Monday, April 20, 2009

Wangekuwa na Robo tu ya Sifa za Nyerere…

Wiki jana muhimu na ya aina yake si tu kwa sisi tunaosisimshwa na kuhamasishwa na maisha ya Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere; bali Watanzania wote kwa ujumla. Ni wiki ya tamasha la kumuenzi Mwalimu Nyerere.

Miongoni mwa wanazuoni maarufu duniani ambao wamekuja Dar es Salaam kushiriki tamasha hili linaloendelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ni mshindi wa tuzo ya Nobel, Profesa Wole Soyinka, mtoto wa Nkwame Nkrumah anayeitwa Gamal Nkrumah na mtoto wa Frantz Fanon (mtunzi wa The Wretched of the Earth) anayeitwa Olivier Fanon, kwa kuwataja wachache.

Kwamba miaka kumi baada ya kifo chake wanazuoni mashuhuri kutoka sehemu mbalimbali duniani wanasafiri na kuja nchini kujiunga na wenzao (kina Shivji) kuhudhuria tamasha hili la kumuenzi, ni ushahidi wa wazi kwamba Nyerere alikuwa zawadi ya pekee ya Mungu kwa Watanzania, na kamwe fikra zake hazitakufa kabisa kwa wapenda haki na amani duniani. soma zaidi.

No comments: