Friday, August 14, 2009

Makamba atwishwa kuwalinda mafisadi

-Ushahidi uliommaliza waanikwa
-Ni mpasuko wa madiwani wa kinondoni

USHAHIDI uliowasilishwa katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, na Mbunge Halima Mdee, kuthibitisha tuhuma dhidi ya Yusuf Makamba kwamba amekuwa akimlinda Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Salum Londa, katika tuhuma za ufisadi ikiwamo ugawaji viwanja eneo la Kawe, Dar es Salaam, msingi wake ni mpasuko wa madiwani wasioridhishwa na mwenendo wa meya huyo, Raia Mwema imebaini.
Imebainika kuwa, madiwani hao waliwahi kumwandikia barua Katibu wa CCM, Wilaya ya Kinondoni na nakala yake kufikishwa kwa Katibu Mkuu wa CCM- Taifa, Yusuf Makamba. Barua hiyo ni yenye kumbukumbu namba MAD/MK/01/08, ya Januari 24, mwaka 2008, inatoa ufafanuzi wa tuhuma za ubadhirifu na uongozi mbovu wa Manispaa ya Kinondoni, ikierejea barua ya awali, yenye kumbukumbu namba MAD/MK/01/08.
Inaelezwa kuwa baada ya madiwani kuchoshwa na kile kinachoelezwa kuwa ni "kumlinda" Meya Londa kwa gharama za walipa kodi wa manispaa, barua hiyo ambayo Raia Mwema imepata nakala yake, iliainisha tuhuma 10 dhidi ya Londa na kuhitimishwa kwa maelezo makali: "Kwa haya machache yanathibitisha kwamba Mstahiki Londa ameshindwa kusimamia utawala bora ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni."
Barua hiyo pia inaeleza ari ya madiwani hao kutaka kuitwa kwa Katibu wa CCM - wilaya na ngazi ya taifa ili kueleza kwa kina madhambi ya Londa ikisema; "Mheshimiwa Katibu utambue kuwa tunayo ya kuzungumza katika kikao ambacho chama mtatuita, lakini kwa haya machache yanathibitisha nani mbabaishaji."
Miongoni mwa tuhuma zilizoelezwa katika barua hiyo ni kuhusu kile kilichoelezwa kuwa; "Madiwani kugundua Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni imegubikwa na wizi wa mali unaotokana na vitendo vya kughushi nyaraka za malipo (payment vouchers).
"Juni, 2007, kwenye kikao cha bajeti tulipitisha kasma (fungu) ya kununua matrela 25 ya kubebea taka kwa thamani ya Sh milioni nane, kila moja baada ya zabuni kutangazwa na mshindi kupatikana. Lakini watendaji wa manispaa wakiwa na baraka za Mstahiki Londa walighushi nyaraka na kuongeza bei kutoka milioni nane hadi milioni 12. Matrekta hayo yakaagizwa tena kwa Sh milioni 15.5.
"Katika kikao cha kamati ya madiwani ya chama (CCM) Januari 7, mwaka 2008, Londa alitetea malipo hayo akidai walipwaji walisahau kuweka Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) walipowasilisha zabuni yao. Swali la kujiuliza hapa ni je, tangu lini VAT ikawa asilimia 50?''
Tuhuma nyingine inahusu ununuzi wa magari, ikidaiwa kuwa magari 15 aina ya Suzuki yalinunuliwa bila kuzingatia taratibu za ununuzi zinazotaka zabuni itangazwe kwanza na kuwa na profoma zaidi ya tatu.
Sehemu nyingine ya tuhuma katika barua hiyo inahusu uuzaji wa mali chakavu ya Manispaa ya Kinondoni na barua hiyo inaeleza; ''Mstahiki Londa aliamuru gari alilokuwa akitumia aina ya Toyota Land Cruiser GX ambalo lilikuwa kwenye orodha ya kupigwa mnada, likarabatiwe kwa kiwango cha juu kwa fedha za Manispaa na matengenezo yaligharimu Sh milioni 9, baada ya matengenezo hayo alilazimisha auziwe gari hilo kwa sh milioni 3.

Soma zaidi

1 comment:

Anonymous said...

its possible you are aware of this already but, i typed out a
huge comment and it got erased, why was that?

Also visit my page ... Debenhams.co.uk Vouchers