Thursday, September 10, 2009

Wanawake jamii ya kimasai wasema "Loliondo hatuami ng’o''

Wanawake wakaazi wa wa eneo la Loliondo linalokabiliwa na mgogoro wa ardhi na mwekezaji wa kampuni ya kiwindaji (OBC) wamesisitiza kuwa katu hawataama katika maeneo yao hata kwa mtutu wa bunduki.

Akiongea na waandishi wa habari, kiongozi wa wanawake hao Bi Juliana Tipa alisema kuwa wapotayari kupambana na kikwazo chochote lakini suala la kuhama katu hawaafikiani nalo.

Aliongeza kuwa Tanzania ni nchi huru na wao ni wananchi ambao wanastahili kupewa haki zao ikiwa ni pamoja na haki ya kuishi na uhuru wa kufanya maamuzi.
Aidha kina mama hao walieleza matatizo wanayokumbana nayo katika maisha yao ya kila siku kuwa ni pamoja na kuishi maisha ya dhiki ambayo yametokana na vitisho na kuchomewa nyumba zao.

Vilevile wamebaibainisha kuwa watoto wao wanashindwa kuendelea na masomo kutokana na wazazi wao kuhamahama na kuokosekana kwa amani katika eneo lao.

No comments: