Wednesday, November 14, 2012

Tamasha la 2 la Jinsia ngazi ya wilaya - Mkambarani 2012



Mtandao wa Jinsia Tanzania [TGNP] kwa kushirikiana na Mitandao ya Wanaharakati wa Masuala ya Jinsia, Haki za Binadamu na Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi wanawaletea Tamasha la 2 la Jinsia katika ngazi ya Wilaya.

MADA KUU Ya mwaka huu ni: Haki ya Uchumi: Ni Suala la Kikatiba , Rasilimali Ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni  

Tamasha hili litafanyika  Morogoro Vijijini,  Mkoa wa Morogoro katika viwanja vya Moseka vilivyoko Mkambarani nje kidogo ya mji wa Morogoro.

 Kuanzia  Tarehe 21-23  Novemba  2012 ,  SAA 3 ASUBUHI HADI – SAA 10 JIONI

Ushiriki ni wa  wazi kwa watu binafsi, vikundi, taasisi, mashirika na mitandao mbalimbali.   Unaweza kushiriki kwa njia ya kutoa burudani – ngoma, nyimbo maigizo, mashairi, visa mkasa, maonesho, kuandika na kuwasilisha mada kwa njia mbalimbali,kualika na kufadhili ushiriki wa watu wengine.

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Waratibu wa Tamasha
Simu 0754 362373 au 0754 613082 au andika barua pepe anna.sangai@tgnp.org, festa.andrew@tgnp.org


Wanawake, Shika Hatamu , Leta Mabadiliko!

WOTE MNAKARIBISHWA!

No comments: