Friday, August 17, 2012

Waziri Mkuu Asema Sheria Iliyotumika Kufunga Mwanahalisi Ni Halali

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kwamba mtu yoyote ambaye anona hakutendewa haki kuhusu kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi anaweza kufafuta utaratibu mwingine wa kwenda mahakamani.

Kauli hiyo ilitolewa leo Bungeni na Waziri Mkuu Pinda wakati akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzania Bungeni , Freeman Mbowe lililouliza kuwa Julai 30, mwaka huu, Serikali ililifungua gazeti la Mwanahalisi kwa muda usiojulikana kwa kutumia sheria ya magazeti ya mwaka 1976.

Maadam katika siku za hivi karibuni serikali imetambua umuhimu wa mahakama ni

Kwanini wamelifungua gazeti hili badala ya kulipeleka mahakamani na wahusika wapate nafasi ya kujitetea kabla ya kuhukumiwa?

Akijibu swali hilo , Waziri Mkuu Pinda alisema "ni kweli serikali imechukua hatua hiyo, lakini imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi na mtu yoyote kwa msingi wa sheria hiyo kama anaona hajatendewa haki ni juu yake kutafuta utaratibu mwingine wa kwenda mahakamani,” alisema Waziri Mkuu Pinda.

Katika swali lake la nyongeza la kiongozi huyo lililouliza kuwa Sheria iliyotumika imekuwa ikilalamikiwa na wadau wengi na vyombo vya habari kwa muda mrefu . Je wewe huamini kwa kutumia sheria hiyo ni kunyima haki na ni msisitizo wa utawala usio bora?

Akijibu swali hilo Waziri Mkuu Pinda alisema “ Mimi siamini hivyo kwa sababu sheria hiyo imetungwa na Bunge tukufu na kuwa bado inatumia ni sheria halali, sisi tutaendelea kuitumia mpaka hapo itakapobadilishwa.

No comments: