Friday, December 10, 2010

RAIS KIKWETE AMTEUA JAJI MSTAAFU SALOME SUZETTE KAGANDA KUWA KAMISHNA WA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Jaji Mstaafu Salome Suzette Kaganda kuwa Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma.

Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar es Salaam, leo, Jumatano, Desemba 8, 2010, na Katibu Mkuu Kiongozi, Mheshimiwa Phillemon Luhanjo, inasema kuwa uteuzi huo ulianza Jumamosi, Desemba 4, 2010.

Jaji Mstaafu Salome Kaganda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mstaafu Stephen Ihema ambaye amemaliza muda wake.


Kabla ya kustaafu, Mheshimiwa Salome Suzette Kaganda alikuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Kusini, Songea.


Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

08 Desemba, 2010

No comments: