Tuesday, August 25, 2009

Mh. Spika Samwel Sitta alikula kiapo


Mh. Samwel Sitta akila kiapo kuwa Spika
Kama tulivyoanza wiki iliyopita,wiki hii tena tunagusa kwenye anga za siasa. Kama umekuwa ukifuatilia kwa makini yaliyojiri wiki hii, kubwa zaidi lilikuwa suala la Mheshimiwa Spika,Samuel Sitta, kukingiwa kifua na wapinzani kutokana na kile ambacho CCM(chama chake Sitta) wamekiona kama “kuwageuka” baada ya kuruhusu masuala ya mijadala ya ufisadi iendelee bungeni.

Walimtishia kumpokonya kabisa uanachama kama asiposikiliza.
Kinadharia wanachosema CCM ni kwamba ukiwa mwanachama au mbunge kupitia CCM,basi sio haki kunyooshea vidole mambo “mbofu mbofu” yanayoweza kuwa yanaendelea ndani ya CCM. Wanadai kama kuna kutofautiana,basi mambo hayo yamalizwe katika vikao vya chama na sio mahali pa wazi kama vile bungeni.

Wao CCM wanasema ni haki yao kumhoji au kumkemea Spika kwani yeye ni mwanachama wa CCM kama walivyo wengine. Anayesema hivyo ni Katibu Mkuu wa CCM,Yusuph Makamba. Kisha anasema bunge ni mali ya chama tawala cha CCM!

Je unadhani nini kinaendelea ndani ya CCM? Spika Samuel Sitta yupo sahihi? Makamba yupo Sahihi?

No comments: