Wednesday, December 8, 2010

MICHANGO YA KUANDIKISHA DARASA LA KWANZA

Tukumbuke kwamba wakati huu ni wakati wa kuandikisha watoto kwenda darasa la kwanza. na Serikali ya Tanzania inasema au tuseme sera ya elimu inasema kwamba elimu ya msingi ni bure. lakini sasa hivi inajitokeza kuwa kila mzazi anayekwenda kumwandikisha mtoto hasa katika shule ya Msingi Bryceson huko Mburahati jijini Dar es salaam kila mzazi/mlezi anayekwenda kuandikisha mtoto anadaiwa apeleke shilingi 22,400 ikiwa ni mchango wa madawati, mlinzi, na mengineyo lakini cha ajabu risiti hazitolewi.

Je uhalali uko wapi? Halafu hili suala la kutochangia kwa maana ya elimu ya msingi bure likoje mbona kama magumashi hivi????????

Najua tukifuatilia kuna mengi mno ambayo tunaweza kuibua. Kazi kwetu!!!

No comments: