Wednesday, October 13, 2010

Udasa yaandaa mhadhara wa Nyerere

Jumuiya ya wanataalima ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(Udasa) kwa kushirikiana na Taasisi ya Mwalimu Nyerere, wameandaa mhadhara utakaofanyika kesho kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 11 ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Mhadhara huo utafanyika chuoni hapo, katika ukumbi namba moja wa Nyerere.

Dk. Kitila Mkumbo, Makamu Mwenyekiti wa Udasa, alisema jana kuwa mada kuu itakayojadiliwa ni ”Mawazo ya Nyerere katika suala la uongozi”.

Aidha, Dk. Mkumbo alieleza kwamba jopo la watu wanne limeandaliwa kuzungumzia maeneo mbalimbali yanayoendana na mada hiyo, ambao ni Jenerali Ulimwengu,Dk. Adolf Mkenda, Joseph Butiku na Dk. Azaveli Lwaitama

Wakataohudhuria ni mabalozi toka katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Afrika kwa ujumla, wanataaluma na wadau toka katika nyanja tofauti.

No comments: