Tuesday, April 21, 2009

Tunaungana na Prof Soyinka juu ya Kuwakosoa Viongozi wetu

Wiki iliyopita katika 'Wiki ya kazi za Kitaaluma za Nyerere' pale UDSM mambo mengi yalizungumzwa na kuazimiwa kutekelezwa katika kuelekea Afrika moja yenye maendeleo ya kweli kwa wananchi wake. Jambo moja muhimu ambalo sisi kama wanaharakati hatuna budi kuliwekea mkazo ambalo Prof. Wole Soyinka aliligusia ni pamoja ule uwezo wa wananchi kuwakosoa viongozi wao na viongozi kukubali kukosolewa kama njia ya kujirekebisha na kufanya vizuri zaidi katika siku za usoni. Katika Afrika yetu ya leo yenye matatizo mengi- ukosefu wa huduma za msingi za afya, barabara, maji, umeme, shule, rushwa iliyokithiri, uongozi mbovu, ukiukwaji wa haki za binadamu, ukatili wa kijinsia na n.k Kwa nini Viongozi wetu wakatae Kukosolewa? soma zaidi.

No comments: