Wednesday, March 2, 2011

TGNP YAADHIMISHA WIKI YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI NA MIAKA 50 BAADA YA UHURU

Mmoja wa jopo la watoa mada akiwasilisha mada yake

Mwenyekiti wa TGNP Bi. Mary Rusimbi akitoa muktadha na kuwakaribisha watu waliofika katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani


Wanaharakati wakiserebuka baada ya kuvutiwa na burudani ya kikundi cha sanaa cha Parapanda


Mtoa mada Bi. Anna Mushi kutoka TGNP akiwasilisha mada yake


Bi. Asseny Muro ambaye ni mwanachama mwanzilishi wa TGNP akimkaribisha mwenyekiti wa TGNP Bi. Mary Rusimbi kufungua maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kwa niaba ya Mkurugenzi wa TGNP

Wanaharakati wakifuatilia mada kwa makini


Mwenyekiti wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Mary Rusimbi akiongea na waandishi wa habari wa kutoka vyombo mbalimbali kuhusu kuelekea kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani na miaka 50 baada ya uhuru na pia kutafakari juu ya maisha ya wanawake kwa kuzingatia elimu bora na kipato endelevu. Mary Rusimbi amebainisha kuwa siku ya wanawake duniani ni kutafakari miaka 100 ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani katika ustawi wa mwanamke wa kitanzania kiuchumi na kijamii, kuainisha michango, mapambano ya wanawake miaka 50 baada ya uhuru na kubainisha changamoto zinazowakabili kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na kupanga mikakati ya baadae, kutandaa na kupashana habari.












No comments: