Tuesday, January 20, 2009

Mkakati wa GDSS 2009 kwa mtazamo wa ukombozi wa mwanamke kimapinduzi.

MUHTASARI WA SEMINA.
(GDSS)

TAREHE:- Semina hii ilifanyika jumatano ya tarehe 14/1/2009.

MADA:- Mkakati wa GDSS 2009 kwa mtazamo wa ukombozi wa mwanamke kimapinduzi.

WATOA MADA:
Anna Mushi - mtoa mada mkuu (TGNP
Lilian Liundi – mtoa mada mshiriki (TGNP).

MWEZESHAJI:- TGNP
MJADALA KWA UFUPI:-
Baada ya salamu na kutakiana heri ya mwaka mpya, utambulisho wa mada ulifuata na fursa kwa washiriki kuelezea mikakati yao kwa mwaka 2009 kuhusiana na namna watakavyo shiriki katika kuendeleza vuguvugu la ukombozi wa mwanamke kimapindizi.

MALENGO KUTOKA KWA WASHIRIKI:-
• Kufanya ushawishi kwa wanawake wengi zaidi kuja kuhudhuria katika semina za GDSS ili kupanua wigo wa harakati za kumkomboa mwanamke.
• Kuhakikisha tekinolojia inamkomboa mwanamke.
• Kufanya maandalizi madhubuti katika kuhakikisha ufanisi wa tamasha la jinsia mwezi wa tisa (GF).
• Kutoa elimu zaidi kuhusu VVU na UKIMWI katika mikoa ya Singida na Dodoma.
• Kuhakikisha kilio cha yatima na wajane kinasikika vilivyo katika jamii.
• Kuandika habari/ makala nyingi zaidi zitakazowezesha ukombozi wa mwanamke.
• Kufanya ufuatiliaji wa kina kuhusiana na masuala ya huduma ya afya.

MJADALA KWA UREFU:-
Baada ya kumalizika kwa zoezi hilo, mtoa mada aliwataka washiriki kujigawa katika makundi matatu (3) na kujadili nini kifanyike ili kuboresha (GDSS) kwa mtazamo wa kumkomboa mwanamke kimapinduzi na kutoa mapendekezo matatu(3) yatakayojadiliwa kwa kina na kupata mapendekezo ya pamoja kwa utekelezaji zaidi.

MREJESHO:-
Baada ya mjadala wa kina kutoka kwa washiriki, yafuatayo yalikubaliwa kwa utekelezaji ili kukamilisha malengo ya washiriki katika kusukuma mbele vuguvugula ukombozi wa mwanamke kimapinduzi kwa mwaka 2009.


• Utunzaji wa kumbukumbu.
• Kutoa elimu ya nini maana ya ukombozi wa mwanamke kimapinduzi.
• Kujitolea.
• Kuanzisha semina za maendeleo na jinsia (GDSS) katika maeneo yetu.
• Kufanya tathmini ya mara kwa mara kuhusu shughuli zetu.

HITIMISHO:-
Wakati wa kufanya hitimisho la semina, mambo matatu (3) yalijiri;
• Hitaji la kuwepo kwa kauli mbiu itakayo tumika kama utambulisho na kichochea hamasa kwa wana GDSS katika shughuli zote za kiharakati.
• Ushiriki wa watoto katika semina za maendeleo na jinsia (GDSS) na shughuli nyingine za kiharakati, maana uzoefu umeonyesha kuwapo na mkanganyiko ambao kwa hakika unahitaji ufumbuzi wa haraka.
• Hitaji la matumizi ya vyombo vya habari hasa television katika kuongeza hamasa kama ilivyokuwa awali ambapo (AGAPE TV) ilitumika kufanya hivyo mwaka 2007.

Mwisho washiriki walikumbushwa kuhusu faida za kufanya kazi kwa ushirikiano ambapo walielezwa kuwa kutawaletea tija haraka na baadaye kusisitizwa kualika watu wengi zaidi kushiriki katika semina zetu.

No comments: