Friday, February 5, 2010

BREKING NYUUUUUUZZZZZ: JERRY MURO NA WENGINE WAWILI WATINGA KIZIMBANI LEO

Mtangazaji wa TBC Jerry Muro na watu wengine wawili, Edmund Kapama na Deogratius Ngassa, wamepanda kizimbani mchana huu wakikabiliwa na mashataka kadhaa likiwemo la kula njama kutaka kupokea rushwa.

Mbele ya Hakimu Gabriel Mirumbe, Jerry Muro na washtakiwa hao wawili walishtakiwa kwa pamoja kwa kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 toka kwa mweka hazina wa wilaya ya Bagamoyo aliefukuzwa kazi hivi karibuni na Waziri Mkuu kwa ubadhirifu Bw. Michael Wage.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali Boniface Stancilaus akiwa na Mwendesha Mashtaka toka TAKUKURU Benny Lincolin wamedai mahakamani hapo kwamba mshtakiwa wa kwanza na wa pili pia wanakabiliwa na shtaka la kujipachika wadhifa ambao sio wao.
Inasemekana January 29, 2010 katika hoteli ya Sea Cliff washtakiwa walijitambulisha mbele ya Wage kuwa wao ni maafisa wa Takukuru wakati sio kweli.

Upande wa mashtaka uliiomba mahakama usitoe dhamana hasa kwa washtakiwa wa kwanza na wa pili kwa madai kwamba waliwahi kufungwa huko nyuma na kuwa kwao nje kutaharibu upelelezi ambao haujakamilika na bado unaendelea.

Hakimu alipowataka kutoa uthibitisho kwamba washtakiwa hao waliwahi kufungwa huko nyuma upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha hivyo dhamana ikawa wazi kwa m ashartia ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili wataosaini bondi ya milioni 5 kila mmoja, ama kwenda rumande hadi Februari 12, mwaka huu kesi itaposomwam tena.

Jerry Muro na Edmund Kapama
walitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa.
Ngassa atapelekwa rumande.

No comments: