Saturday, July 5, 2014

Tamasha la Jinsia Lafunguliwa Tarime.




Na Pendo Omary , Tarime.
Tamasha la Jinsia Limefunguliwa katika kijiji cha Ng’ereng’ere, kata ya Nyamaraga Tarime.  Mada kuu ikiwa “ Ukeketaji, Ndoa za utotoni na Haki ya uchumi”.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo, Kaimu mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Mary Nsemwa amesema, tamasha hilo ni fursa ya kuwakutanisha viongozi, wanaharakati na wananchi katika kutafakari changamoto, fursa na namna ya kuchukua hatua katika kukomesha  ukatili wanaofanyiwa wanawake na watoto wa kike kwa kuzingatia muktadha.
“Tamasha la jinsia ni jukwaa la wazi, linalowaleta pamoja watu, tasisi na viongozi kukutana na kupashana habari, kutafakari na kusheherekea  harakati hasa kwa kuangalia muktdha.” Amesema Nsemwa.
Aidha mtoa mada katika tamasha hilo, mwazilishi wa shirika la Kivulini , Maimuna Kanyamala amesema, wameamua kuongelea mada hiyo Tarime kwa sababu wanajali utu wa kila mtu bila kujali umri, elimu, dini, kabila na itikadi, ambapo wanaotendewa ukatili huo ni watoto  wa kike na wanawake ambapo ni kinyume cha haki za binadamu.
“Tunaongelea masuala haya Tarime kutokana na hali halisi ilivyo. Mkoa wa Mara unaongoza kwa asilimia 72 ya ukatili wa kimwili na kijinsia. Pia Mara ni kati ya mikoa mitatu nchini Tanzania ambayo inaongoza kwa kiwango kikubwa sana cha ndoa za utotoni,” amesema Kanyamala.
Mgeni rasmi katika Tamsha hilo, Afisa Utawala wa wilaya hiyo Baraka Nyamsenda amesema, bado jitihada zaidi zinahitajika katika kukomesha ukeketaji kwa watoto wa kike.
“Halimashauri ya wilaya ya Tarime inajitahidi kukomesha ukeketaji, lakini jitihada zaidi zinahitajika kwa sababu jamii hufanya ukeketaji kwa siri,” amesema Nyamsenda.
Tamasha hilo limefadhiliwa na Shirika linaloshughurikia idadi ya watu duniani (UNFPA) litafanyika kwa siku tatu ambapo washiriki zaidi ya 500 wanahudhuria kutoka mikoa ya Mara, Mwanza, Mbeya, Dar es Salaam, Morogoro na Shinyanga.  Washiriki wengine ni  OXFAM,

No comments: