Friday, January 29, 2010

Sitta na Lowassa wagongana tena


-Kamati ya Mwinyi yawashindwa
-Ujasusi watumika kuwinda vigogo wa CCJ

KIWEWE cha kuanzishwa kwa Chama Cha Jamii (CCJ) kinachohusishwa na baadhi ya vigogo maarufu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinashika kasi huku kamati ya wazee iliyoongozwa na rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, ikishindwa kumaliza makundi kama ilivyokusudiwa, blogu yetu imefahamishwa.

Habari za ndani ya CCM na Serikali zinaeleza kwamba kamati ya Mzee Mwinyi imekumbana na vizingiti kadhaa kutokana na baadhi ya vigogo wa juu wa chama hicho kuanza kutegeana katika kufikia makubaliano ya kumaliza tofauti zao.

Tayari CCJ kinaelezwa kuwa chama ambacho kitategemea zaidi matokeo ya kamati ya Mzee Mwinyi na baadhi ya wachambuzi wamekwisha kuonyesha kuwa chama hicho ambacho hata usajili wa muda hakina, kimeitikisa vilivyo CCM ambayo viongozi wake wamekuwa wakitoa kauli za kukiponda.

Pamoja na kuwapo makundi manne ndani ya CCM, makundi mawili ndiyo yanayotajwa kuwa chachu ya misuguano ndani ya chama hicho, yakiongozwa na wanasiasa wawili wazito, Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa kiasi kwamba Kamati ya Mwinyi imekuwa ikiyazingatia zaidi makundi hayo katika kazi yake.

Kundi jingine ndani ya chama hicho ni la viongozi wastaafu ambao ni pamoja na mawaziri wakuu wastaafu; Dk. Salim Ahmed Salim na Jaji Joseph Warioba na Frederick Sumaye ambalo linaelezwa kuwa na nguvu kubwa inayowaumiza vichwa wakubwa ndani ya CCM kiasi cha kuanzisha propaganda ya kuwahusisha wastaafu hao na CCJ.

Soma zaidi

No comments: