Monday, December 14, 2009

'Masoko ya usiku yanaongeza kasi ya ukimwi'

MKUU wa wilaya ya Kasulu, Zainab Kwikwega, amepiga marafuku
masoko ya usiku wilayani humo yanayodaiwa kuwa chanzo cha ngono.

Inadaiwa kwamba masoko hayo yanachochea maambukizi mapya ya Virusi Vinavyosababisha Ukimwi (VVU) wilayani humo.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha Msambara wilayani humo, Kikwega alisema, utafiti wa wataalamu unaonyesha kuwa masoko hayo yamekuwa chanzo kikuu cha ngono zisizo salama zinazochangia maambukizi mapya ya Ukimwi.

Alisema, kuanzia sasa masoko yote yatafanya kazi hadi saa 12:30 jioni na pia vilabu vya pombe za kienyeji vitafungwa muda huo huo.

Kikwega amesema, lengo la kupiga marufuku masoko hayo ya usiku ni kurudisha maadili katika jamii.

Kwikwega alisema, masoko ya usiku na vilabu vya pombe vimesababisha wanajamii wasikae pamoja kujadili mambo yenye manufaa kwa familia hivyo kusababisha mmomonyoko wa maadili.

No comments: