Thursday, September 24, 2009

Mwanafunzi abakwa, anyongwa Tabora

WATU wasiojulikana wamembaka na kumyonga mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Kanyenye, mkoani Tabora.

Watu hao walimbaka binti huyo, Pili Kapusha, Jumamosi wakati amekwenda kuchota maji kisimani.

Walimvamia, wakambaka, na kisha kumnyonga jirani na kisima cha maji.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, Emmson Mmari, amesema, mama mzazi wa binti huyo aliposubiri na kuona mwanawe harudi nyumbani aliamua kwenda kisimani kumfuata.

Kamanda Mmari amesema, alipofika kisimani alikuta ndoo zina maji na wakati anamtafuta alimuona ameuawa na kutupwa kwenye shimo jirani na kisima hicho kwenye kata ya Itetemya.

Amesema, ripoti ya daktari inaonyesha kuwa binti huyo alibakwa kabla ya kunyongwa.

No comments: