Wednesday, February 10, 2010

Halmashauri kupatiwa fedha za kununulia dawa

WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii imekubali wazo la kupeleka fedha katika Halmashauri kwa ajili ya kununulia dawa.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk Aisha Kigoda amesema, Serikali inafanya tathmini ili kupata namna ya kudhibiti matumizi ya fedha hizo.

Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa ametoa wazo hilo bungeni wakati anauliza swali la nyongeza na kuiuliza Serikali kama haiwezi kupeleka katika Halmashauri asilimia 20 ya fedha za kununulia dawa ili zinunue popote kwa ajili ya wananchi badala ya kusubiri dawa kutoka Bohari ya Dawa(MSD).

Dk Kigoda amewaeleza wabunge kuwa, MSD imekasimu madaraka zaidi kwa bohari za kanda ili kuimarisha mfumo wa usambazaji wa dawa, vifaa tiba, na vitendanishi.

No comments: