Wednesday, September 30, 2009

Pinda akataza ununuzi wa magari ya kifahari


WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amewaagiza watendaji wa Serikali watafute namna ya kupunguza matumizi ya fedha za umma ikiwa ni pamoja na kutonunua magari ya kifahari.

Amewataka watendaji hao wabadilike, waache ubinafsi, na wasijifikirie wao tu, kuna mamilioni ya watanzania wanaohitaji fedha kidogo zilizopo.

Waziri Mkuu ametoa mfano kuwa, katika Wizara za Serikali kuna magari mengi ya aina ya Toyota Land Cruiser VX yanayouzwa kati ya Sh milioni 160 hadi 220 na kwamba Tanzania sin chi ya neema kiasi cha kutaka ufahari kiasi hicho.

“Watanzania hembu tubadilike, kuna watu kule chini wanahitaji hizi fedha kidogo tulizonazo” amesema Waziri Mkuu.

Pinda amesema, Serikali isiponunua magari hayo ya kifahari kwa miaka miwili au mitatu maisha ya watanzania yatabadilika kwa kuboresha kilimo na sekta ya mifugo.

Waziri Mkuu amesema, kuna mtazamo usio sahihi miongoni mwa watumishi wa Serikali, viongozi ni wabinafsi, na kwamba, wanajifikiria wao tu.

“Lakini mindset za watanzania bado bado kweli kweli” amesema Waziri Mkuu mjini Dodoma, wakati anafungua mkutano wa siku tatu wa Watendaji wa Serikali na wadau wa sekta ya mifugo.

4 comments:

Anonymous said...

you love this? HYnkoWpY [URL=]replica designer handbags[/URL] for more detail ZPRPqKxo [URL= ] [/URL]

Anonymous said...

click to view VAyIEovF [URL=http://www.replica--designerhandbags.weebly.com/]knock off designer purses[/URL] and get big save nVDCOKNQ [URL=http://www.replica--designerhandbags.weebly.com/ ] http://www.replica--designerhandbags.weebly.com/ [/URL]

Anonymous said...

view QkJLKORK [URL=http://www.ugg--outlet-online.blogspot.com/]discount ugg boots[/URL] at my estore dhJbuEMl [URL=http://www.ugg--outlet-online.blogspot.com/ ] http://www.ugg--outlet-online.blogspot.com/ [/URL]

Anonymous said...

buy a nPLjpofN [URL=http://www.ugg--outlet-online.blogspot.com/]ugg boots outlet[/URL] to take huge discount cEsFbHHE [URL=http://www.ugg--outlet-online.blogspot.com/ ] http://www.ugg--outlet-online.blogspot.com/ [/URL]