Monday, October 31, 2011

Mbunge: TGNP saidieni wagombea wanawake majimboni

Wajumbe wa kamati ya Bunge ya kudumu ya Huduma za Jamii wakimsikiliza Mkurugenzi wa TGNP Usu Mallya ( hayupo pichani)

Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Juma Mtanda akizungumza

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Usu Mallya akiwaelezea Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma za jamii shughuli za TGNP

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP) umetakiwa kuwawezesha wanawake wanaojitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi hasa Ubunge na Udiwani majimboni ili washinde.

Wakizungumza katika ofisi za TGNP wabunge wa kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya jamii wamesema TGNP inalojukumu la kuwasaidia kwa kuwajengea uwezo wagombea wanawake watakaojitokeza kugombea ili waweze kujiamini na hata ikiwezekana kwapatia rasilimali za kuwawezesha kuwashinda wanaume.

Idadi ya Wabunge waliochaguliwa kwenye majimbo imengozeka kutoka 12 mwaka 2000, hadi 17 mwaka 2005 na katika uchaguzi wa mwaka 2010 wamefikia wabunge 20. Sawa na asilimia 36 ya wabunge wote.

Mbunge wa Jimbo la Nkenge,MKoani Kagera Mchangaji Asumpta Mshana (CCM) amesema kuwa hata yeye binafsi ameshinda katika jimbo hilo kwa taabu kutokana na kupambana na mgombea aliyekuwa waziri na mwenye nguvu kubwa.

“Wanawake tunapomua kugombea tunashindwa kutokana na tatizo la rasilimali hasa fedha, unakuta wanaume wanatumia fedha nyingi wakati sisi hatuna kitu, tutawezaje kushinda? TGNP wekeni mkakati wa kuhakikisha Mwanamke atakayesimama kugombea anapata msaada wa kujengewa uwezo na hata raasilimali”

“Mimi nilisimama na Waziri, ilikuwa kazi kwelikweli, wanawake wachache tumeshinda kwasababu wananchi walipima ni kitu gani tutakipata tukimpa huyu mwanamke,…”alisema Mshana

Mshana aliitaka TGNP kwa kupitia Chuo chake cha Mafunzo ya Jinsia (GTI) kuwaelimisha wabunge wanawake juu ya uchambuzi wa bajeti kwa mtazamo wa kijinsia ili wakati wa Bajeti ya serikali wabunge wote wanawake wasimame kudai bajeti yenye usawa wa kijinsia ambayo haimbagui mwanamke na mwanamme masikini.

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu Mallya aliwaeleza wabunge hao kuwa TGNP ni shirika huru lisilofungamana na siasa wala dini, na ni shirika la mfano kwa hapa nchini ambalo mwanachama wake akijihusisha na siasa anaacha kuwa mwanachama mara moja.

Mallya alitoa mfano wa Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) na Waziri Kivuli wa Wizara ya Jinsia, wanawake na watoto Naomi Kaihula, na Naibu waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, utamaduni na Michezo, Dk. Fenela Mkangala, ambao kwa Pamoja mwishoni mwa mwaka jana walijitoa kwenye Bodi ya Shirika baada ya kujiingiza kwenye siasa na kuchaguliwa kuwa Wabunge.

Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Said Mtanda, aliomba TGNP kutoa mafunzo elekezi kila mwaka mara moja kwa wabunge kwaajili ya kujifunza masuala ya bajeti, sera na mauala mengine ya kijamii yanayoweza kuwasilishwa Bungeni.

“Ipo haja ya TGNP kukutana na kamati hii na kupatiwa semina elekezi, mtupatie mafunzo ya jinsia, tunapokaa Bungeni tuweze kuyaelezea, mtupatie maarifa ili tuweze kutoa maoni ya wadau.

No comments: