Thursday, April 28, 2011

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Uchambuzi wa seria ya KILIMO KWANZA,Ajira, Biashara na Maisha Endelevu

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), umezindua muhtasari ya uchambuzi wa sera ya KILIMO KWANZA: Maana na umuhimu wake kwa jamii iliyoko pembezoni, Wanawake, Wanaume wa Tanzania na Ajira, Maisha endelevu na Biashara
Muhutasari huu umelenga kutoa uch ambuzi yakinifu wa sera za serikali na mgawanyo wa bajeti katika sekta hizi mbili muhimu. Ajira na Maisha Endelevu na Kilimo, kwani zina mahusiano ya karibu na maendeleo ya wanawake walioko pembezonina wanaume; na ni kitovu cha kampeni yetu ya: “Haki ya Uchumi: Rasilimali ziwanufaishe wanawake walioko pembezoni.


Kila muhtasari wa uchambuzi wa sera tulioufanyia kazi uliuliza maswali kadhaa kuwa ni kwa kiasi gani sera hizi zinaweka vipaumbele mahitaji muhimu ya wanawake hasa wa kipato cha chini wa vijijini na mijini sio tu kinadharia bali kwa mikakati imara ya mgawanyo sawa wa rasilimali?
Idadi kubwa ya wanawake wa Kitanzania wanategemea kilimo cha mikono kwa maisha endelevu, kama chanzo cha kujipatia kipato, pia kama chanzo cha chakula cha kila siku kwa familia na jamii. Pia idadi kubwa ya wanawake na wanaume bado imeendelea kutegemea sekta ya kipato isiyo rasmi kama chanzo cha kujipatia kipato kwa ajili ya mahitaji ya kila siku kwa wote wanaoishi vijijini na mijini
TGNP katika uchambuzi huu wa sera hizi mbili, tumeona


kuwa sera na bajeti zinaweka kipaumbele madai na mahitaji ya makampuni makubwa ya nje na ndani kama msingi wa kuendesha na kukuza biashara ya nje. Kutokana na kipaumbele hiki umuhimu wa kusimamia ukuaji wa uchumi wa Taifa kwa kujitegemea umesahaulika pamoja na mkakati wa maendeleo ya wananchi wenyewe.


Lengo kuu la sera ya KILIMO KWANZA ni kuweka nguvu kwa wazalishajiwakubwa kwa kuwapa kupata vipaumbele kutoka serikalini hasa katika maeneo ya mikopo, misamaha ya kodi, ruzuku na nyinginezo. Pia wamekuwa wakitumia njia hiyo kudai soko huria katika ardhi, umiliki wa ardhi, kwa kigezo kuwa watawafikia wananchi wa hali ya kawaida walioko vijijini.


Changamoto kubwa katika sera hii ya sasa ya KILIMO ni jinsi inavyoonekana kukubali na kuukabiribisha mfumo mpya wa matumizi ya mbegu zilizorekebishwa – “genetically modified seeds” (GM), maarufu kama “mbegu za miujiza” (Miracle Seeds), unaolenga kuzalisha mbegu za mazao katika maabara, kilimo cha mazao ya nishati (Biofuel), matumizi makubwa ya mbolea za viwandani na madawa ya kilimo.

Uchambuzi uliofanywa kuhusu mfumo huu hapa Afrika na Asia umeweka wazi athari na changamoto za tekonolojia hii ya uzalishaji mbegu inayomlazimisha mkulima mdogo kuwa na majukumu makubwa kinyume na uwezo wake. Mfumo unaelekeza nguvu zake katika kilimo kikubwa wakati walengwa ni masikini. Hatua hii inapelekea mashirika makubwa yanayojihusisha na kilimo na biashara kunufaika kupitia ukodishaji wa mashamba, uuzaji wa pembejeo, madawa na mbolea na kuwaacha wakulima masikini mikono mitupu.

Wakati mwingine hawa ndio wamekuwa wananunuzi wa kubwa wa mazao yanayozalishwa kwa kulangua, mabenki makubwa pia yameonesha kunufaika zaidi kuliko mwananchi masikini kutokana na kudai riba kubwa katika mikopo ya kilimo hasa hiki cha uzalishaji wa mbegu.
Mfumo huu wa mbegu za GM umekuwa kikwazo kwa wakulima wadogo kwa sababu hawawezi kuhifadhi mazao yao ili kuandaa mbegu kwa ajili ya msimu unaofuata, kwa hiyo unawalazimisha wakulima wadogo kuendelea na mtindo wa kununua mbegu madukani kila mwaka badala ya kuzalisha za kwao kwa njia za asili. Athari nyingine ni matumizi ya zana kubwa katika kilimo kinachotumia mitambo na mafuta, hivyo kusababisha makampuni makubwa ya mafuta kujiingiza humo, kama wanufaika wakubwa na hivyo kujenga nguvu kubwa ya ushawishi ya kuendeleza aina hii ya kilimo.


Ili kutimiza hili, sehemu ya ardhi ya kilimo cha chakula lazima itumike, na hivyo mkulima kulazimika kugawa muda wake kati ya kilimo cha mazao ya biashara ambayo serikali inayataka (na kwa yeye kupata fedha kulipia kodi), na kilimo cha chakula kwa ajili ya familia yake.
Kwaupande mwingine kukimbilia teknolojia hii, serikali inajivua wajibu wa kumwendeleza mkulima mdogo na kufungua milango kwa masetla; hivyo kumfanya abaki kibarua kwenye ardhi yake aliyoirithi.


Mfumo wa GM umekuwa ukishinikizwa Tanzania na nchi jirani na Jumuiko la Mapinduzi ya Kijani Kibichi Afrika, (AGRA), Ukuzaji wa Kilimo katika mwambao wa Kusini na mashirika makubwa ya kilimo cha biashara. Banki ya StanBanki na kampuni za Monsanto, SAB Miller, Diageo, Syngenta na General Mills, wamewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye kilimo ambacho hakitoi usalama wa chakula wala ajira kwa Watanzania, bali ni kunufaika katika kuuza chakula nje na mzao ya nishati mbadala na kuongeza bei ya chakula katika soko la ndani.


Uchambuzi wetu wa Sera ya Ajira, Maisha na endelevu na Biashara umeongozwa na swali je,ni mikakati gani imewekwa ya kuongeza Ajira na maisha endelevu kwa Watanzania wote wanawake na wanaume? Mtazamo wa serikali na mwelekeo wake umeonekana kuwa ni kuangalia vikundi vidogo vya uzalishaji ambavyo hata hivyo wanaonufaika nao ni wanawake na wanaume wajasirimali wenye uwezo walioko mijini wakati walio wengi vijijini wakiwa wameachwa.
Kwa sasa idadi kubwa ya wanawake na wanaume wa vijijini na mijini wamenyang’anywa kila fursa ya uzalishaji kwa ajili ya maisha endelevu, kama vile ardhi, maji, misitu, nk. Athari hizi ni matokeo ya unyang’anyaji wa ardhi za wananchi, mikakati ya mipango miji, kukimbizwa na kufukuzwa kwa wamachinga, vibanda vidogo, bomoa bomoa na kuingiza ardhi katika biashara huria. Wakati huo huo mfumo wa uchumi kuuza mazao nje ya nchi bila mkakati mathubuti ya kuendeleza soko la ndani unaendelea kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha tabaka kati ya masikini na tajiri kwa wote wanaoishi vijijini na mijini.


Katika mkanganyiko huu wanawake wanakumbana na changamoto zaidi zinazotokana na mfumo dume ulioko serikalini na katika taasisi za kijamii kwa kupata nafasi chache za ajira, mikopo, ardhi, na elimu kuliko wanaume.
Kwa mfano katika kiwango cha asilimia 14 ya masaa yote ya ya siku wanawake huwa wanafanya kazi isiyo na malipo, wakati wanaume ni asilimia 5 tu ya muda wao hutumika kufanya kazi za nyumbani zisizo na malipo. Utafiti wa kitaifa wa soko la ajirawa mwaka 2006, uliainisha kwamba asilimia 66 ya wanaofanya kazi kama wasaidizi kwenye familia bila malipo ni wanawake. Wakati huo huo, taratibu wa kumiliki na kurithi ardhi ya familia unaendelezwa kwa kufuata mfumo dume wa mila na desturi ambazo zinawanyima haki wanawake.
Wanaharakati wa kifeministi wanaamini kuwa Watanzania wote wanaume na wanawake wana haki sawa ya kupata ajira na maisha endelevu. Kufikia ajira kwa wote kunategemea mabadiliko ya kisasa katika mikakati ya maendeleo sera za nchi.

Imetolewa na:
Usu Mallya
Mkurugenzi Mtendaji

3 comments:

Anonymous said...

It's a pity you don't havе a donate button! I'd definitely donate to this fantastic blog! I guess for now i'll ѕеttle for boоκ-maгking and adԁing your RSS
fееd to my Googlе acсount.
I look foгward to fгeѕh updаtes and will sharе this sitе with my Fасebook group.
Tаlk sοon!

Αlso vіsit my ωeb blog - xxx penis dick Cunt Vagina
my web page > xxx penis dick cunt vagina

Anonymous said...

Greetings! Very useful advice within this post! It is the little changes that produce the biggest changes.
Thanks for sharing!

Look at my web blog :: diets that work

Anonymous said...

A fascinating discussion is worth comment. I believe that you need to write more
about this issue, it may not be a taboo matter but usually people do not talk about these topics.
To the next! Best wishes!!

My page Visit Website