Thursday, January 28, 2010

MSWADA WA SHERIA YA GHARAMA ZA UCHAGUZI




Jana katika mfululizo wa Semina za kila siku ya Jumatano mada iliyojadiliwa ni kuhusu mswada wa sheria ya gharama za uchaguzi mwezeshaji bw. Hebron Mwakagenda aliukosoa mswada huo kwa kushindwa kuweka ushindani ulio sawa katika uchaguzi kwa mfano:- Wakati CCM ikipata ruzuku ya Shilingi bilioni moja kuna baadhi ya vyama havipati kabisa ruzuku hiyo mfano CHAUSTA na vinginevyo.
Kwa hiyo mswada huu unalenga kuua demokrasia iliyopo na kuendeleza mfumo mbaya wa utawala.

Katika maoni yake mchangiaji mada Bw. Eliab Maganga alisema mswada huu unalenga kuleta matabaka nchini kwani sehemu kubwa ya vyama vya siasa nchini vinapata msaada kutoka nchi wahisani hivyo mswada huu kuzuia vyama hivyo kupata misaada ni sawa na kuwagawa watanzania kivipato na kushindwa kugombea nafasi mbalimbali nchini kwani wenye nacho tu ndio watakaoweza kushiriki katika chaguzi mbalimbali nchini.

No comments: