Tuesday, April 5, 2011

Pinda: Kutahiri wanaume kunapunguza kasi ya Ukimwi

Kampeni ya kupambana na Ukimwi nchini imeendesha mpango wa majaribio wa kutahiri wanauwe watu wazima waliokuwa hawajawatahiriwa ikiwa ni njia ya kupunguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo,.

Tayari jumla ya wanaume 31,432 wamekwishatahiriwa nchini chini ya mpango huo unaotarajiwa kuenezwa katika mikoa minane nchini yenye kiwango cha juu ya maambukizi, ifikapo mwaka 215.

Hayo yalisema na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati akizindua rasmi Mkakati wa Taifa wa Kinga ya Ukimwi (2009 - 2012) pamoja na Mpango Kazi kuhusu Jinsia na Uukimwi (2010 – 2012) Ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Uzinduzi huo ulishuhudiwa pia na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dkt. Asha Rose Migiro ambaye anatembelea Tanzania na aliyefuatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloratibu mapambano ya Ukimwi (UNAIDS), Michel Sidibe, na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Alberic Kacou.

Nchini Tanzania baadhi ya wanaume hutahiriwa na wengine huwa hawatahiri kulingana na tamaduni mbalimbali na kwamba kitaalamu kutotahiri kunaongeza kasi ya maambukizi ya Ukimmwi.

Kwa mujibu wa utafiti, kasi ya maambukizi ya Ukimwi imepungua Tanzania kati ya mwaka 2003 na 2008, kutoka asilimia saba hadi asilimia 5.7, ambayo ni idadi ya watu karibu watu milioni moja, ambao asilimia 10 ni watoto wadogo.

Mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya na Iringa ina kasi kubwa ya maambukizi ya zaidi ya asilimia tisa, kwa mujibu wa utafiti huo.

Waziri Mkuu alisema pia kwamba bado Tanzania ina maambukizi mapya kwa watu 90,00 kila mwaka na kwamba alipozindua Uchunguzi wa Hali ya ukimwi nchini mwaka 2009, alielekeza TACAIDS kufanyakazi na tawala za mikoa ili kutengeneza mipango ya uzuiaji wa ukimwi kulingana na mahitaji na hali ilivyo katika kila mkoa.

CHANZO: NIPASHE

No comments: