Wednesday, May 7, 2014

BUNGE LA BAJETI LAAHIRISHWA HADI AUGOSTI 5

















Bunge la Katiba linaahirishwa hii leo kupisha Bunge la Bajeti, likiwa limetumia  gharama ya karibia billion 27, za walipa kodi kwa mujibu wa Waziri wa Fedha Bi. Saada Mkuya. Ndani ya siku 67 ambayo Bunge hilo limekaa kujadili Rasimu ya pili ya Katiba, haijaweza kupitisha hata ibara moja, kati ya ibara 240. Swala la kujiuliza ni kwamba, je hizo siku 60 walizo ongezewa ambazo zitaanza August 5 mwaka huu zitaweza kuzaa matunda ama wataendelea na malumbano bila kuleta kitu cha maana kwa Watanzania. Wajumbe walioko ndani ya Bunge la Katiba wanabidi watambue kwamba fedha hizo wanazozitumia zingeweza kufanyia shughuli nyingi sana za maendeleo kama kuboresha vituo vya afya, kuongeza vituo vya elimu ama kuboresha miundombinu yetu. Hivyo, wanapaswa kutumia muda waliopewa kuujadili na kupitisha rasimu zote 240, bila ya kuongezewa muda zaidi.

No comments: