
Nilihuzunika baada kunieleza historia ya maisha yake, pia nilijiuliza maswali mengi, je, ingekuwa mimi nakumbana na tatizo hili ningekaa kimya au ningewaeleza wenzangu? Je, marafiki, wazazi na jamii kwa ujumla wangelipokeaje tatizo langu ingawa mimi mwenyewe nimeshaamua kulitangaza ili nipate msaada? Binafsi sina uwezo mkubwa wa kumsaidia Salama lakini naamini watu mbalimbali pamoja na wahisani, wataguswa na habari hii na kumsaidia kwa kuwa licha ya kuwa anaishi na VVU, pia ana watoto watatu na mjukuu mmoja.
Salama ni mtu mwenye haiba, huwezi kuamini kuwa anaishi na VVU mpaka alipojitangaza kuwa na hali hiyo, umati uliokusanyika pale Mabibo katika Viwanja vya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Siku ya Maadhimisho ya Mwanamke Duniani, inayofanyika Machi 8 kila mwaka. Isome zaidi habari hii kwa kubofya hapa.
No comments:
Post a Comment