Friday, September 4, 2009

Tamasha la ukombozi wa Wanawake kimpinduzi kuzinduliwa wiki ijayo

Kwa mara nyingine Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) & FemAct wanayo furaha kukukaribisha kwenye Tamasha la Jinsia la mwaka
2009 litalojumuisha watu kutoka mataifa mbalimbali litakalofanyika wiki ijayo tarehe 8/9/2009 mpaka tarehe 11/9/2009 katika viwanja vya Mtandao wa Jinsia Tanzania.

Madhumuni ya matamasha ya jinsia ni kuwapa nafasi
wanamtandao na washirika wao kupeana moyo,
kutafakari, kuitathimini hali ya jinsia, kushirikishana
hatua za maendeleo na kupeana mikakati ya utekelezaji.

Unaalikwa na unakaribishwa kushiriki kwa matarajio
utakuwa kiungo muhimu katika kujenga vuvugu la nguvu
za pamoja za kuleta maisha bora kwa wanawake na
wanaume walioko pembezoni.

Kuwepo kwenye tamasha, kushiriki majadiliano,
kuhudhuria vipindi vyote bila kuchomoka chomoka ni
jambo linalotegemewa.

Wote mnakaribishwa!!

No comments: