Thursday, April 30, 2009

TANESCO yaingizwa katika kashfa mpya


-CAG abaini malipo tata ya mabilioni

-Ni yanayolipwa kampuni ya Songas

-Sasa Bunge kuwasha moto mpya

UTATA mpya umeibuka katika mkataba wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO) ukihusu shirika hilo la umma na kampuni ya kuzalisha umeme ya Songas Limited, iliyolipwa kila mwezi zaidi Sh Bilioni tano katika mazingira yanayotia shaka, imefahamika.

Fedha hizo ni zile zilizolipwa na TANESCO kila mwezi kwa ajili ya kununua umeme kutoka kampuni ya Songas Ltd ya Dar es Salaam, ikiwa ni malipo ya ‘capacity charges’ zinazoelezwa kwamba si sahihi, na zimelipwa katika mazingira tata.

Kutokana na hali hiyo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, amependekeza kupitiwa upya kwa mkataba huo unaotajwa kumalizika muda wake miaka 25 ijayo, yaani mwaka 2024. Bunge linatarajiwa kuazimia kumuunga mkono CAG kuhusu suala hilo.

Hatua hiyo ya Bunge inatokana na taarifa ya CAG ya ukaguzi wa Mashirika ya Umma kwa mwaka wa fedha 2007/2008 ndani ya TANESCO, shirika ambalo linaaminika kuwa katika matatizo makubwa ya kifedha lakini likiwa na mianya mingi ya kupoteza fedha, hususan katika ununuzi wa umeme kutoka kampuni binafsi au zenye ubia na Serikali.

Soma zaidi

No comments: