Wednesday, February 23, 2011

Wanaowatoza fedha watoto, wajawazito na wazee kukiona

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri wabunge au mtu yeyote mwenye majina ya wahusika katika hospitali za Serikali wanaowatoza fedha wazee, akina mama wajawazito na watoto wampelekee ili wahusika washughulikiwe.

Mwanri amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, wenye majina ya watu hao wampe ili Serikali ibanane nao.

Mwanri alikuwa anajibu swali la nyongeza la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyedai kuwa watoto na wazee wanatozwa fedha wanapokwenda kupata tiba.

Kwa mujibu wa Mwanri ni sera ya serikali inaagiza kwamba, wazee, akina mama wajawazito na watoto wasitozwe fedha wanapokwenda kupata tiba.

Kwa mujibu wa Lissu, akina mama wanapowapeleka hospitali watoto wanadaiwa sh.5,000 na wazee pia wanatakiwa kutoa kiasi kama hicho ili wapate tiba.

Awali, wakati anajibu swali la msingi la Mbunge wa Vunjo, Augustino Mrema, Mwanri alisema, hospitali mpya ya wilaya ya Moshi iliyotokana na kupandishwa hadhi kwa kituo cha afya cha Mji Mdogo wa Himo inatarajiwa kuanza kutoa huduma kwa wagonjwa wan je Mei mwaka huu.

No comments: