Thursday, February 4, 2010

Msekwa alia na Spika Sitta

WAKATI Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi ikitarajiwa kupokea, Jumatano ijayo, taarifa ya Kamati ya Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi inayotafuta njia ya kumaliza msuguano ndani ya chama hicho, mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa, ameelezwa kutaka Spika wa Bunge Samuel Sitta achukuliwe hatua, Raia Mwema limefahamishwa.

Habari za ndani ya CCM zimeeleza kwamba Msekwa, ambaye alipoteza nafasi yake ya Uspika baada ya kushindwa na Sitta, amekuwa akionyesha waziwazi kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya Sitta na wabunge wanaomuunga mkono katika vita dhidi ya ufisadi.

Hata hivyo, Msekwa amekuwa akipata pingamizi kutoka kwa wajumbe wenzake, akiwamo Mzee Mwinyi, na Spika wa kwanza wa Baraza la Kutunga Sheria la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Abdurahaman Kinana.

Wakati Kinana ameelezwa kuwa na msimamo mkali zaidi akitaka pande zote husika zichukuliwe hatua kulingana na uzito wa tuhuma, kwa watuhumiwa wa ufisadi kushughulikiwa kukisafisha chama na Sitta na wenzake kukemewa, Mzee Mwinyi amekuwa akielezwa kutumia busara zaidi kutoa maoni yake.

“Msekwa alisema wazi kwamba matatizo ya sasa yasingekuwapo kama Sitta angechukuliwa hatua na vikao vya CCM vilivyoandaliwa mahususi kumshughulikia, lakini Mzee Mwinyi akamwambia chama hicho tawala hakiendeshwi kwa jazba,” anasema mtoa habari wetu ndani ya CCM.

Soma zaidi

1 comment:

Anonymous said...

Ni wivu tu unaomsumbua Msekwa hapo, alipomshinda kwenye kugombea uspika ndio chanzo cha yote hayo.

Mwana GDSS