Friday, July 22, 2011

SHAIRI LA BAJETI

Na Bi. Subira Kibiga
TGNP

Karibuni karibuni, tuijadili Bajeti
Hotuba imewasili,bungeni kuisapoti
Tuisome kwa makini, hoja tuzijengeni
Bajeti imsbani, aliyekufa ni nani?

Bajeti imsibani, aliyekufa ni nani
Kila siku matangani marehemu hatoki ndani,
Vijana wako sandani,wazee makaburini
Bajeti imsibani,aliyekufa ni nani?

Bajeti inamlenga nani,umaskini ndio ilani
Takwimu ulipata wapi,hata usome bungeni
Sisi twakushangaeni,wananchi hali ya chini,
Bajeti imsibani, aliyekufa ni nani?

Ajira ndio msingi, bajetini hatuoni
Nimeongeza vitini,vya vikoba mitaani
Na mikopo ya mitaani,ufilisi majumbani
Bajeti imsibani aliyekufa ni nani?

Hamkuweza kuthamini,makundi ya pembezoni
Mkulima habadiliki, kila siku wa zamani
Jembe lake mkononi,trekta aweze nani
Bajeti imsibani aliye kufa ni nani?

Elimu ni mtihani, kwa asilimia Fulani
Watoto wa mashakani, mazingira hayafanani
Wajisomea njiani, usafiri awape nani
Bajeti imsibani, aliyekufa ni nani?

Hotuba tuisomeni, kisha tuichambueni
Inaleta tija gani, kwa makundi pembezoni
Kijana wa kijiweni,au mzee wa maskani
Bajeti imsibani aliyekufa ni nani?

Bajeti ni muhimili, kwetu sisi maishani
Mipango si matumizi,ndio iliyoko bungeni
Hotuba tuisomeni, pesa hazionekani
Bajeti imsibani aliyekufa ni nani?

No comments: