Thursday, March 10, 2011

Mfanyabiashara adaiwa kumnajisi mtoto

MFANYABIASHARA Joseph Mathew (40), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam akidaiwa kumnajisi mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 10.

Mbele ya Hakimu Wilberforce Luhwago, Mwendesha Mashitaka Sakina Sinda alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Machi 3 mwaka huu, saa 2 usiku katika mtaa wa Narung’ombe wilayani Ilala.

Alidai kuwa kwa makusudi mshitakiwa alimuingilia kinyume na maumbile mtoto huyo (jina limehifadhiwa) na kumsababishia maumivu.

Mshitakiwa alikana mashitaka na kurudishwa rumande hadi Machi 24 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena. Katika hatua nyingine, watu watano wamefikishwa katika Mahakama hiyo kwa tuhuma za kuiba vifaa vya umeme vyenye thamani ya Sh 694,000 zikiwemo nyaya.

Washitakiwa hao ni Omary Issa (23) mkazi wa Kiwalani, Nuhu Idrisa (23) mkazi wa Kariakoo, Christopher Mwaitobe (36) mkazi wa Yombo, Juma Ally (20) mkazi wa Jangwani na Hamis Salim (20) mkazi wa Tandika.

Ilidaiwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Luhwago kuwa Machi 4 mwaka huu saa 10 jioni katika mtaa wa Lindi, washitakiwa hao walipanga njama na kuiba mali hizo.

Washitakiwa hao walikana mashitaka na kurudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini, na kesi hiyo itatajwa tena Machi 24 mwaka huu.

Hivi karibuni kumezuka tabia ya watoto wadogo kufanyiwa ukatili wa namna
mbalimbali ikiwemo kubakwa, kama jamii unaliongeleaje hili?

No comments: