Tuesday, March 31, 2009

Tujikumbushe ya rada, tusijesahau

SASA imedhihirika kwamba Mkataba wa Ununuzi wa Rada wa mwaka 1999, kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Uingereza ya BAE Systems, uligubikwa na rushwa kubwa, kwa mujibu wa Ofisi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya nchini Uingereza – Serious Fraud Office (SFO).

Wapelelezi wa ofisi hiyo juu ya mkataba wa ununuzi wa chombo hicho kwa Sh. bilioni 40 wamekuwa wakipeleleza kampuni hiyo na washukiwa wanane, wakiwamo Waingereza wanne - Sir Richard Harry Evans (67), Michael Peter Rouse (61), Michael John Turner (61), John Aldridge (52), na Watanzania watatu (majina tunayo, umri miaka 63, 44 na 45).

Katika taarifa yao ya awali ya Machi 2008, walisema: “Kuna kila sababu kuamini kwamba watu wote hao na Kampuni ya BAE Systems walitenda makosa ya rushwa katika ununuzi warada hiyo”.

Wakibainisha jinsi sehemu ya mavuno ya rushwa hiyo yalivyogawanywa kupitia benki mbili za kigeni, kati ya Juni 19, 1997 na April 17, 1998, taarifa hiyo inasema hivi kuhusu Wa/Mtanzania hao/huyo: “SFO inahitimisha kwamba kuna kila sababu na kwa ushahidi tosha kwamba kwa kufanya hivyo (watu/mtu hao/huyo) alikuwa akiuweka uchumi wa Tanzania hatarini”.

Ni dhahiri pia kuwa Serikali inawajua watu hao nao wanajijua; na ingekuwa kwa Nchi Zilizoendelea, zenye kuheshimu dhana ya kuwajibika, wangekuwa wameachia ngazi zamani kuponya nyuso zao. Lakini si kwa Mtanzania, ambaye kwake wizi, ubadhirifu na ufisadi ni ushujaa wa kupokelewa kwa kutandikiwa zulia jekundu.

Ningekuwa mimi ndiye Rais, ningewashauri watu hao kuachia ngazi kiungwana ili kutoipaka tope serikali yangu. Ningekuwa mimi ndimi mshukiwa, nafsi yangu ingenisuta na kujiuzulu sawia. Huu ndio uungwana; huu ndio ustaarabu wa binadamu, wa kuweka mbele maslahi ya walio wengi, tofauti na wanyama kama Nyang’au, wanaoweka maslahi binafsi mbele kwa maana ya “Rule of the Jungle”- Kanuni za mwituni”. Na haya yanapotokea, tuliowaweka kusimamia serikali, wako wapi?. Au wametusahau kwa kujichongea mzinga wa asali?

Tabia ya kikundi cha viongozi wachache ya kulishwa asali kidogo na wawekezaji kwa kutumia mamluki wa ndani, ili kutetea manunuzi na uwekezaji usio na maslahi kwa taifa, inaendelea kuitafuna nchi. Tumejionea hili kwa mradi wa IPTL, ununuzi wa ndege mbovu ya Rais, mbuga za wanyama (Ortello), Richmond, mikataba ya madini na sasa Dowans, bila kusahau sakata hili la Ununuzi wa Rada.

Miradi yote hii imethibitika kuwa bomu la maangamizi kwa Taifa kiuchumi na kijamii. Na kwa nguvu ya fedha ya kifisadi, imeweza kuingiza “wateule” Bungeni, Chama tawala, Taasisi nyeti za serikali na serikali kuu. Ndiyo maana kero za wananchi hazipati majibu kutokana na jeuri za kifisadi, eti kwamba “dua la kuku halimpati mwewe”.

Ungekuwa mmoja wa waliotetea ununuzi wa rada na ndege ya Rais kwa maneno makali ya kutunisha mishipa ya shingo; kisha unagundua kwamba kwa kufanya hivyo uliudanganya umma, ungefanyaje? Ungekuwa na ujasiri tena kusimama kadamnasini, macho makavu, na kuusalimia umma unaoteseka kiuchumi kwa ulaghai wako?.

Rais Richard Nixon wa Marekani, kwa ustaarabu, alijiuzulu urais kwa kashfa ya Watergate. Naye Waziri Mkuu wa Israeli, amejiuzulu hivi karibuni kwa kashfa ya rushwa; wengi walipita njia ulimwenguni, kwa ustaarabu wao; wewe je? Utetezi wa matusi kwa kujificha ndani ya mbawa za chama kinalisaidia nini Taifa lako?.

Rushwa ya mtu mmoja ni mbaya vya kutosha, lakini Serikali nzima inapohusishwa na rushwa kwa matendo ya wachache ndani yake wasioguswa, kwa sababu tu wanaonekana kukipenda chama tawala kuliko Taifa, hili si jambo la kufumbia macho.

Tuangalie mfano wa sakata la rada. Wakati hoja ya utapeli wa mkataba huo ilipoibuliwa na wapinzani, Naibu Waziri wa Fedha, Abdulsalaam Issa Khatibu; Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mark Mwandosya na Mkurugenzi Mkuu wa Kurugenzi ya Usafiri wa Anga, Margareth Munyangi, ndio waliokuwa wa kwanza kutetea mradi huo wakisema: “Rais hawezi kudiriki kamwe kuacha usalama wa wasafiri wa ndege, mikononi mwa bahati nasibu”.

Hakuna aliyekuwa akipinga hili, bali kilichopingwa ni bei kubwa na ubora hafifu wa kifaa hicho mtumba, kwa sababu tayari jumuiya za kimataifa na Waziri Clare Short wa Uingereza, walikwishaonya na kuitahadharisha Serikali juu ya ulaghai wa dili hilo. Kwa nini hawakuamka kwa tahadhari hiyo?

Naye Rais Benjamin William Mkapa, kwa kuambukizwa na watu waliomzunguka, na pengine kwa kutumia Chama, akiwa ziarani Mbeya alitetea ufisadi huo akisema: “Wanaoikosoa Serikali si tu wanaibeza Serikali na Chama chake, bali wanawabeza Watanzania waliokipatia Chama cha Mapinduzi mamlaka ya kutawala kwa wingi wa kura (bila kujali zilivyopatikana) ili kiweze kutekeleza ilani na sera sahihi, zenye kulenga kumletea maendeleo mwananchi….. Hao ni vipofu na viziwi”.

Baada ya kuthibitika kwamba ndege ya Rais na rada aliyokuwa akitetea ni mabomu na kikwazo kwa maendeleo ya mwananchi; kati ya yeye na hao aliowaita eti ni vipofu na viziwi, ni yupi aliyekuwa akiwabeza Watanzania?.

Tangu mwanzo, Baraza la Mawaziri la Uingereza lilikuwa limegawanyika juu ya Uingerza kuiuzia Tanzania ndege mbovu, licha ya kwamba zoezi zima lilikuwa la udanganyifu. Waziri wa Fedha, Gordon Brown (sasa ni PM) na Mama Clare Short, Waziri wa Ushirikiano na Misaada ya Kimataifa, Mashirika ya Oxfam, Benki ya Dunia, Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Shirika la Kimataifa la Usalama wa Anga (ICAO), Jane’s Air Traffic Control na wengine, wote waliweza kubainisha mapema juu ya udanganyifu wa mkataba huo, kiasi kwamba Benki ya Dunia ikatishia kuzuia misaada kwa Tanzania.

Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair, alijua yote haya; lakini aliishinikiza Kabineti yake imruhusu kutoa kibali cha mauzo kwa BAE Systems ili kuokoa ajira za Waingereza 280 wa Kampuni hiyo, iliyopo katika kisiwa cha Isle of Weight, ili Chama chake kisipoteze ushindi katika jimbo lililohusika. Rais Mkapa alipeleka salaam kwa Blair, kumshukuru kwa kuweza kuifanya Serikali yake iidhinishe mauzo ya mtambo huo mbovu chini ya mkataba wa kitapeli.

Juni 21, 2002 Waziri wetu wa Fedha wa wakati ule, Basil Pesambili Mramba, katika kauli iliyoonekana kutowakilisha maslahi ya Taifa, alitamka Bungeni maneno yafuatayo ambayo itawachukua Watanzania muda mrefu kuyasahau: “Tunakataa kuambiwa mambo yakufanya hata kama sisi ni masikini … Wanawezaje kuwa na ujasiri wa kutuambia kwamba rada hiyo ni aghali sana kwetu?... Tuko tayari kula majani, na kama wanataka, waache kutupa misaada yao”.

Kuonyesha kwamba hoja za wananchi hazikuwa na uzito kwake, Mramba, kwa wakati tofauti, alisema: “Baadhi ya watu wanaokota okota maneno baa na kuyafanya wimbo rada … rada … rada kwa kujisumbua; hawajui kwamba Serikali ya Uingereza imekwishatoa leseni ya kuiuzia Tanzania rada; na kinachotokea Uingerza sasa ni mgogoro ndani ya Serikali ya huko ambayo wanataka kuuleta katika Serikali ya Tanzania”.

Mramba na wenzake waliilewa vizuri Kampuni ya BAE Systems na malengo yake; kwani wakati huo ilikuwa imekumbwa na kashfa ya madai ya kutoa rushwa kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, baada ya nchi hiyo kutiliana sahihi mkataba wa kampuni hiyo kuiuzia silaha za kijeshi. Na kufuatia upelelezi wa SFO, kama inavyofanya hapa kwetu kwa sakata la rada, ilibainika kuwa BAE Systems, iliweka Pauni za Kingereza milioni saba katika Akaunti ya Mifuko (Trusts) huko Jersey, katika Visiwa vya Channel, na kutokana na uchunguzi zilimilikiwa na Waziri huyo.

Baada ya kuonekana mambo yanamwendea vibaya, Waziri huyo aliutema mfupa, akalipa Pauni milioni sita kwa mamlaka za utawala wa visiwa hivyo kama fidia ya usumbufu walioupata kutokana na upelelezi huo, na kwa maelewano ya kusimamishwa kwa upelelezi.

Kwa kufanya hivyo, inaweza kutafsiriwa kuwa, ama Waziri huyo alikuwa anautema mlungula kwa nafsi yake kumsuta, au naye alikuwa anatoa rushwa ili upelelezi usitishwe.

Hakuna shaka yoyote sasa kwamba wabeba mikoba ya ufisadi wa rada ya Tanzania, wanafahamika kwa mujibu wa taarifa ya SFO kwamba: “There is every reasonable cause to believe that all the above named persons and Company have committed offences of corruption …. The SFO concludes to believe that in taking this stance….. (name/s) was putting the economic interest of Tanzania at risk”, ni maneno ambayo tafsiri yake tumeitoa hapo mwanzo.

Je, kwa taarifa hii ya SFO, wahusika wa kashfa ya rada nao sasa wanaweza kuitema milungula kama alivyofanya Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar; au watazuia wasiwajibishwe, au Sheria kuchukua mkondo wake, kwa nguvu ya fedha walizo nazo? Hivi ni mpaka SFO waje Tanzania ndipo tubaini vitendo vya ufisadi vyenye kuangamiza uchumi wa nchi yetu?

Source: www.raiamwema.co.tz

3 comments:

Anonymous said...

yapo mambo mengi sana ya kufuatilia katika nchi hii ili kuweza kuiweka sawa. Pasipo sababu ya msingi mambo yanapindishwa-pindishwa na hatua za uhakika hazichukuliwi dhidi ya wahusika wa skendo kadhaa za ulaji wa "njuluku" za taifa. Lakini pamoja na harakati zao za kutaka kufunkika baadhi ya kweli hilo halitawezekana kabisa, siku zinakuja ambapo ukweli tupu utabaki hadharani... Mwisho wa Ubaya ni aibu!

Anonymous said...

We seem to forget so easily so fast, it is almost shocking!

Let me give you some recollection and food for thought.

"The Tanzanian Government has defended its decision to buy a new air traffic control system from the United Kingdom. Tanzanian Foreign Minister Jakaya Kikwete tells the BBC's File on Four editor David Ross why he is puzzled by the furore."

:

http://www.ntz.info/gen/b00413.html - you can google further for all these details - they are all over!!
Quote:

Tanzania responds to air traffic furore

The Tanzanian Government has defended its decision to buy a new air traffic control system from the United Kingdom. Tanzanian Foreign Minister Jakaya Kikwete tells the BBC's File on Four editor David Ross why he is puzzled by the furore.

The controversy over the contract hit the headlines towards the end of December.

There were even reports of splits in the UK cabinet, with ministers such as International Development Minister Clare Short angry at the government's decision to grant BAE Systems an export licence for the $39.5m (£28m) system.

Critics claim it is too expensive for Tanzania's needs and is intended for military as much as civilian use.

But, speaking on the BBC's File on 4 programme, Mr Kikwete maintains there was no need for the fuss.

We are not a department of the World Bank - we are a country and it's a bit insulting to suggest that we need to wait for the World Bank to prescribe what's best for us

Tanzanian Foreign Minister Jakaya Kikwete

"Our engineers prescribed the system which we required", he says.

"We put the contract out to tender, four companies competed and we got BAE Systems delivering to our specification. This is the system we wanted."

Which is fine except for the background against which the contract became public.

Debt relief

Tanzania is one of the poorest countries in Africa, and one of only four countries in the world to have had a portion of its international debt written off - a total of $3bn (£2.1bn) which will be discounted over the next 20 years.

The relief will make a healthy dent in Tanzania's total international borrowings of more than $7bn.

Tanzania: one of the poorest countries in Africa

It was confirmed only after the Government in Dar es Salaam signed an agreement with the World Bank to implement the conditions of a so-called Poverty Reduction Strategy Paper (PRSP).

Under the PRSP specific targets will be met for improvements across a wide range of social issues.

These range from infant mortality and increased access to education and health, to the provision of more roads and clean water supplies.

'Insulting'

Critics of the air-traffic control deal say the $39.5m (£28m), borrowed at a reported interest rate of 4.9% from the UK's Barclays Bank, could have been better used to fund clinics or schools.

Even the World Bank has quietly demurred and is still reviewing the contract.

Foreign Minister Kikwete is adamant that it is not anyone else's business how his government elects to prioritise spending.

"We are not a department of the World Bank - we are a country and it's a bit insulting to suggest that we need to wait for the World Bank to prescribe what's best for us," Mr Kikwete said.

"The responsibility for Tanzania is in the hands of Tanzanians."

Benefits?

But the debate does not end with air traffic control and it raises fundamental questions about the overall benefits of the debt relief package.

Primary school education improved as part of debt package

One of the conditions to which the Tanzanian Government had to agree was greater access to education - all primary aged children will be in schools with class sizes under 50 in the next five years.

As part of that agreement, basic primary school fees have been abolished.

But the cost of these reforms will be $600m - and nearly half of that will have to be financed by further loans from the World Bank.

The government has also signed up to borrowing another $65 million from the Bank to fund agricultural improvement through a project which will provide subsidised seeds and fertiliser.

Critics question the wisdom of this. They say the project is modelled on a previous, smaller-scale scheme which collapsed and warn that it will do little to build a viable and sustainable agricultural sector.

In both these cases the Tanzanian Government hopes that its new borrowing will be paid for out of increases in gross domestic profit.

The World Bank and IMF predict that the necessary 6% growth in the country's economy is achievable.

But, for Kevin Watkins, Policy Director at Oxfam, the risk is that the benefits of debt relief will be wiped out by the government's need for further loans to fund reform.

"I think these are very fundamental questions. These are scarce financial resources and it's imperative that recipient governments are seen to direct those resources to areas where they will have a real impact on human development," Mr Watkins said.

Back in the foreign ministry, Mr Kikwete acknowledges a paradox in Tanzania's situation.

His government now needs to meet targets on social reform in order to qualify for help with its previous debt.

The spending on reform is likely to drive Tanzania further into debt.

But Mr kikwete says his country has little choice.

"What else do you do? If there were better conditions we would take them.

"But if these are the conditions, then this is the world we are in and this is the reality we have to understand. We are biting the bullet."

File on Four 4 is broadcast on Tuesday 29th January on BBC Radio 4 at 2000GMT and repeated on Sunday at 1700GMT.

End Quote:


Who is the defender of this nation really? Ask yourself and act on the answers.

Anonymous said...

In fact, if they were to be listed, your eyes go dehydrated, and
eventually die. It's as well an exercising that a big cover, you but pauperism to tinge an field of your cutis tissues between the ovolo and the Index finger feel. An increasing phone number of ladies are Gainful attention to their is enough to afford cosmetics aimed at reducing Cellulite a pellet. hormonal changesAccording to Delavier, the growth and Appearance of cellulite is as roly-poly and Salty foods can drive cellulite.

My blog post cupping massage cellulite