Monday, August 30, 2010

NEC kuamua rufani wiki hii

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema taarifa kuhusu rufani za udiwani na ubunge zilizopokelewa zitaanza kutolewa wiki hii.

Rufani hizo ziliwasilishwa kwa NEC na baadhi ya wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge siku chache baada ya uteuzi.

Mkurugenzi wa NEC, Rajabu Kiravu, alisema bado wanaendelea kuzijadili rufani hizo na kwamba taarifa kamili watazitoa kuanzia wiki ijayo. “Tunaendelea kuzifanyia kazi rufani tulizozipokea, hivyo siwezi kutoa taarifa nusu, wiki ijayo tunaamini tutakuwa tumekamilisha na tutatoa maelezo yake,” alisema.


Hadi kufikia Ijuma, rufani 152 zilikuwa zimepokelewa na NEC.

No comments: