Thursday, April 30, 2009

Mwakyembe kulipua bomu la Kiwira bungeni



-Ben Mkapa kuguswa

WAKATI wowote kuanzia leo, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe atawasilisha hoja binafsi kuhusu mgodi wa Kiwira ili kuwatetea wafanyakazi wa mgodi huo ambao hawajalipwa mishahara yao kwa zaidi ya miezi 10, hali inayowafanya kushindwa kumudu gharama za maisha.

Dk. Mwakyembe amelazimika kuchukua hatua hiyo ambayo imekubaliwa na uongozi wa Bunge hususan Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah kutokana na kile kinachoelezwa kuwa shinikizo la wafanyakazi hao kwa mbunge wa eneo ulipo mgodi huo.

Wafanyakazi wa mgodi huo ambao wamepunjwa malipo ya mafao yao na kutolipwa mishahara kwa zaidi ya miezi 10 sasa, wanadai wamefikia hatua hiyo kutokana na ukimya wa Serikali katika kushughulia matatizo hayo.

Soma zaidi

No comments: