashirikiana vizuri na wabunge bila kujali vyama vya siasa wanapotoka.

Rais Kikwete amewaomba wabunge wampe ushirikiano Waziri Mkuu kama walivyofanya katika Awamu ya Kwanza ya Serikali yake.

Kwa mujibu wa Kikwete, Serikali atakayoiunda itakuwa na vipaumbele 13 ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba, Tanzania inaendelea kuwa nchi yenye umoja na usalama, na kwamba, Muungano uendelee kudumu na kuimarika.

Ametaja kipaumbele kingine kuwa ni kuendeleza juhudi za kukuza uchumi na kupunguza umasikini kwa kuharakisha mapinduzi ya kilimo, ufugaji, uvuvi na viwanda.

Wabunge wameelezwa kuwa, kipaumbele kingine cha serikali itakayoundwa kitakuwa ni kuongeza jitihada za kuwawezesha kiuchumi wananchi wa makundi yote ili washiriki na kunufaika na uchumi unaokua.

Alisema, Serikali itaendelea kujenga na kuimarisha sekta binafsi nchini na kutengeneza mazingira mazuri ya ushirikiano na sekta ya umma sanjari na kuimarisha uwezo wa serikali kupanga mipango ya maendeleo na kusimamia utekelezaji wake bila kuingilia shughuli za sekta binafsi.

Rais Kikwete amelieleza Bunge kuwa, Serikali itatumia fursa ya kijiografia ya nchi yetu na kuifanya Tanzania kuwa lango kuu la biashara na usafiri kwa nchi za Afrika Mashariki na kati.

Bunge limeelezwa kuwa, Serikali pia itaongeza jitihada za kuhakikisha kuwa taifa letu linanufaika zaidi na maliasili zake zilizo juu na chini ya ardhi hivyo itahakikisha kwamba, kunakuwa na sera za uvunaji na matumizi ya rasilimali hizo.

Alisema, Serikali itaboresha ukusanyaji wa mapato ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa pamoja na kuimarisha nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma.

Kikwete alisema, miaka mitano iliyopita ilikuwa migumu sana kwa kazi ya kujenga uchumi na kupunguza umasikini nchini kwa kuwa uchumi ulipata misukosuko mikubwa ukiwemo ukame uliokausha mazao mashambani.

“Hivi sasa uchumi wetu umekuwa tulivu tena, kasi ya ukuaji ni nzuri, mfumuko wa bei umeshuka sana kutoka wastani wa asilimia 12.1 mwaka 2009 hadi kufikia asilimia 4.2 hivi sasa” alisema.

Thursday, November 18, 2010

Kikwete amuapisha Pinda

RAIS Jakaya Kikwete amemuapisha Mizengo Pinda (62) kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.

Rais Kikwete juzi alimteua Pinda kuwa Waziri Mkuu, Bunge likamthibitisha kwa kupiga kura.

Hii ni mara pili kwa Pinda kuapishwa kushika madaraka hayo, kwa mara ya kwanza aliapishwa Februari mwaka 2008 kuchukua nafasi ya Edward Lowassa.

Pinda ameapa kuwa mwaminifu kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wake wote.

Mbunge huyo wa Katavi, pia ameapa kuihifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwanasiasa huyo ameapa kuwa, atamshauri kwa hekima Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na hatatoa siri za Baraza la Mawaziri.

Katika kiapo hicho katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chamwino, Dodoma, Pinda ameapa kuutetea na kuulinda umoja wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Viongozi wote wakuu wa Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar wamehudhuria sherehe za kumuapisha Pinda akiwemo Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.

Wengine waliohudhuria ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Seif Ali Idd.

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, mawaziri wakuu wastaafu, John Malecela, Frederick Sumaye, na Edward Lowassa pia walikuwepo wakati Pinda anaapishwa.

Viongozi wengine wakuu waliohudhuria sherehe hizo ni Spika wa Bunge la Tanzania, Anne Makinda, Naibu Spika wa Bunge hilo, Job Ndugai, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, Jaji Mkuu, Augustino Ramadhani, na Mkuu wa Majeshi, Davis Mwamunyange.

Makatibu wakuu wa Wizara, wakuu wa mikoa, watendaj wakuu wa taasisi za umma na binafsi, mabalozi wa nchi mbalimbali, na viongozi wa vyama vya siasa pia walikuwepo kwenye sherehe hizo.

Tuesday, November 16, 2010

Dk Shein ateua Baraza la Mawaziri la Kitaifa

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ameunda Baraza jipya la Mawaziri lenye sura ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa, kwa kuwapa nafasi nyeti
baadhi ya vigogo wa juu wa Chama cha Wananchi (CUF).

Baraza hilo lenye wizara 16, pia limejumuisha baadhi ya manaibu waziri wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete iliyomaliza muda wake na mawaziri wa serikali iliyopita wa Serikali ya Dk.

Amani Abeid Karume, huku aliyekuwa Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha akiachwa.

Baadhi ya vigogo hao wa CUF walioteuliwa katika baraza hilo, yupo aliyekuwa mgombea mwenza wa urais wa Jamhuri ya Muungano katika Uchaguzi Mkuu uliopita, Juma Duni Haji
ambaye amepewa Wizara ya Afya.

Wengine wa CUF walioteuliwa katika baraza hilo ni pamoja na mwanamama Mwakilishi machachari wa CUF, Fatma Abdulhabib Fereji, ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais.

Wengine kutoka CUF na nafasi zao katika mabano ni Aboubakar Khamis Bakary, ambaye
alikuwa Kiongozi wa Upinzani katika Baraza la Wawakilishi (Waziri wa Katiba na Sheria), Hamad Masoud Hamad aliyekuwa Waziri kivuli wa Miundombinu (Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano).

Pia yumo Abdilahi Jihad Hassan ambaye ni mwakilishi mpya wa Magogoni (Waziri waAhmed Mazrui aliyeteuliwa dakika za mwisho na Rais Karume baada ya maridhiano (Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko).

Dk Shein pia amemteua Said Ali Mbarouk aliyekuwa Waziri Kivuli wa Fedha (Waziri wa Mifugo na Uvuvi), Haji Faki Shaali aliyekuwa Waziri kivuli Uratibu wa Shughuli za Baraza
la Wawakilishi (Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri asiyekuwa na Wizara Maalumu).

Wengine kutoka CUF ambao wameteuliwa kuwa manaibu waziri ni Zahra Ali Hamad (Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali), Bihindi Hamad Khamis ( Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo) na Haji Mwadini Makame (Naibu Waziri wa Ardhi, Makazi,
Maji na Nishati).

Mawaziri kutoka CCM ni pamoja na Dk. Mwinyihaji Makame (Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu), Omar Yussuf Mzee, aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi Serikali ya Muungano (Waziri Ofisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo).

Wengine ni Haji Omar Kheri ambaye alikuwa Waziri anayeshughulikia Uratibu wa Shughuli za Baraza la Wawakilishi (Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Mohammed Aboud Mohammed aliyekuwa Naibu Waziri wa Afrika Mashariki katika Serikali ya Muungano (Waziri Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais).

Wengine ni Ramadhan Abdulla Shaaban ambaye alikuwa Waziri wa Katiba na Utawala Bora (Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali), Zainab Omar Mohammed aliyekuwa Waziri asiye na Wizara Maalumu anayeshughulikia Pemba (Waziri wa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya
Wanawake na Watoto).

Mawaziri wengine kutoka CCM ni aliyekuwa Naibu Waziri Kiongozi, Ali Juma Shamhuna (Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji na Nishati), Mansoor Yussuf Himid aliyekuwa Waziri wa
Nishati, Ujenzi na Maji (Waziri wa Kilimo na Maliasili).

Pia yupo Haroun Ali Suleiman aliyekuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali (Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika), Suleiman Othman Nyanga, aliyekuwa Waziri wa Tawala za Mikoa (Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri asiyekuwa na Wizara
Maalumu) na Machano Othman Said, aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano ( Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum).

Katika unaibu waziri, Dk Shein amemteua Issa Haji Ussi (Naibu Waziri ya Miundombinu na Mawasiliano), mmoja wa wawakilishi wapya walioteuliwa na Rais, Dk. Sira Ubwa Mamboya ( Waziri wa Afya) na Thuwaiba Edington Kissasi (Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko).

Mbali na Nahodha, wengine walioachwa ni Samia Suluhu Hassan (Utalii, Biashara na Uwekezaji), Burhan Saadat Haji (Kilimo na Mifugo) na Asha Abdallah Juma (Kazi na
Maendeleo ya Wanawake na Watoto).

Wengine walioachwa ni Sultan Mohamed Mugheiry (Afya na Ustawi wa Jamii Taffana Kassim Mzee (Naibu Waziri wa Nishati, Aridhi na Maji) Shawana Buheit Hassan (Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii ).

Pia yumo Khamis Jabir Makame (Naibu Waziri Elimu na Vyuo vya Ufundi), Khatib Suleiman
(Naibu Waziri wa Kilimo na Mifugo) na Mahmoud Thabit Kombo (Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo).

Mawaziri wapya wataapishwa rasmi leo jioni katika viwanja vya Ikulu, Zanzibar.

Chadema waanza mchakato wa kudai tume huru ya uchaguzi.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesisitiza bado hakiyatambui matokeo yaliyotangazwa na tume ya Taifa ya uchaguzi na kumpa ushindi Rais Jakaya Kikwete ,lakini imefafanua kuwa hatua hiyo haina maana kwamba wabunge wake na madiwani hawatatekeleza wajibu wao.

Chama hicho kimesema kuwa kutokana na mfumo uliopo sasa kuendelea kupendelea chama tawala, tayari kimeanza mchakato wa kudai tume huru ya uchaguzi kupitia Bunge na mabadiliko ya katiba ili uwanja wa kisiasa uweze kutoa fursa sawa kwa wote.
Mwenyekiti wa Chama hicho Bwana Freeman Mbowe amewaambia waandishi wa habari Mjini Dodoma kuwa amesema kuwa ni muhimu sasa kuundwa kwa tume maalumu kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa uchaguzi uliopita ili hatimaye ibainishe kasoro zilizopo na kutoa majibu sahihi kwa nini wananchi wengi hawakujitokeza kupiga kura.

Kwa upande wake aliyekuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia CHADEMA Dokta Willbroad Slaa amesema yupo tayari kutaja majina ya maofisa wa usalama wa Taifa waliohusika katika kuvuruga zoezi la uchaguzi iwapo majina hayo yatahitajika kama ushahidi mahakamani maana kitendo kilichofanywa ni kosa la jinai.

Monday, November 15, 2010

UWT wamtabiria Pinda

WAKATI kesho Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kumteua Waziri Mkuu, Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), umeanza kumtabiria Waziri Mkuu aliyemaliza
wake, Mizengo Pinda, kuwa atateuliwa tena kushika wadhifa huo.

Hata hivyo, Pinda amewaambia kuwa anaogopa, kwani Rais Kikwete anaweza kusema wanampangia, hivyo akafuta uteuzi wake, lakini kama atarejeshwa, ameahidi kushirikiana naye.

Wanawake hao walieleza hisia zao wakati wa sherehe za kumpongeza Spika wa Bunge, Anne Makinda kwa kuchaguliwa kushika wadhifa huo, zilizofanyika jana mjini hapa.

Sherehe hizo ziliandaliwa na UWT Mkoa wa Dodoma pamoja na wabunge wanawake.
Mwanamke wa kwanza kutoa utabiri huo alikuwa Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma, Fatma Tofiq wakati akitoa risala yawanawake hao, kwa kumtaja Pinda kama Waziri Mkuu mtarajiwa.

Alipompa nafasi ya mke wa Pinda, Tunu Pinda kuwasalimia na kuzungumza na wanawake waliofika katika sherehe hizo, wakati akitoa utangulizi alisema, “Waziri Mkuu mstaafu si ndiyo (akacheka)… Waziri Mkuu mtarajiwa…hapo sawaaaaa (watu wakacheka) na Mbunge wa
Katavi… tumeanza vizuri kuwa na Spika mwanamke na natarajia miaka ijayo, Waziri Mkuu pia atakuwa mwanamke.”

Naye Mwenyekiti wa UWT Taifa, Sophia Simba wakati akitoa utambulisho, alimtaja Pinda kama Waziri Mkuu mtarajiwa akiamini rais atamteua tena.

Hata hivyo, Pinda alipopewa nafasi kusalimia hadhara hiyo, alisema “nimeogopa mlivyosema mimi Waziri Mkuu Mtarajiwa kwa sababu Mzee Kikwete anaweza kusikia akasema mnanipangia, sitaki sasa…kama nitakuwa bounceback (kurejea tena) nitashirikiana
naye”.

Naye Makinda alipopewa nafasi kama mgeni rasmi kutoa hotuba yake, alianza kwa kusema
“Mheshimiwa bounceback” na ndipo watu wakacheka.

Rais Kikwete kesho anatarajiwa kupeleka bungeni jina la mteule wake wa nafasi ya Waziri Mkuu ambalo litapigiwa kura na wabunge ili kuidhinishwa kushika wadhifa huo, kama Katiba inavyoelekeza.

Pinda aliyeingia madarakani Februari 2008, baada ya kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa kwanza
aliyeanza na Rais Kikwete katika Awamu ya Nne, Edward Lowassa, anatajwa kupewa nafasi ya kuendelea na wadhifa huo katika kipindi hiki cha pili na cha mwisho kikatiba kwa Rais Kikwete.

Uadilifu wake na uwezo mkubwa wa kusimamia shughuli za serikali zikiwamo za Bunge; kubana na kusimamia kikamilifu matumizi ya fedha za serikali na kutojihusisha na makundi ndani ya chama chake, ni mojawapo ya sifa zinazompa nafasi kubwa Pinda kuendelea na
kiti hicho katika kipindi chake cha mwisho cha miaka mitano kama mbunge baada ya kutangaza kutowania tena nafasi hiyo mwaka 2015.

Makinda: Sitabadilika, nitakufa mwadilifu

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda ambaye ushindi wake umekuwa gumzo na hasa baada ya kuenguliwa kwa mtangulizi wake, Samuel Sitta aliyekuwa amejitokeza kutetea kiti hicho, amesema kamwe watu wasitegemee kama atabadilika na kuacha uadilifu wake.

Mwanasiasa huyo mkongwe aliyewahi kuwa Waziri katika Serikali za awamu mbalimbali, amesema yeye ni mwadilifu wa kuzaliwa na hakuazima wala kukopa kwa mtu, hivyo ana uhakika atakufa na uadilifu wake.

Spika huyo aliyechaguliwa wiki iliyopita, alitoa maelezo hayo wakati alipowahutubia wabunge na wakazi wa mji wa Dodoma katika sherehe za kupongezwa zilizoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dodoma pamoja na wabunge wanawake.

“Uadilifu siazimi wala sikopi kwa mtu, nimezaliwa hivyo na nitakufa nao, baba yangu alikuwa mwadilifu na mwanasiasa na akafa vivyo hivyo,” alisema Makinda (61).

Alisema katika kupata nafasi hiyo, hajatumia hata senti moja wala kutoa kitu, bali ameupata
kutokana na kupigiwa kampeni na watu ambao hawajui, ila kwa utashi wao wenyewe kutokana na kuwa na imani naye.

“Hakuna aliyeniweka katika kiti hiki na nitafanya kazi bila upendeleo na naamini nitasaidiwa na Mungu na hata siku ya kupitishwa asubuhi nilikwenda kanisani kuomba Mungu anipe malaika wa kunisaidia,” alisema.

Tangu amepitishwa na kuchaguliwa kwa kishindo na wabunge, Makinda amekuwa akivumishiwa maneno mengi, ikiwemo kuwa alisaidiwa kupata uteuzi na kushinda kiti hicho na kundi hasimu na aliyekuwa Spika Sitta, jambo ambalo mwanamama huyo amelikanusha tangu aliposhinda kiti hicho.

Spika huyo wa kwanza mwanamke nchini tangu kupata Uhuru, aliweka wazi kuwa nafasi hiyo anaiweza na haendi kujifunza, bali kwenda kufanya vizuri zaidi na

kuzingatia ushauri wa wananchi katika kuliendesha Bunge ambalo litakuwa moja bila kujali itikadi ya vyama vya siasa. Aliahidi

kulifanya Bunge hilo kuwa moja na imara na wawakilishi wawe wa kweli kuwawakilisha wananchi na si mtu binafsi, huku akisema Bunge la sasa lipo wazi hivyo si rahisi mtu kulibadilisha zaidi ya kuwashauri wabunge kufahamu sheria na kanuni.

Alirejea kauli yake kuwa kama Sitta angepitishwa na Kamati Kuu ya CCM kutetea kiti chake, angeondoa jina lake na kuongeza “ingewezekanaje mimi na Sitta wote tuondoke kwenye Bunge, isingekuwa sahihi, kweli tuache watu kutoka nje?

Ndiyo maana mimi pia nilichukua fomu…maneno ya mitaani nayachukulia ni ya watu waliofilisika, mimi sina tatizo na Siita, ni kaka yangu tumefanya kazi pamoja.”

Naye Waziri Mkuu aliyemaliza muda wake, Mizengo Pinda alisema Makinda ana uwezo na anashaurika vizuri na kushauri wenzake vizuri, hivyo ana imani atawasaidia Watanzania.

Katika sherehe hizo, wanawake walimpa Makinda zawadi ya picha yenye mchoro wa mama aliyebeba mzigo wa kuni na mtoto mgongoni pamoja na seti ya mkufu wa dhahabu yenye lulu.

Friday, November 12, 2010

BREAKING NEWS: ANNE MAKINDA NDIYE SPIKA MPYA

MHESHIMIWA ANNE MAKINDA NDIYE SPIKA MPYA WA BUNGE BAADA YA KUMSHINDA MH. MGOMBEA MABERE NYAUCHO MARANDU KATIKA UCHAGUZI WA KUMPATA SPIKA MPYA WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA. MAMA MAKINDA KAPATA KURA 265 WAKATI MH. MARANDO KAPATA KURA 53

HIVI SASA SPIKA HUYO MPYA ANASIMAMIA ZOEZI LA KUAPA LA WABUNGE WAPYA WA BUNGE HILI LA 10. BUNGE LA TISA LILIMALIZA MUDA WAKE JULAI 16, 2010. ZOEZI LA KUAPA WABUNGE WAPYA LINATARAJIWA KUCHUKUA SIKU ZAIDI YA 2.

Ni Makinda Vs Marando

MGOMBEA wa uspika wa Bunge la Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Anne Makinda (61), amesema, akichaguliwa, Bunge litakuwa imara na lenye kasi kuliko lililopita.

Makinda amewaeleza waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa, ana uzoefu wa kuliongoza Bunge na ameiva kushika madaraka hayo.

Ametoa kauli hizo baada ya kushinda katika kura za wabunge wa CCM waliopendekezwa kugombea nafasi hiyo.

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM jana ilimteua Makinda, Anna Abdallah na Kate Kamba kuwania kuteuliwa kugombea uspika kwa tiketi ya CCM.

Mbunge huyo wa Njombe Kusini ameshinda kwa kupata kura 211, Kate kamba alipata kura 15, na Anna Abdallah alipata kura 14.

Makinda atachuana na mgombea wa Chadema anayewania uspika wa Bunge, Mabere Marando.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amesema, chama hicho kinaamini kuwa, mgombea wake atashinda.

Makinda amesema, amewahi kushika nyadhifa mbalimbali katika Bunge la Tanzania hadi kuwa Naibu Spika.

Amesema, wakati akiwa Naibu Spika wa Bunge alipata uzoefu wa kuliongoza Bunge kwa kutembelea mabunge mbalimbali duniani na kuona uendeshaji wake.

Makinda amesema, kambi ya upinzani isitegemee kuwa kutakuwa na mteremko katika utoaji wa maamuzi, yatatolewa kwa kufuata taratibu na kanuni za Bunge.

Amesema, wabunge wote wanapaswa kazifahamu kanuni za Bunge ili wasije kulalamika unapotolewa uamuzi kwa kufuata kanuni hizo.

Makinda amesema, wabunge hao wakizifahamu kanuni hizo mapema wataweza kuwa makini wanapochangia mijadala na pia kama kuna kanuni ambayo haifai kwa wakati huu basi wawaze kuibadili mapema.

Shein aahidi utawala bora

RAIS wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, amesema Serikali yake ya Awamu ya Saba ambayo ni ya Umoja wa Kitaifa, imejipanga kusimamia na kuhakikisha kuwa suala la amani, maadili, demokrasia na utawala bora linakuwa ajenda kuu ya kitaifa.

Pia amesema katika kuhakikisha kuwa matatizo ya wafanyakazi visiwani hapa yanapatiwa ufumbuzi hasa kimaslahi, Serikali hiyo inatarajia kuunda wizara mpya ya Utumishi wa Umma ambayo itakuwa na jukumu la kusimamia masuala yote ya wafanyakazi.

Aidha, ametoa shukrani kwa Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume na Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad, kwa maridhiano waliyofikia ambayo yameleta mabadiliko ya kisiasa visiwani na kuvipatia sifa duniani kote.

Akizindua Baraza la Wawakilishi jana mjini hapa, Dk. Shein alisema wakati umefika kwa Serikali hiyo mpya itakayojenga historia ya Zanzibar, kuonesha mfano kwa kusimamia maadili na utawala bora hasa katika kupiga vita rushwa, lakini pia kuwahudumia wananchi kwa misingi ya Katiba na Sheria.

“Maadili ndio itakuwa ajenda yetu ya kitaifa, tunapaswa kama viongozi kuwajibika kwa wananchi waliotuchagua, nawahakikishia kuwa tutapambana na rushwa kwa hali yoyote ile na nitashughulikia kuanzishwa kwa Sheria ya Rushwa, na kwa kuanzia, nitaziba mianya yote ya upoteaji ovyo wa mapato ya Serikali,” alisema Dk. Shein na kushangiliwa.

Alisema tangu mchakato wa uchaguzi uanze na kumalizika, Wazanzibari wameonesha hali ya amani, utulivu na kupendana na hivyo kutoa fursa kwa Serikali hii kutumia nafasi hiyo kama chachu ya kuwaletea maendeleo.

“Jamii imepata matumaini mapya, hali ambayo imetoa fursa sasa ya kuijenga nchi kiuchumi kwa pamoja,” alieleza.

Alisema atahakikisha anawaongoza wananchi wake kwa kufuata misingi ya Katiba ya Zanzibar, bila kujali itikadi zao na kipaumbele kikiwa ni kuwajengea maisha na uchumi bora ambao kwa mujibu wa dira ya Serikali hiyo, hadi mwaka 2015 uchumi utapanda na kufikia asilimia 10.

Aliwataka wananchi kudumisha jitihada za maridhiano kwa kusimamia umoja na mshikamano ili kuiwezesha Serikali itimize ahadi ilizotoa na kuwaletea maendeleo wanayotarajia ambapo pia alisisitiza juu ya umuhimu wa wananchi kushiriki maendeleo ya nchi yao.

Aliwaahidi wananchi hao kuwa Serikali yake itatekeleza kwa vitendo ahadi zote ilizotoa wakati wa kampeni ambazo ni kuimarisha sekta ya kilimo, viwanda, uvuvi na ufugaji, miundombinu kuanzia barabara, bandari na viwanja vya ndege, huduma za kijamii kama vile maji, elimu, afya na umeme na ajira, lengo likiwa ni kuwakwamua wananchi na umasikini.

Aliahidi kwa kushirikiana na Rais Jakaya Kikwete kusimamia na kutatua kero za Muungano ambapo Serikali yake itaanza kwa kuboresha Kamati ya Pamoja ya kutatua kero hizo.

Akitoa shukrani, Mwakilishi wa Kambi ya Upinzani, Abubakar Hamis Bakari, alisisitiza juu ya ushirikiano baina ya Wazanzibari bila kujali itikadi za vyama vyao, na kuahidi kuwa hotuba hiyo ya Rais itatumika kama moja ya zana za ujenzi wa Zanzibar mpya.

“Kuna mwanasiasa mmoja nchini Marekani alisema nyumba iliyogawanyika si imara, tudumishe umoja wetu,” alisema Bakari.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Maalim Seif na Jaji Mkuu Hamid Mahamoud waliokuwa katika msafara wa Rais.

Wageni waalikwa wengine ni Mama Mwanamwema Shein, wake wawili wa Spika wa Baraza hilo, Pandu Ameir Kificho, huku mke wake wa tatu akishindwa kufika kutokana na dharura pamoja na mabalozi wadogo waliopo nchini.

Wednesday, November 10, 2010

Vacancies (Nafasi za Kazi)

Tanzania Gender Networking Programme (TGNP) is a non governmental organisation which advocates for a transformed Tanzanian society where there is gender equality, equity and social justice. The overall objective is building a feminist social movement that is capable of engaging, challenging and claiming changes in policies, institutional structures and processes at all levels for social gender transformation and women’s empowerment. TGNP’s main strategies are policy analysis and research, training and capacity building, information, lobbying and advocacy, coalition building and networking. TGNP seeks to recruit suitable and qualified candidates for the vacant positions listed below. For all posts, we are looking for persons with:

a) Commitment to gender, women empowerment, social justice and human rights issues,

b) Commitment to team work and participatory approaches

c) Motivation with strong interpersonal relations. The advertised posts carry an attractive salary with fringe benefits.

TGNP is an equal opportunity employer and encourages applications from qualified women and men Tanzanian citizens.

1.0 Programme Officer - Monitoring and Evaluation

Responsibilities:

Oversees and facilitates the planning and formulation of programs/projects; proposals writing, fundraising and resource mobilisation, implementation, monitoring/ evaluation and reporting. Develops, improves and documents results based monitoring and evaluation systems, procedures, processes, tools within the organisation including strategic programme framework. Provides methodological and technical support to Monitoring and Evaluation activities for the organization including the coordination of advisory services.

Key Qualifications and experience:

Masters degree in Social Sciences, with specific focus on planning (programming) applied research methods and evaluation, including formal training in project management (M&E). Working experiences of at least 3 years of work in similar position. Exposure and experience to the management of consultancy activities and assignments.

Key Competencies:

•Excellent knowledge in planning including logical framework based planning and evaluation methodologies for projects/programmes.

•Capacity in designing/ development of programmes, projects and implementing monitoring and evaluation systems.

•Exposure and understanding of participatory methods in programming M&E

•Knowledge of statistics and database.

•Good communications and writing skills, public speaking and presentation ability;

•Knowledge of NGOs work and understanding of gender and development will be an added advantage

2.0 Programme Officer: Human Resource Management

Responsibilities: Determining human resource strategic and programmatic needs and priorities of the organisation. Oversee and provides leadership in the various human resource functions which include recruitment, staffing, training and development, performance monitoring and employee counselling.

The HR Officer detailed responsibilities will include:

◦Coordinating staff recruitment and selection processes and selection processes to ensure timely and comprehensive procedure in hiring staff

◦Monitor staff performance and ensure accountability

◦Developing skills and capacities of staff to enhance performance

◦Developing HR policies on working conditions, performance, management, and disciplinary procedures

◦Undertaking salary reviews and other remuneration issues including promotions and benefits

◦Administration of the payroll system, maintaining staff records, supporting line managers on all HR policies or other employment legislations

Key Qualifications and experience:

A bachelor’s degree in Human Resource, Business, or related discipline. A graduate degree is preferred. Working experiences of at least 3 years as senior HR officer or similar position.

Key Competencies:

◦Effective verbal listening and communication skills

◦Ability to prepare reports, proposals, policies and procedures

◦An understanding of relevant legislations, policies and procedures/labour laws

◦Effective PR skills and public speaking skills

◦Good communications and writing skills, public speaking and presentation ability;

◦Computer skills including ability to operate spreadsheet and word programmes at a
highly proficient level

◦Excellent organizational, time and stress management skills

◦Strong interpersonal skill, team work and communication skills

◦Knowledge of NGOs work and understanding of feminism/gender and development will be an added advantage

Personal attributes:

◦Maintain confidentiality, use sound judgement and perform independently

◦ Maintain standards of conduct and be respectful and demonstrate sound work ethics

◦Demonstrate sound work ethics

◦Be flexible while maintaining consistency and fairness

◦Prepared/ready to deal with emergencies/adhoc and activities/stressful situations at any time

3.0 Programme Officer: Library and Information Services

Key Responsibilities:

The Programme Officer Library and Information is expected to provide co-ordination, and technical expertise for the delivery of all information and knowledge management services including library and information services, database and cyber café, to TGNP programmes and other stakeholders of the organisation. Knowledge and skills in Feminist bookshop management and information technology are added advantages.
Qualifications

Minimum of a University degree in librarianship /information science/ Information Management, Information studies from a recognised institution. Competencies

•Competence in both manual and computerized library management systems database management systems, manual and computerised document/ record management systems, content management systems for website and other knowledge and information management packages for information centre.

•Programming skills and project management i.e. planning, implementation, monitoring and evaluations.

•Highly computer literacy with several knowledge and information management packages.

•Customer relations and communication skills

•Budgeting skill

•Gender awareness
Experience

•Minimum of three years working experience

•Specialised information service delivery with specialised users.

•Marketing and promotion in relation to library outreach dissemination

4.0 Programme Officer - Monitoring and Evaluation

Responsibilities:

Oversees and facilitates the planning and formulation of programs/projects; proposals writing, fundraising and resource mobilisation, implementation, monitoring/ evaluation and reporting. Develops, improves and documents results based monitoring and evaluation systems, procedures, processes, tools within the organisation including strategic programme framework. Provides methodological and technical support to Monitoring and Evaluation activities for the organization including the coordination of advisory services.

Key Qualifications and experience:-

Masters degree in Social Sciences, with specific focus on planning (programming) applied research methods and evaluation, including formal training in project management (M&E). Working experiences of at least 3 years of work in similar position. Exposure and experience to the management of consultancy activities and assignments.

Key Competencies:

◦Excellent knowledge in planning including logical framework based planning and evaluation methodologies for projects/programmes.

◦Capacity in designing/ development of programmes, projects and implementing monitoring and evaluation systems.

◦Exposure and understanding of participatory methods in programming M&E

◦Knowledge of statistics and database.

◦Good communications and writing skills, public speaking and presentation ability;

◦Knowledge of NGOs work and understanding of gender and development will be an added advantage

5.0 Programme Officer Records Management

Overall Purpose:

To provide day-to-day records and document management within the Organization ensuring there is systematic control, organization, access to and protection of the Organization’s information in whatever media: tape, disc, paper or film, from its creation through its use, to its permanent retention or legal destruction. Main

Duties and Responsibilities:

•Responsible for day-to-day records management issues in the TGNP;

•Responsible for controlling both quantity and quality of records created by the Organization;

•Responsible for ensuring that records are properly captured and classified;

•Responsible for ensuring that records are kept secure and neither destroyed prematurely nor kept too long;

•Conducting wise selection of records for either destruction or preservation in the archive;

•Ensuring continuity of business operations in case of disaster;

•Responsible for implementation of TGNP Document Management Policy & Standards;

•Responsible for implementation of TGNP Records Retention & Disposal Policy;

•Responsible for updating/amending the Document Management Policy & Standards and Records Retention & Disposal Policy;

•Responsible for coordinating records/documents capture in the electronic system and availing them to users in time;

•Responsible for records/documents back up in the electronic system on daily basis as a disaster recovery measure.
General Qualifications and Requirements

•Education: preferably Bachelors Degree in Library & Information Sciences. Alternatively, First Degree and Diploma in Library & Information Studies/Diploma in Archives & Records Management

•Experience: Minimum of three years’ in both manual and electronic Records & Archives Management
Competencies

•Excellent interpersonal and teamwork skills;

•Computer literate;

•Excellent knowledge of document management systems;

•Excellent knowledge in library management and administration;

•Good knowledge of statutory record keeping and compliance requirements;

•Good communication skills (written and oral, including listening skills);

•Excellent analytical skills.

6.0 Personal assistant to the ED Responsibilities:

The Personal Assistant to the Executive Director will have overall responsibilities Providing management and administrative support to the ED. This position requires an excellent all rounder who has knowledge and skills to handle a diverse work load. The position requires supporting the ED by proactively creation and maintaining systems to keep the ED organised and effective.

The key responsibilities will include:

•Manage the calendar of the ED on issue of invitations, booking meetings, and make priorities

•Filter ED’s incoming calls, e mails, paper mail and visitors

•Prepare official correspondences i.e. thank yous, invitations

•Act as administrative contact for Directors of the Board, TGNP Members, donors and other key partners

•Manage ED’s travel and meetings including sending notice of the meeting, material and minute taking,

•Preparing press statements for the ED

•Book travel for ED including preparation of itineraries, post trip follow-up including retirement of impress as well as short reports on the trips.

Key Qualifications and Experience:-

Holders of BA Social Sciences with relevant working experience of not less that three years. Key Competencies:

•Positive attitude and excellent customer service skills

•Highly organised with outstanding time management capabilities

•Highly motivated with ability to work under pressure

•Team player with excellent word processing and communication skills

•Highly developed written and verbal communication skills

•High standard social marketing skills (Public Relations skills),

•Highly developed written and verbal communication skills including strong spelling,grammar and communications skills

•Highly developed knowledge in using Microsoft office soft ware (world processing, excel and power point)

•A can do positive attitude

7.0 Programme Officer - Capacity Building and Marketing.

Responsibilities:

Overall responsible for the designing, planning, implementation and monitoring of training programme activities, outputs and impacts. Responsible for the coordination and delivery of quality gender training products and services, monitoring and impact evaluating. Develops and updates training manuals and materials, tools and methodologies for enhancing feminist, animation gender capacities of development actors at different levels within and outside the country. Responsible for identifying, developing, strengthening, expanding of the base of resource persons / trainers and facilitators. Responsible for the strengthening and developing linkages with clients, peer Gender Training Institutions and other strategic actors/institutions for the promotion of GTI activities.

Key Qualifications and experience:-

Minimum of a Masters Degree in social sciences or equivalent plus course work in training and management of training institutions


◦ Training and facilitation experiences for minimum 2-3 years

◦ Experiences in working in training institutions, training processes and curriculum development.

◦ Course work on gender or women’s studies

◦ Relevant experience of 3-5 years of working with gender and development issues.

◦ inter-personal relationships and marketing management

◦ MS word, power point, excel and e-mail and internet
Key Competencies ◦Capacity in training institutions management.

◦Capacity in curriculum development, training& manual materials development

◦Gender analysis and training.

◦Good writing, public speaking and presentational skills·

◦Coaching/mentoring ability

◦Communication, spoken and written in Kiswahili and English.

◦Computer literacy in word, power point, excel and e-mail and internet

8.0 Systems Administrator

Overall purpose: Providing systems support for a large scale and high performance computing including installation and management of computer systems, workstations, operating systems, peripheral and system interface.

Position Summary:

•Design, develop, program and manage websites, databases, servers and other computing and IT systems for the Organization.

•Formulate policies, establish priorities independently resolve routine and non-routine technical matters; provide technical analysis, user support and oversee repairs/upgrades for the full range of organization ICT needs;

•Manage administrative and technical functions to ensure a complete, up-to-date and smoothly functioning IT infrastructure. Provide direct IT support for events and other special requirements.

Key Tasks: ·

◦Investigate user problems, identify their source, determine possible solutions, test and implement solutions.·

◦Design, develop, program and manage websites, databases, servers and other computing and IT systems for the Organization.

◦Analyzing system logs and identifying potential issues with computer systems·

.Performing routine audits of systems and software’s.

◦Supervise daily Management Information System (MIS) operations·

◦Introducing and integrating new technologies into existing databases environment.·

.Maintain registry of ICT equipment·

◦Institute security measures for computers and other ICT hardware as per ICT policy and guidelines·

◦Create a backup and recovery policy·

◦Answering technical queries·

◦Prepare ICT reports
Qualification:

1.
◦Bachelors Degree in computer Science or Information Technology from a recognized Institution.
◦Required Knowledge, Skills, and Abilities
PC network and systems administration.
◦HTML+CSS or more of the following programming skills- PHP, SQL, JavaScript/AJAX.
◦Ability to communicate policies and procedures to a diverse population at all levels. Demonstrated knowledge and understanding of information technology applications in complex networked/on-line system environments.
◦Ability to make decisions independently and without direct supervision.
◦Ability to work cooperatively as a member of an interdisciplinary team, communicate effectively and persuasively to senior IT and administrative management, and represent the Organization in internal and external interactions.
◦Excellent organizational, interpersonal and problem-solving skills.
All applications supported by CV, a statement of not more than three pages on your experience related to the job you are seeking, and why you want to work in this position; two writing samples of up to five pages each; two reference letters and supporting documents to be submitted within three weeks from date of first appearance this advertisement. The organisation is an equal opportunity employer. Women and youth are highly encouraged to apply. Applications should be addressed to:

The Executive Director,
Tanzania Gender Networking Programme (TGNP),
P.O. Box 8921,Dar es Salaam,Tanzania.
E Mail: info@tgnp.orgThis e-mail address is being protected from spambots, you need JavaScript enabled to view it
Website: http://www.tgnp.org/
Note: Only short listed applicants will be contacted.

Uongozi wa juu Zanzibar wakamilika

SAFU ya uongozi wa juu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar imekamilika baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein, kuteua makamu wake wawili, Maalim Seif Shariff Hamad na Balozi Seif Ali Iddi.

Kwa mujibu wa marekebisho ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, yaliyozaa Serikali ya Umoja wa Kitaifa baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kutakuwa na makamu wa rais wawili; wa kwanza akitoka chama kilichoshika nafasi ya pili na wa pili akitoka chama kilichotoa rais.

“Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 39 (1),(2) na (3) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein, leo amemteua Seif Sharif Hamad kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais,” ilieleza taarifa ya Ikulu Zanzibar jana na kuongeza:

“Wakati huo huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 39(1),(2) na (6) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein amemteua Balozi Seif Ali Iddi kuwa Makamu wa Pili wa Rais.”

Taarifa hiyo ya Ikulu ilisema uteuzi huo ulianza jana na wawili hao walitarajiwa kuapishwa jana hiyo hiyo.

Kwa mujibu wa kifungu cha 39 (1), (2) na (3) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ndani ya siku saba baada ya kushika madaraka, Rais atateua Makamu wa Kwanza wa Rais na Makamu wa Pili wa Rais.

Kwa mujibu wa Ibara ya 3 ya kifungu hicho, Makamu wa Kwanza wa Rais atatakiwa awe na sifa za kumwezesha kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na atateuliwa na Rais baada ya kushauriana na chama kilichoshika nafasi ya pili katika matokeo ya uchaguzi wa rais.

Ibara hiyo pia inaeleza kuwa iwapo chama kilichotokea nafasi ya pili katika matokeo ya kura ya uchaguzi wa rais kimepata chini ya asilimia tano ya kura zote za uchaguzi huo; au endapo rais atakuwa hana mpinzani katika uchaguzi, basi nafasi ya makamu wa kwanza itakwenda kwa chama chochote cha upinzani kilichoshika nafasi ya pili kwa wingi wa viti vya majimbo katika Baraza la Wawakilishi.

Ibara ya nne inaeleza kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais hatakuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi; Ibara ya 5, inaeleza kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais atakuwa mshauri wa Rais katika kutekeleza kazi zake na atafanya zote atakazopangiwa na Rais.

Kwa mujibu wa Ibara ya 6 ya kifungu hicho cha 39, Makamu wa Pili wa Rais atateuliwa kutoka miongoni mwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka chama anachotoka Rais; na
Ibara ya 7, inaeleza kuwa Makamu wa Pili wa Rais atakuwa ndiye Mshauri Mkuu wa Rais katika kutekeleza kazi zake na pia atakuwa kiongozi wa shughuli za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika Baraza la Wawakilishi.

Balozi Iddi ni mwanasiasa mwenye kufuata siasa za mrengo wa wastani na amekuwa na uzoefu wa muda mrefu katika siasa, aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania katika nchi mbalimbali; Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar na kabla ya uchaguzi, alikuwa Naibu Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hamad ambaye ni maarufu kama Maalim Seif, aliwahi kuwa Waziri wa Elimu, Waziri Kiongozi wa SMZ na kwa sasa ni Katibu Mkuu wa CUF.

Alikuwa mgombea urais wa chama hicho katika uchaguzi wa mwaka huu na alishika nafasi ya
pili nyuma ya Dk. Shein.

Kulingana na Katiba ya sasa ya Zanzibar, CUF iliyoshika nafasi ya pili katika uchaguzi huo ilipaswa kupendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, wakati CCM ikitakiwa kutaja jina la Makamu wa Pili wa Rais.

Chini ya makubaliano hayo ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa, nafasi za mawaziri zitagawanywa sawa, miongoni mwa vyama hivyo, vikuu vya kisiasa Zanzibar.

Wakati huo huo, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho amechaguliwa tena kwa kura nyingi kuendelea na wadhifa huo ikiwa ni Baraza la Kwanza la Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Kificho alipita kwa kura 45 kutoka kwa wawakilishi 78 waliopiga kura, dhidi ya mshindani wake Abbasi Juma Mhunzi wa CUF ambaye alipata kura 32.

Katika uchaguzi huo, kura moja iliharibika ambapo mshindi alitangazwa kwa kupata kura nyingi.

Hii ni mara ya nne kwa Kificho ambaye ni kada maarufu wa CCM, kushika wadhifa huo na alikuwa mwanachama pekee kupitia chama hicho aliyekuwa akiwania nafasi hiyo.

Baada ya kula kiapo cha utii, Spika Kificho aliwaapisha wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakiwamo wanane walioteuliwa na Rais Dk. Ali Mohammed Shein juzi.

Shibuda aitahadharisha CCM kuhusu Uspika

AKIONEKANA kuguswa na mambo yanavyokwenda ndani ya CCM kuhusu upatikanaji wa mgombea uspika wa Bunge la Muungano, Mbunge mteule wa Maswa, kupitia Chadema John Shibuda amekihadharisha chama hicho tawala.

Amewataka wana CCM kufanya uamuzi wa busara juu ya kumpitisha mgombea uspika, vinginevyo watakisambaratisha chama hicho.

Alisema hayo jana wakati akizungumza na gazeti hili muda mfupi baada ya kufika kwenye viwanja vya Bunge kujisajili, ikiwa ni mojawapo ya ratiba za wabunge wote wateule.

Shibuda alisema kuna kila sababu ya wana CCM kuwa makini katika kumpitisha mgombea uspika vinginevyo watakuwa wanatengeneza mwanya wa kukisambaratisha chama hicho.

Alisema inasikitisha kuona kuwa nafasi hiyo inagombewa na watu wasio na misingi ya uongozi na wanaonesha wazi uchu wa kiti hicho huku wakiwa na mawazo ya kulipiza kisasi.

Hata hivyo hakuwataja. Aidha, alimtaka Rais Jakaya Kikwete, kuhakikisha analisimamia vyema jambo hilo kwa umakini mkubwa na kudai kuwa iwapo chama tawala kitashindwa kuteua jina la mgombea makini ambaye anaweza kuongoza Bunge ni wazi kiti hicho kitachukuliwa na vyama vya upinzani.

Shibuda alisema kinachosumbua zaidi katika CCM ni makundi ambayo yamekuwa yakiibuka pindi inapoonekana kuwa yanatetea masilahi ya wengi.

Alisema Rais Kikwete anajitahidi kuongoza chama chake vizuri lakini kinachosumbua ni baadhi ya watendaji wake ambao hawataki kufanya mambo katika misingi ya ukweli na uwazi.

Alisema kutokana na tatizo hilo, ni wazi kuwa chama tawala kisipokuwa makini kijue wazi ushindi wa kishindo utaelekea katika vyama vya upinzani hususani Chadema na wasijisumbue kuendesha kampeni kwa lengo la kusaka urais.

Kwa sasa katika mji wa Dodoma wabunge wanaonekana kukaa vikundi huku wakijadili ni nani atateuliwa na CCM kugombea nafasi hiyo nyeti ya uspika.

Pamoja na kampeni kuwa kali zaidi kati ya vigogo wawili ambao ni spika wa aliyemaliza muda wake, Samuel Sitta na Mbunge mteule wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, bado Watanzania wengi wakiwamo wabunge wa vyama mbalimbali wanasubiri kuona hatimaye
moshi mweupe utamfukia nani.

Hadi jana wabunge mbalimbali waliochaguliwa katika uchaguzi mwaka huu walikuwa wakiendelea kujisajili, huku Kamati Kuu ya CCM, leo ikitarajiwa kutangaza mgombea wake wa uspika.

Tuesday, November 9, 2010

Zitto na Mbowe kinyang'anyiro bungeni

TOFAUTI ambazo zimekuwapo kati ya viongozi wawili wa ngazi za juu wa Chadema, Freeman Mbowe na Naibu Katibu Mkuu wake, Kabwe Zitto, sasa zinahamia bungeni baada ya Zitto kutangaza nia ya kuwania nafasi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni.

Nafasi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni inashikwa na chama chenye wabunge wengi miongoni mwa vyama vya upinzani bungeni, na kwa mujibu wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Chadema ina viti vya majimbo 22 na CUF viti 23.

Hata hivyo, Chadema itaweza kuwa na viti vingi zaidi bungeni kwa sababu ya kura zake nyingi ilizopata katika ushindi huo majimboni kulinganisha na CUF.

Kura za wabunge za majimbo kwa kila chama ni mojawapo ya vigezo vya uteuzi wa kupata idadi ya wabunge wa Viti Maalumu.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ametangaza nia yake ya kuwania nafasi hiyo na anachosubiri ni utaratibu wa chama hicho wa namna ya kumpata kiongozi huyo.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Kabwe alisema ameshatangaza nia yake ya kuwania nafasi hiyo kupitia mtandao wa Facebook na anachosubiri ni utaratibu rasmi wa chama chake.

“Chama hakijaweka utaratibu wa namna kiongozi wa upinzani bungeni anapatikana. Utaratibu ukishawekwa nitatoa taarifa rasmi ila kwa sasa pitia Facebook yangu utaona ujumbe wangu,” alisema.

Katika mtandao huo, Zitto aliandika “nimewajulisha viongozi wangu wa chama Taifa kuwa nina nia ya kugombea nafasi ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni.

Mara baada ya taratibu za chama kuhusu nafasi hii kuwa wazi nitawajulisha.” Gazeti hili liliwasiliana na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Mbowe kuhusu maandalizi ya utaratibu wa kumpata kiongozi huyo wa wapinzani bungeni na kama na yeye, ana nia ya kuwania nafasi hiyo, lakini alijibu kwa kifupi kuwa chama hicho kinaamua mambo yake kupitia vikao na kukata simu.

Ingawa si rasmi na haimo katika kanuni za Bunge, kwa kuwa Mbowe ambaye ni Mbunge Mteule wa Hai atakuwa ndani ya Bunge, kwa wadhifa wake wa uenyekiti wa Taifa wa Chadema, ingetarajiwa ndiye apitishwe kuwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni; hali inayoonesha Zitto anaipinga kwa kutangaza nia yake.

Kwa muda sasa, Mbowe amekuwa na tofauti na Zitto katika masuala kadhaa ya uendeshaji wa chama hicho, huku Mbunge huyo kijana akijitokeza hadharani kuweka misimamo yake anapoamini chama kwenda kinyume, na wakati mwingine misimamo hiyo imemletea matatizo na viongozi wengine.

Aliwahi kujitokeza kuwania uenyekiti wa Taifa wa chama hicho mwaka jana, lakini akazuiwa na Baraza la Wazee, kabla ya kujitoa kumkabili Mbowe baada ya wazee kumsihi asifanye hivyo.

Pia alikuwa na msimamo mkali katika uchaguzi wa Baraza la Vijana na Baraza la Wanawake la Chadema baada ya kuhisi mchezo mchafu unataka utendeka, na kuonesha kuwa kulikuwa na rafu, uchaguzi huo ulisimamishwa kiasi cha kuathiri hata uteuzi wa wabunge wa viti maalumu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, aliyekuwa Kiongozi wa Upinzani katika Bunge lililopita kupitia CUF, Hamad Rashid Mohammed, ambaye alikuwa Mbunge wa Wawi, alisema kwa mujibu wa kanuni za Bunge, chama kinachotoa kiongozi wa upinzani ni chenye
wabunge wengi bungeni.

Alisema katika uchaguzi wa mwaka 2005, CUF ilikuwa na wabunge wengi bungeni ndiyo maana aliwania nafasi hiyo na kushinda ambapo kwa sasa atalazimika kuachia ngazi kwa Chadema.

Katika Bunge lililopita, CUF ilikuwa na wabunge 33 na Chadema 11.

Kutoka Dodoma, Jasmin Shamwepu, anaripoti kwamba viongozi wa Chadema wameandaa mapokezi makubwa ya waliowaita majemadari wa chama hicho walioibuka kidedea katika ubunge.

Akizungumza na HABARILEO jana, Katibu wa Mkoa wa Chama hicho, Stephen Masawe, alisema uongozi umeandaa mapokezi makubwa ya wabunge walioshinda katika majimbo kwa madai kuwa ni wakombozi wa wananchi.

Alisema mapokezi hayo yataanzia katika njia panda ya Nzuguni hadi kwenye ofisi za Chadema mkoa, ambako viongozi hao watapata fursa ya kusalimiana na wananchi wa Mkoa wa Dodoma.

Masawe alidai kuwa uongozi ulikuwa umeandaa maandamano makubwa lakini kutokana na
ugeni uliopo mkoani hapo hawakupewa kibali cha maandamano baada ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa kudai kuwa askari hawatoshi.

Hata hivyo alisema watakachokifanya ni kukodi basi dogo ambalo litapambwa bendera za chama, shamra shamra hadi ofisi ya mkoa.

Alisema pongezi hizo zitaambatana na utambulisho wa wanachama wapya wa chama hicho. Pia alidai kutakuwa na tendo la kutangaza madiwani wa kata tatu za manispaa ambao wameshinda kata walizogombea.

Nikiwa Spika Nitatibu Majeraha Ya Waliojeruhiwa- Chenge



Mbunge mteule wa jimbo la Bariadi Mashariki, ambaye pia aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikari Andrew Chenge amesema kuwa ameamua kuwania nafasi ya Uspika wa bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ili aweze kutibu majeraha yaliyosababishwa na uongozi uliopita. Chenge aliyasema hayo hivi karibuni wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Protea Courtyard Upanga jijini Dar es Salaam.

Monday, November 8, 2010

BREAKING NYUUUUUZZZZ: TAKUKURU YATOA TAMKO JUU YA CHENGE


Bosi wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA

Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.

TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010
S. L.P. 4865,
Dares Salaam.



Simu: 2150043-6/2150360
Nukushi: (022) 2150047
Baruapepe:dgeneral@pccb.go.tz
Mtandao www.pccb.go.tz

ESRF yamtaka JK kuzingatia utawala bora

TAASISI ya Utafiti wa Masuala ya Kijamii na Kiuchumi (ESRF), imepongeza ushindi wa Rais Jakaya Kikwete na kuishauri serikali yake kutilia mkazo suala zima la utawala bora kwa kuwa ni eneo ambalo linalalamikiwa zaidi na wananchi.

Akizungumza na gazeti hili juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Bohela Lunogelo alisema wananchi kwa sasa wanahitaji kuona mabadiliko katika mfumo wa utawala bora zaidi, ili kuona kama maisha bora kwa kila Mtanzania yanapatikana.

Akitoa mfano, Dk Lunogelo alisema wananchi wanahitaji kupatiwa huduma bora zinazowajali wateja wanaohitaji huduma hizo, ili kuondoa malalamiko.

Alisema kama hakuna utawala bora ina maana mteja hawezi kuridhika na huduma inayotolewa na hivyo kuishia kulalamika.

Kwa mujibu wa Dk. Lunogelo, kwa sasa utafiti unaonesha kuwa wananchi wanahitaji zaidi majengo ya shule, zahanati na miundombinu kwa kuwa serikali ilifanya vizuri maeneo hayo kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Alisema kwa sasa wanahitaji serikali ijayo iwekeze zaidi nguvu zake kwenye utawala bora na usimamizi wa maliasili za serikali.

"Kama hakuna utawala bora, ni dhahiri kuwa kutakuwepo na ucheleweshwaji wa maendeleo kwa wananchi.

Mmahospitalini wananchi wanahitaji huduma bora na dawa ziwepo, na pia kwenye mashule walimu wawepo wa kutosha na walipwe mishahara kwa wakati na wapatiwe makazi bora, haya yanaangukia kwenye utawala bora," alisema

Alisema wananchi pia wanahitaji kufahamu mapato yatokanayo na rasilimali za serikali kama vile madini na mazao ya ardhi na misitu ili watambue yanasaidia vipi kuboresha huduma za kijamii nchini kwa kuwa ni maeneo ambayo yanazusha malalamiko kwa wananchi.

"Wananchi kwa sasa wamebadilika, siyo kama ilivyokuwa zamani, wakiona kuna dalili za rushwa au usimamizi mbovu wa rasimali za serikali wanahoji kwa nini hali hiyo inatokea, utawala bora usiishe maofisini tu bali ufanyike kwa vitendo na utiliwe mkazo,"alisema.

Dk Lunogelo serikali ijyao pia inapaswa kuhakikisha inaboresha mfumo mzima wa kuchagua vijana wanaojiunga na kozi mbalimbali vyuo vikuu kwa kuwa malalamiko yamekuwapo kuwa
ukosefu wa utawala bora umechangia kwa wao kukosa nafasi.

Chenge amshambulia Sitta

MGOMBEA wa uspika wa Bunge, Andrew Chenge, amemshambulia Spika anayemaliza muda wake, Samuel Sitta kuwa ni mtu hatari aliyemwaga sumu kubwa kwa wananchi dhidi ya viongozi wa serikali katika miaka mitano ya uongozi wake bungeni.

Sumu hiyo kwa mujibu wa mgombea huyo, imesababisha majeraha kwa taifa, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi na pia imezaa majeruhi wengi akiwamo yeye binafsi.

“Mimi kama walivyo wengine wengi, ni miongoni mwa majeruhi wa uongozi wa namna hiyo (wa Sitta). Kama Bunge, hatuna budi kukabiliana nalo kwa nguvu kubwa,” alisema Chenge katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari aliouitisha Dar es Salaam jana.

Moja ya majeraha hayo kwa CCM kwa mujibu wa Chenge, ni matokeo ya uchaguzi uliomalizika wiki iliyopita.

“Matokeo yake (ya uongozi wa Sitta), ni wananchi ambao siku zote wamekuwa na imani kubwa na viongozi wao, wamelishwa sumu mbaya na hilo limechochea chuki, hasira na kutoaminiana miongoni mwa jamii.”

Chenge, aliyejiita mwarobaini wa majeraha hayo na kuweka wazi kuwa Sitta ‘anatakiwa kuondolewa kwa nguvu kubwa’, mbali na kumshutumu Spika huyo ambaye ameshatangaza nia ya kutetea kiti hicho, pia alielezea uzoefu wake katika uongozi aliosema unatosha kumpa sifa ya kuwa Spika.

“Nimechukua fomu ya kugombea kiti cha uspika nikiamini kwamba, ninao uwezo wa kutibu majeraha makubwa yaliyoliumiza Bunge na Taifa, wananchi na chama changu (CCM),” alisema.

Kwa mujibu wa Chenge, majeraha hayo yamesababishwa na “kiongozi aliye tayari kujitafutia na kujitwalia umaarufu au ushujaa wake binafsi kwa njia ya kuwahujumu, kuwaumiza na kuwachafua wengine kwa kutengeneza tuhuma na kashfa za kila aina.

“Bunge limekuwa na changamoto kubwa katika miaka mitano iliyopita. Viongozi ambao wajibu wetu wa msingi ni kuonesha njia, badala yake tumekuwa vinara wa uzushi, uongo, fitina na majungu,” alisema Chenge.

Tiba ya uongozi wa aina hiyo kwa mujibu wa mgombea huyo, ni kuchagua kiongozi bora wa Bunge na njia bora ni kupata kiongozi mbadala mwenye uwezo na nia njema.

Sitta alipotafutwa kwa njia ya simu, ilipokelewa na mtu mmoja aliyejitambulisha kuwa ni mlinzi wake na kusema kuwa anafahamu kinachotafutwa ni kuhusu Chenge lakini Sitta hatajiingiza katika malumbano hayo.

“Mzee hatuwezi kumruhusu ajibu, tumemzuia asijibu, hawezi kuingia katika malumbano,” alisema mlinzi huyo na kuendelea, “watu wanaona, subirini wakati wa kampeni.”

Chenge alisema Sitta aliendesha mijadala kwa kuwafanya wabunge wa chama tawala na wa Kambi ya Upinzani upande mmoja na serikali upande mwingine.

“Mimi nikiwa spika siwezi kuruhusu kitu kama hicho.” Alifafanua kwamba demokrasia ya kibunge, inataka wabunge wa chama tawala na serikali wawe upande mmoja na kambi ya upinzani upande mwingine na kusisitiza kuwa, pamoja na kuwa majeruhi wa uongozi wa Sitta, hatalipiza kisasi katika uongozi wake.

Kwa mujibu wa Chenge, wabunge wa chama tawala wanaruhusiwa kuzungumza lolote kuhusu utendaji wa serikali katika kamati yao ya chama na wakiingia bungeni, wanapaswa kuikosoa Serikali kwa lengo la kuboresha utendaji wake kwa staha.

Kuhusu kambi ya upinzani, alisema yenyewe ndiyo inayopaswa kuikosoa serikali ikibidi iiondoe madarakani kwa kuwa hilo ndilo lengo lao kuu.

Mbali na kuwageuza wabunge wa chama tawala na kambi ya upinzani dhidi ya serikali, Chenge alisema pia Sitta hakutekeleza wajibu wake kama mwamuzi (referee) kwa kuzingatia sheria na kanuni, badala yake aligeuka shabiki na aligeuza Bunge sehemu ya kutoa maoni yake binafsi.

Alipoulizwa kama ametumwa kugombea uspika, Chenge alihoji mbona alipokwenda kugombea ubunge Bariadi Mashariki, hakuna mtu aliyehoji nani aliyemtuma?

Alisisitiza kuwa uzoefu wake kama Mwanasheria Mkuu wakati wa uongozi wa awamu ya pili na ya tatu ndio kilichomsukuma.

Waandishi walipotaka awataje majeruhi wengine na kuhoji kama ni mkakati wake na wa majeruhi hao wa kuingia katika siasa za kusaka uongozi kwa mwaka 2015, Chenge alisema kila mtu aliyekuwa akifuatilia mambo ya Bunge, anafahamu majeraha na majeruhi wengine. Hata hivyo hakutaka kufafanua kuhusu kampeni za 2015.

Alipoulizwa kama aliwahi kufanya jitihada zozote kunusuru hali hiyo akiwa kama Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya chama hicho, alisema chama chake kimefanya kazi kubwa katika hilo, ikiwemo kuundwa kwa Kamati ya Mzee Mwinyi.