Tuesday, October 27, 2009

Bunge lamuapisha mrithi wa Mwanyika

BUNGE la Tanzania limemuapisha, Frederick Werema, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Werema ameapishwa leo saa tatu asubuhi hivyo, kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania amekuwa sehemu ya Bunge.

Werema ameapa kuwa atakuwa muaminifu kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, ataitumikia kwa moyo wake wote, ataihifadhi, atailinda, na kuitetea Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete alimteua Werema kuchukua nafasi ya Johnson Mwanyika.

MKUTANO wa 17 wa Bunge la Tanzania umeanza leo mjini Dodoma.

No comments: