Friday, March 12, 2010

Rushwa ya wazi katika majimbo

MATUMIZI ya fedha kwa ajili ya kujiweka katika nafasi nzuri kuteuliwa kugombea ubunge katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) yameshika kasi miezi minne kabla ya uteuzi rasmi utakaodhibitiwa kwa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ambayo imepitishwa na Bunge hivi karibuni, badala ya kanuni za chama hicho zisizoheshimika tena miongoni mwa vigogo wake, Raia Mwema imefahamishwa.

Uchunguzi wa Raia Mwema na taarifa za ndani ya CCM na vyombo vya dola, vimethibitisha kuwa kuna majimbo katika mikoa zaidi ya 14 ya Tanzania Bara na Visiwani, ambako tayari fedha zimekwisha kuanza kutolewa kufanikisha ushindi, kila mwanasiasa kwa staili yake, baadhi wakiwa ni viongozi waandamizi wa serikali wakiwamo mawaziri, makatibu wakuu na hata maofisa wa ofisi nyeti za umma walio karibu na ‘wakubwa.’

Hali hiyo inaendelea wakati tayari utafiti wa wasomi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) ukibainisha kuwa CCM ambayo miongoni mwa ahadi kwa wanachama wake ni kutambua kuwa “rushwa ni adui wa haki,” kinaongoza katika masuala ya utoaji rushwa wakati wa michakato ya uchaguzi, na uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa umedhihirisha usugu wa chama hicho katika vitendo vya rushwa.

Utafiti huo wa UDSM, ulitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita, jijini Dare es Salaam, ukipewa jina la Mapambano ya Rushwa kwenye Serikali za Mitaa, ukigusa vijiji, vitongoji, mitaa na kata. Katika utafiti huo, CCM inaongoza katika kujihusisha kwenye vitendo vya rushwa kwa kupata asilimia 49.5, Chadema kikipata asilimia saba, CUF 2.7, NCCR-Mageuzi kikipata asilimia 0.5 kama ilivyo pia kwa TLP.

Kutokana na mkanganyiko huo, CCM makao makuu kupitia kwa Katibu wake wa Uenezi, John Chiligati imetangaza rasmi kuwa yeyote mwenye malalamiko ya viongozi kutaka ubunge kwa kutoa rushwa wakaripoti (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa) TAKUKURU moja kwa moja kwa kuwa hayo ni makosa ya jinai, yaliyo nje ya chama.

Soma zaidi

No comments: