Friday, June 1, 2012

CAG akosoa mfumo wa bajeti

MKAGUZI Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovic Utouh ameitaka serikali kubadili mfumo wake wa kutoa bajeti kwani bado ni mbovu.

Utouh pia aliionya serikali kuwa makini katika kuanda bajeti yake kwa kuwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita haikufanya vizuri katika usimamizi wa fedha.
Utouh aliyasema hayo katika kikao cha mwisho cha uwajibikaji  kilichofanyika jijini Dar es salaam juzi .

 “Kwa mfumo huu tuliokuwa nao kunahitajika mabadiliko ya haraka kuweza kunusuru nchi yetu bila hivyo kila  siku bajeti zitakuwa mbovu tu”alisema Ludovick.

Alieleza kuwa kufikia malengo hayo kunahitajika mabadiliko kwa wananchi na serikali kujua bajeti kwa usahihi kabla hazijapitishwa katika bunge.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha za Hesabu za Serikali (PAC) Joh Cheyo  alisema  wabunge wameonyesha uwezo wao kuangalia mahesabu ya serikali kwa umakini na siyo kwa upinzani,hivyo ni dhahiri kuna mabadiliko na siku za nyuma.

Cheyo alieleza kuwa mkutano uliokuwa ukielendelea kwa siku tatu umewapa mwangaza zaidi wa kuliangalia Taifa kwani wamepata changamoto kutoka kwa wageni waliotoka nchi za jirani na kuhudhuria kwa kutoa ushauri na majadiliano.

“Tumepata uzoefu kwa wageni toka Uganda, Malawi na Sudan kwa kweli wametupa changamoto za maswali na ushauri”alisema Cheyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mashirika ya Umma Zito Kabwe alisema kuwa wananchi wameona hatua iliyo chukuliwa na serikali katika swala la uwajibikaji,hivyo ni vyema kuwa makini katika swala hilo kunusuru Taifa.

“Htimaye wananchi wameona hatua zilizo chukuliwa na serikali kwa swala la uwajibikaji, ni vyema kujifunza kabla hayaja kukuta makubwa” alisema Zito.

Zito alifafanua kuwa huu siyo muda wa kukaa na kuongelea mambo yaliyo pita bali ni wakati mzuri wa kuundwa sheria za utekelezaji wa bajeti.

No comments: