Thursday, February 11, 2010

Nguza Viking na mwanae papii wafungwa maisha.wawili waachiwa huru

Mahakama ya Rufaa Tanzania mapema leo imewaachia huru watoto wawili wa Mwanamuziki nyota wa muziki wa dansi hapa nchini Nguza Viking (Nguza Mbangu wa pili kulia na Francis Nguza wa mwisho kulia) huku yeye mwenyewe pamoja na mtoto wake Papii Kocha wakifungwa maisha.Baadhi ya Watu wamesema kuwa kutokana na kutolewa kwa hukumu hiyo mpaka sasa njia inayoweza kuwaokoa ni kwa Mh. Rais kutoa msamaha kwa makosa waliyoyafanya ya kubaka . Rufaa hiyo ilikuwa ikisikilizwa na Jaji Masati wa mahakama kuu ambapo hukumu hiyo imesomwa na Neema Chusi Naibu msajili wa mahakama ya Rufaa hukumu.Aidha hali ya Mahakamani hapo kwa ndugu na jamaa zao walishikwa na butwaa kwa kile kilichotokea huku wengi wao wakilia kwa uchungu.

No comments: