Friday, April 24, 2009

Kigoda cha Mwalimu: Ni wakati wa umma kuongoza

TAMASHA la Kigoda cha Mwalimu Nyerere, limemalizika kwa mafanikio makubwa. Chuo kikuu cha Dar es Salaam, kimeweka historia isiyofutika.

Heshima ya chuo hicho iliyovuma miaka ya sabini na wakati wa mapambano ya ukombozi wa nchi za Afrika zilizokuwa zikikaliwa na wakoloni na Makaburu, imerudi kwa kasi mpya.

Vijana wanauliza: Leo hii tunawaimbia sifa za Mwalimu; tunawaimbia fikra za Mwalimu na mchango wa Mwalimu wa kuikomboa Tanzania na kuzikomboa nchi nyingine za Afrika; tunawaimba wimbo wa Nkrumah na wanamapinduzi wengine wa Afrika; wimbo wa utumwa na Ukoloni: Je wao watawaimbia wimbo gani watoto wao na wajukuu wao?

Kwa lugha nyepesi, swali la vijana ni je, sisi kizazi chetu kimefanya nini? Kigoda cha Mwalimu, ambacho hapo baadaye kitaratibu masomo ya Umajumuhi wa Afrika, ni jibu la swali la vijana wa Tanzania na vijana wa Afrika!

Tamasha hili lilikuwa na matukio mengi; mengine ya kuburudisha, kufurahisha, kufundisha na kutafakarisha, lakini mengine ya kusikitisha. Ni vigumu kuyaandika yote hapa. Ni imani yangu kwamba mengine yataandikwa au yameandikwa tayari na kuchambuliwa na wengine. Mimi nitaongelea machache ambayo yaliugusa moyo wangu na niliyaona kama changamoto kubwa:

Soma zaidi

No comments: