Friday, January 30, 2009

MREJESHO WA SEMINA (GDSS) YA TAREHE 28/1/2009

UTANGULIZI:
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umejiwekea utaratibu wa kufanya muendelezo wa semina za jinsia na maendeleo kwa kila siku za jumatano (GDSS),ambazo hufanyika makao makuu ya ofisi za mtandao huo zilizopo Mabibo jijini Dar es salaam.
Semina hizi zina lengo la kupeana taarifa, kujengeana uwezo na kuibua mijadala ya masuala mbalimbali katika jamii ni kwa watu wote bila kujali jinsia, umri, rika, kabila, kiwango cha elimu au utafiti kwa mshiriki.

TAREHE:-
Semina hii ilifanyika jumatano ya tarehe 28/1/2009.

MADA:-
Tathmini miaka kumi (10) ya sheria ya makosa ya kujamiiana (SOSPA) 1998-2008.

MWEZESHAJI:- Kaka Venant William, kutoka TGNP.

MAHUDHURIO:-
Washiriki waliohudhuria GDSS hii walikuwa kama ifuatavyo:-
Wanawake: 50
Wanaume: 38
Jumla: 88

KUHUSU WASHIRIKI:-
Washiriki wa semina hii walikuwa ni wanachama wa semina za jinsia na maendeleo (GDSS), wafanyakazi wa mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) na wananchi kwa ujumla.

MJADALA KWA UFUPI:-
Baada ya mrejesho kutoka kwa washiriki wa semina kuhusu kumbukumbu ya mada zilizotolewa juma lililopita na watoa mada Bi. Ananilea Nkya kutoka (TAMWA) na Bi. Scholastika Jullu kutoka (WLAC) kuhusu historia fupi iliyopelekea msukumo wa kutaka kutungwa kwa sheria ya makosa ya kujamiiana, mafanikio pamoja na changamoto kuhusu (SOSPA) mwanzoni mwa miaka ya tisini 1990.
Washiriki waliyataja baadhi ya mambo yaliyopelekea msukumo wa kutaka sheria hii kutungwa kuwa pamoja na:-

•Athari za utandawazi kuanza kuibuka.
•Madhara ya ukimwi kuanza kuonekana wazi zaidi.
•Kushamiri kwa vitendo vya kishirikina (Ramli).
•Ukosefu wa haki hasa kwa wanawake na watoto.
•Mgawanyo mbaya wa rasilimali katika jamii.

MJADALA KWA UREFU:-
Mjadala ulilenga zaidi katika changamoto na nini kifanyike kuhusiana na sheria hii ya makosa ya kujamiiana (SOSPA) hasa baada ya waziri wa sheria na mambo ya katiba kutoa tamko kwa umma kupitia vyombo vya habari kuwa wanaharakati walishinikiza sheria mbaya ya makosa ya kujamiiana mwaka 1998 na kusema kuwa inapingana na sheria ya ndoa ya mwaka 1971 na kutamka azma ya serikali kuifanyia mabadiliko haraka iwezekanavyo.
Washiriki walisema pamoja na sheria kuonyesha makali yake, lakini hali imezidi kuwa mbaya sana kwa sasa maana vimezuka vitendo vingine vingi zaidi vyenye kumdhalilisha zaidi mwanamke na mtoto.Waliyataja baadhi ya mafanikio kuwa ni pamoja na:-
•Kutiwa hatiani kwa wahalifu wengi wa makosa ya kujamiiana toka kuanzishwa kwa sheria hii miaka kumi (10) iliyopita, takriban robo tatu (¾) ya wahalifu wanatumikia adhabu katika magerezani mbalimbali nchini.
•Sheria imewezesha ulinzi kupatikana kwa wanawake wengi zaidi na watoto nchini.
•Kupungua kwa vitendo vya ukeketaji. Takwimu zimeonesha kuwa mwaka 2006 vitendo hivyo viliripotiwa kupungua kwa zaidi ya asilimia ishirini (20).
•Kupungua kwa vitendo vya kidhalilishaji/bughudha dhidi ya wanawake.

CHANGAMOTO;
Kwa miaka kumi iliyopita ya utekelezaji wa sheria hii changamoto kadhaa zilizo orodheshwa, nazo ni pamoja na:-

•Ukali wa sheria bado haujawa tiba ya matatizo kwa wote wanaoshiriki katika vitendo vya ubakaji/udhalilishaji.
•Kumekuwapo na tabia ya kutokuwajibika kwa wana jamii na hususan katika jeshi la polisi linapokuja suala la utekelezaji wa sheria hii (SOSPA).
•Kukosekana kwa utu miongoni mwetu kunakopelekea msukumo mdogo wa kuleta mabadiliko chanya katika jamii.
•Mila,desturi na tamaduni zetu bado ni tatizo katia utekelezaji wa sheria hii.
•Miongozo ya dini katika masuala ya ndoa itazamwe upya kwa maana katika baadhi ya dini humnyima mwanamke.

NINI KIFANYIKE?;
Baada ya mjadala wa kina mapendekezo kadhaa yalitolewa na wana GDSS pamoja na wana jamii kwa ujumla kuhusu nini kifanyike kwa mustakabali wa sheria hii na kutaka;

•Tamko la kumtaka waziri wa maendeleo ya jamii,jinsia na watoto Mh. Magreth S. Sitta kwa umma kuhusu mfanikio ya sheria ya makosa ya kujamiiana SOSPA ya mwaka (1998).
•Waziri wa sheria na mambo ya katiba Mh. Mathias Chikawe aombe radhi kwa tamko alilolitoa kuhusu SOSPA.
•Wana GDSS kuandaa tamko na kulitoa rasmi jumatatu tarehe 2/2/2009 kwa umma kupinga kauli iliyotolewa na waziri wa sheria na mambo ya katiba kuhusu SOSPA.
Na katika kutoa tamko hili, timu ya watu wa nane (8) iliundwa na washiriki wa semina ili kuwawakilisha wenzao.
Washiriki hao ni:-

1. Esther Jackson.
2. Nuru Ruksan
3. Eva Nganda
4. Subira Kibiga
5. Eliab Maganga
6. Badi Darussi
7. Pius Manyama
8. Titus Ntanga

HITIMISHO:-
Wakati wa kufanya hitimisho la semina ilikubaliwa na wote kuwa yote yalioazimiwa yafanyiwe kazi kikamilifu na ifikapo jumanne ya tarehe 3/2/2009 kuwe na jibu kamili la maazimo ili kabla ya kuanza GDSS ya wiki ijayo utolewe mrejesho wa yote tuliyokubaliana.

4 comments:

Anonymous said...

Hi to every body, it's my first visit of this web site; this website includes remarkable and in fact fine stuff designed for readers.

my blog post: online graduate certificate programs

Anonymous said...

Sweet blog! I found it while searching on Yahoo News.

Do you have any suggestions on how to get listed in Yahoo News?
I've been trying for a while but I never seem to get there! Appreciate it

My blog post :: www.realestateinformations.com

Anonymous said...

Hi there friends, good piece of writing and pleasant arguments commented at this
place, I am truly enjoying by these.

Also visit my page; Read Full Report

Anonymous said...

Inсredible! This blog looκs exactly liκе my old
one! It's on a entirely different topic but it has pretty much the same page layout and design. Great choice of colors!

Also visit my web blog :: herbal party pills