Tuesday, November 9, 2010

Nikiwa Spika Nitatibu Majeraha Ya Waliojeruhiwa- Chenge



Mbunge mteule wa jimbo la Bariadi Mashariki, ambaye pia aliwahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikari Andrew Chenge amesema kuwa ameamua kuwania nafasi ya Uspika wa bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ili aweze kutibu majeraha yaliyosababishwa na uongozi uliopita. Chenge aliyasema hayo hivi karibuni wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Protea Courtyard Upanga jijini Dar es Salaam.

No comments: