Tuesday, July 28, 2009

Mjadala kuhusu mgodi wa Kiwira

Hivi juzi tu serikali ilitoa tamko rasmi kuhusu mjadala mkubwa wa mgodi wa kiwira ulioibua hisia na jazba bungeni na wananchi wa kawaida kwa takribani mwaka sasa.

Serikali imetamka rasmi kuwa Mkapa na Yona ambao ndio walionunua mgodi huo kwa bei ya kutupa ya shilingi za kitanzania milioni 70 watarejeshewa gharama zao walizotumia kuukarabati ambazo zimekadiriwa kufikia shilingi bilioni mbili za kitanzania.

Hii ni sawa kwa kiongozi kutumia madaraka yake vibaya na kisha baada ya kugundulika afidiwe gharama?

Viongozi hawa walistahili wachukuliwe hatua za kisheria au warejeshewe gharama zao zinazodaiwa kutumika kwenye kuendesha mgodi huo?

Jadili!!

No comments: