Thursday, December 10, 2009

Zuma kumvisha nishani Anna Abdallah

MBUNGE wa Viti Maalumu, Anna Abdallah (CCM) ameteuliwa kupokea nishani ya Kitaifa ya Uongozi inayotolewa na Afrika Kusini.

Atakabidhiwa nishani hiyo ijulikanayo kama Order of the Grand Companions of O.R. Tambo, Silver.

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ndiye atakayemvisha nishani hiyo ya juu nchini humo; kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Bunge, Dar es Salaam.

Ilieleza kuwa barua ya uteuzi inaonesha kwamba hafla ya kutunukiwa tuzo itafanyika kesho katika Ikulu ya Afrika Kusini mjini Pretoria.

Mbunge huyo anaondoka nchini leo kwenda Afrika Kusini kupokea nishani hiyo.

Katika msafara wake, Mbunge huyo aliyewahi kuwa Waziri na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake ya CCM (UWT), atafuatana na Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shellukindo (CCM) na maofisa wawili wa Bunge, Justina Shauri na Ernest Zulu.

No comments: