Tuesday, August 23, 2011

TGNP YASHINDA KESI !

TGNP yashinda kesi ya Jengo
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), umeshinda keshi ya madai namba 215/1997 iliyofunguliwa na waliokuwa wapangaji wa Benki ya Uwekezaji (TIB) kabla ya jengo hilo kuuzwa kwa TGNP Juni 1997.
Jengo lenye kesi ni jengo la gorofa moja zilipo ofisi za makao makuu ya shirika Mabibo Dar es salaam,
Chini ya Mheshimiwa Jaji T.B. Mihayo, 15 Oktoba 2009, TGNP Ilishinda kesi hiyo na walalamikaji walidai kuwa TGNP imependelewa. Oktoba 19, 2009, walifungua rufaa katika makahakama kuu ya Rufaa ya Tanzania, wakiipinga hukumu ya kesi ya msngi namba 215/1997 na kukawa na kesi ya rufaa namba 129/2009 ili pia waendelee kukaa kwenye jesngo hilo.
TGNP iliiomba mahakama kufuta ombi la walalamikaji la kuendelea kuwa kwenye jengo ili shirika liweze kufanya shughuli zake, kesi ambayo ilisikilizwa na majaji watatu waheshimiwa jaji Msasali, jaji Msofe, na jaji Rutakanga Julai 22,2011.
Leo tarehe 23. 08.2011, TGNP imeamua kwa mujibu wa sheria kuwatoa kwa nguvu wapangaji hao ambao kwa muda wote wa zaidi ya miaka 10 wamekuwa wakifanya shughuli zao kwenye jengo la TGNP bila kulipa kodi wala ruhusa yetu. Pamoaja na ushindi tulioupata , bado tunaendelea kuheshimu maamuzi ya mahakama kutokana na shauri walilolipeleka mahakamani.
Sote kwa pamoja tunaamini katika haki na na rasilimali lazima zirudi kwa wananachi!
TGNP

No comments: